Iliokua Embassy Hotel, vipi na yenyewe panaendeleaje?? Ila uwa nikikaa na kufikiria sana naona Jiji la Dar linarudi nyuma badala ya kwenda mbele. Miji yote duniani pale katikati ya jiji uwa ndio sehemu haswa ya starehe, mahoteli na ma restaurant ya nguvu, ma night clubs, mabebez usiku. Yaani watu wanatoka vitongojini wanaenda "central" kula bataz. Lakini Dar eti bataz zipo huko vitongojini ndio maana foleni haziishi. Zamani tulikua tunatoka vitongojini tunaenda ma movie Avalon, New Chox, Empress n.k na night clubs zilikua mjini. Usiku mji umechangamka, siku mjini wamebaki wahindi tu. Jiji linakufa hilo.