Moshi vijijini kunani?

Alvin Slain

JF-Expert Member
Aug 30, 2011
6,375
3,655
Jimbo la Moshi vijijini ni moja ya majimbo yenye historia ndefu sana katika halmashauri za mji wa moshi nk Likiwa na utajiri wa kutisha, lakini raia wa jimbo hili wameendelea kuwa katika mazingira yasiyoridhisha kutokana na kukosa muwakilishi sahihi katika kipindi chote ambacho Chaguzi zimekuwa zikifanyika

Mwanzoni kabisa jimbo hili kabla halijatoholewa na kupatikana jimbo la Vunjo lilikua chini ya Augustine Mrema kipindi hicho akiwa NCCR-Mageuzi, Katika mambo mengi ambayo yalifanyika katika jimbo hili, baadhi ni mradi wa KIDEFU, Mradi huo ulikua na lengo la kutengeneza barabara za kibosho,kirima,mpaka Ubwe kwa kiwango cha lami, Raia wa maeneo haya wakaletewa progam maalum ambayo iliwalazimu kukatwa shilingi 20 kila wanapoenda kuuza kahawa KNCU.

Asilimia 90 ya raia wa jimbo hili ni wakulima wa kahawa, ikumbukwe mradi huu uliifanyika Mrema akiwakilisha jimbo la Moshi vijijini na baadaye Thomas Ngawaiya akafuatia Cyril Chami na Antony Komu wote hawa walishindwa kulisemea jimbo la Moshi vijijini na hivyo mradi ule wa kidefu ukaishia njiani mpaka leo matank hayo yaliyoletwa chini ya Mrema kwa ajili ya kutengeza barabara yapo kati ya Usagara Kirima na hakuna kikichoendelea kutoka hapo, Sasa tunataka msemaji kule Bungeni.

Mtu anaelewa anaefahamu changamoto zilizopo ndani ya jimbo hili, Hatuwezi kuchagua Mbunge ambae anakuja kutembea wakati wa kampeni, Hivyo mgombea atoke chama chochote, ila cha msingi na kilicho na mbolea awe msemaji wa changamoto za raia kule Bungeni.

FB_IMG_1594808936545.jpg
 
Kati ya watia nia ambao wamejitokeza Hadi sasa ni yupi uliyekwisha kumuona kuwa anafaa faa
Watia nia mpaka hivi sasa wamefika watatu
Hansi Mmass
Professor Ndakidemi na Victor Tesha hawa wametia nia kupitia chama cha mapinduzi
 
Kumbe Moshi Ni jimbo maskini kama majimbo mengine nchini. Lakini watani zangu wachaga huwa wanatutambia hapa kwamba Moshi vijijini ni kama New York.
 
Watia nia mpaka hivi sasa wamefika watatu
Hansi Mmass
Professor Ndakidemi na Victor Tesha hawa wametia nia kupitia chama cha mapinduzi


Aisee kama hujui kitu bora ukae kimya kabisa hao sio wa Vunjo kabisa na usije sema hujui vunjo ni kwa Mbatia mpk sasa kuna watia nia
1. Crispin Meela CCM
2. Kimei CCM
3 Mbatia NCCR
 
Vunjo ilitoholewa kutoka jimbo moja la Moshi Vijijini ndio ikatokea vunjo, kwa hiyo vunjo ilikua Sehemu ya Moshi Vijijini.
Aisee kama hujui kitu bora ukae kimya kabisa hao sio wa Vunjo kabisa na usije sema hujui vunjo ni kwa Mbatia mpk sasa kuna watia nia
1. Crispin Meela CCM
2. Kimei CCM
3 Mbatia NCCR
 
Watia nia mpaka hivi sasa wamefika watatu
Hansi Mmass
Professor Ndakidemi na Victor Tesha hawa wametia nia kupitia chama cha mapinduzi
Watu wa Moshi achaneni kabisa na CCM tafadhali mnataka kurudi nyuma?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom