Moshi imebadilika sana

Delegate

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2012
Posts
331
Reaction score
203
Nashukuru wote mlionipokea hapo Moshi December,kwa kweli nilijidai sana na wageni wangu walifurahi sana baada ya kula mtori na gali nyama choma vitu ambavyo havipo kabisa mitaa hii!!!

Kilichonishangaza ni jinsi mji wa Moshi ulivyobadilika sana sana,kwa kweli nilipoondoka niliacha maduka karibu yote makubwa yanaendeshwa na Wahindi,kusema kweli sikuona Mhindi hata mmoja,sijui wako wapi,,wamekimbia competition??]

Nimeshangaa kuona msururu wa magari na kuna traffic kubwa ya magari kitu ambacho hakikuwepo,pale soku kuu Moshi zamani tulikuwa tunapita na speed ya 120 lakini sasa hivi kutoka soko kuu kwenda stand ya mabasi utatumia dakika 20 na gari jambo la kushangaza sana

Vilevile tulishangaa kuona jinsi watu wa Moshi walivyobadilika na kutumia magari yao kwenda nyumbani,tulitoka moshi tarehe 23 kwenda dar,tulipishana na magari binafsi sio mabasi kuanzia Moshi mpaka Dar,magari mengi sana kitu ambacho hakikuwepo,
naona watanzania wameamka sana sasa hivi,hongereni sana wandugu.
 
Tulipisha barabarani lakini sikukutambua tena, kumbe muda mrefu uliondoka Moshi, karibu tena
 
Karibu tena pasaka.Maendeleo uliyoyaona ni juhudi binafsi za watu wa moshi pamoja na kodi kuwa kubwa hawajakata tamaa
 
Kwa ukabila uliojaa uchagani si muhindi tu hakuna mtu yeyote atakayeweza atakayeweza kushindana na akashinda

Aisee nenda kanunue zile mbao kwenye duka la shirima usinunue mahali pengine kabisaaa
 
Aisee nenda kanunue zile mbao kwenye duka la shirima usinunue mahali pengine kabisaaa

hahahahahah utahama mwenyewe miak ya 2001 -2003 maduka mengi ukipita hii njia ya kindoroko ni whindi tupu kumbe hawapo tena hahahahahahaah na hata arusha wamewakimbiza kiaina
 
Tulipisha barabarani lakini sikukutambua tena, kumbe muda mrefu uliondoka Moshi, karibu tena

kwa kweli tulipigwa na butaa kwa jinsi mambo yanavyobadilika haraka,sikutegemea ipo siku watu watasaifiria magari yao binafsi long distance
 
vipi hali ya usafi umeionaje???
 
Mnaenda kuuchumia huko kwenye maboxi na kulia huko huko, karibu tujenge taifa yapo mengi zaidi ya kula mtori na kula nyama choma na kuona msururu wa magari, home is the most beautiful place chini ya mbingu hii.
 
Wahindi hawana ubavu wa kushindana na mchaga hata kidogo ingawa wafanyabiashara wengi wa Moshi hawajasoma lia kwenye mambo ya pesa wana PHD.
Wahindi walikuwa wanalipa kodi 40000/= kwa mwezi chumba cha biashara ila mchaga anaenda shirika la nyumba anawaambia atalipa Laki 3 kwa mwezi wamtimue muhindi halafu achukue hicho chumba.
ndio maana wahindi wameisha double road Moshi, maduka yote ni wachaga tu.
 

Mimi ni msukuma lakini wachaga kwa kweli ninawazimia(siyo wale majambazi).
 

Wewe usiifananishe Moshi uliyoiona December na Moshi ya kawaida. Hizo trafic jam ulizoziona ni kwa sababu ya tabia ya Wachaga kukimbilia Moshi december. Ukitaka kuijua Moshi vizuri itembelee kuanzia February, baada ya Hijja ya Wachaga. Wahindi bado wapo ingawa wamepungua, pita double road kama unaenda soko la kati ndio utawaona vizuri, na barabara ya Hindu Mandal wamejazana mbaya.
Mji ushaanza kutulia sasa hivi hakuna cha jam na Wahindi wako bize na maduka yao.
Karibu tena Mo- Town!
 
Wewe unapaangalia moshi December njoo February uione ilivyopoa utaionea huruma.Na hiyo foleni ni kwa sababu ya jam ya raia kuelekea migombani
 
Ukiwa Moshi kwa WAZEE wa Bandari a.k.a Wazee wa Ku IMPORT hakuna shida
tena mizigo ya kumwaga... kweli Moshi imebadilika
 
sikuficha hali ya uchafu inarudi kwa kasi..............ama kweli UKIMSIFU MGEMA...............
 
Jamani muelewe kwamba msongamano wa magari barabarani ni ishara ya kulemewa kwa miundombinu na si kipimo bora cha maendeleo....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…