Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni

Confidencer

Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
29
Reaction score
9
Rais Kikwete ni mojawapo ya marais bora kutokea katika jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Nasema hivyo nikiwa na reflect hali ilivyokua kutoka kipindi cha Mwinyi, Mkapa na mpaka sasa anamalizia Kikwete.

Ni suala lililo wazi na linaloonekana kua katika kipindi hiki tumeshuhudia maendeleo makubwa tu ambayo yanamgusa mtanzania wa kawaida moja kwa moja. Miundombinu imeboreshwa kwa kiasi kikubwa hasa barabara, viwanja vya ndege na hata reli japo kwa kiasi kidogo. Tumeshuhudia barabara mbali mbali zikijengwa kwa ubora wa hali ya juu including ile ya Dodoma Arusha, Ruaha mbuyuni Iringa, Dar mwanza na nyingine nyingi tu ambazo wewe msomaji unazijua.

Kumekua na comparisons nyingi tu za watu Kumkejeli kwa kushindwa kuwashughulikia vigogo wala rushwa, na kasi ya ukuaji uchumi. Itakumbukwa kua katika kipindi cha Mkapa kulikua na kasi nzuri ya ukuaji wa uchumi lakini uchumi huo ukawa ni wa baadhi ya watu. Mwananchi wa kawaida wa kule mbinga vijijini na Lupa tinga tinga haukumsaidia kwa lolote.

Anayebeza haya abeze tu lakini kimoyomoyo anashuhudia kua

1. Wafanyakazi wa ndani wamekua adimu sana na mishahara yao imepanda kisa ni shule za kata(japo zilipondwa sana
mwanzoni)

2. Wachangiaji wengi na waropokaji humu wamesoma katika shule na vyuo ambavyo vimepatikana ndani ya uongozi wa Kikwete

3. Bodi ya mikopo kwa wanafunzi, sekretarieti ya ajira pamoja na ukuaji mkubwa wa viwanda hapa Dar ni chini ya uongozi wake..

Kuna mambo mengi sana ambayo kwa kweli jamaa amejitahidi ukizingatia kua amekua katika kipindi ambacho serikali inafuatiliwa kwa umakini na watu wake.

Kuna mapungufu ambayo rais kikwete anayo ambayo ni kushindwa kukemea baadhi ya matatizo kama ufisadi na rushwa. Haya ni mapungufu ambayo tunategemea raisi ajaye kwanza atutoe hapa tulipo lakini atufikishe juu zaidi ya hapa.

Mi najua kua kama binadamu wa kawaida anayo mapungufu yake na haya ndio mapungufu makubwa ya rais wetu huyu, simlaumu kwa sababu kila binadamu ana mapungufu na hata wewe msomaji unayo yako kwa mfano inawezekana kuna demu mmoja unamhonga sana na anakufanyia vitimbi lakini bado uko naye na kumuacha unashindwa japo hupendi vitendo vyake. Matatizo mengine ni ya kimfumo zaidi na nadhani katiba ndio ilibidi iwe suluhu japo uongozi wake imeichakachua.

Suala ni kuhakikisha kua raisi ajaye awe na positive side sifa zoote za rais kikwete na negative side sifa ziwe chache...!Any way mi naishia hapa ila Big up Kikwete you stood for what you do bilieve na umeachive so Hongera...

Waropokaji na wasiokupenda watabwabwaja tu ila hata wao wakikalia hiko kiti chako hapo cha kwanza watataka wajaze matumbo yao.Is human nature hakuna malaika humu.
:A S crown-1::A S crown-1::A S crown-1::A S crown-1:
 
Kwa vile kila mtu na mtizamo wake na wewe uko sawa.
Nionavyo mimi ni kweli kabisa kila binadamu ana mapungufu yani ukamilifu kwa binadamu haiwezekani kwa vile si malaika.
Mtu huagaliwa Stregth zake na pua weakness zake thn anafanyiwa comparison na kuangalia ni upande upi una athari. Mimi sikubariani na wewe tu kwa sababu nionavyo mimi Ben Mkapa alifanya kazi kubwa mno na ni ya ziada,alipewa nchi ikiwa mfilisi kabisa. Ni yeye alieinyanyua nchi hii kutoka kutokopesheka hadi kukopesheka. Ben ndo alikuta madeni hayalipiki toka utawala wa mzee Ali,alilipa madeni,akajenga barabara na kuacha pesa ya kutosha hazina!
Miradi ya barabara ilianzishwa na Ben na JK kaja kukamilisha tu hiyo miradi.
Labda unisaidie mradi mkubwa na wa maendeleo kwa watanzania umeanzishwa na serikali ya JK na sio ule tu wa kukamilisha.
Na nikuambie tu rais ajaye atakuwa na wakati mugumu sana sawa na mzee Ben. Hazina itaachwa shida!
Weakness kwa JK ni kubwa zaidi ya strength,hana msimamo hawezi kuwa na maamuzi yeye kwake yote sawa tu ilimradi asionekane kamkosea mtu! Characteristics hizi ni hatari kwa taasisi kubwa km RAIS!
Ni maoni yangu km ulivyotoa yako!
 
Hayo yote uliyoyasema hayakuwa katika mipango ya Kikwete.

Barabara

Mfumo mzima wa miundo mbinu ya barabara ilisukwa wakati wa Mkapa,ndio maana kikwete alivyojaribu kuweka waziri tofauti anayehusika kuitengeneza mikakati husika (Magufuri) utendaji ulikuwa ni wa kutia aibu.

Kikwete alifanya jitihada kubwa sana za kuupaka matope utawala wa Mkapa, akafikia hatua ya kumdharirisha magufuri kwa kumteua kwa shingo upande kuwa waziri wa mboga, lakini maji yalipozidi unga akalamba matapishi yake mwenyewe, akamteua tena magufuri bila kujali kwamba alihusika na ugawaji holela wa nyumba za serikali kitu ambacho Kikwete alisema atapigana nacho kwa uwezo wake wote ndani ya Bunge letu la Jamhuri ya Muungano, na mbele ya macho zaidi ya milioni sabini ya watanzania katika Television.

Hakuna Jipya alililolifanya Kikwete katika Barabara, Hizi barabara zote tunazoona zinajengwa zilikuwa kwenye mikakati ya 2020 ya bwana Mkapa, na zaidi hazijengwi kwa pesa zetu, pesa zetu kikwete anazitumia kwenye safari zisizo na msingi ni mambo mengine ya hovyo hovyo ambayo hayakuwa katika mipango ya serikali, kama huu upuuzi wa Katiba Mpya.

Shule za Kata
Wewe unaweza ukawa ni mmoja wa watanzania wajinga kuliko wote kwa kujitokeza mbele ya jukwaa hili na kupigia chapuo shule za kata, tena bila aibu na kudai zimeongeza soko la Mahouse Girl. Ni aibu kubwa kwa mpiga debe wa rais kuja kuzungumzia mambo ya ma HOUSE GIRLS katika dunia iliyojaa changamoto na fursa lukuki za kimaendeleo.

UFISADI

Yeye ndio kiongozi wao, kwa hiyo sio kwamba ameshindwa kuwashughurikia, hawezi kusaliti cult members wenzake.
 
Akina mama na vijana
Akina mama na vijana wamepewa nafasi katika nafasi za uteuzi kuliko kipindi kingine chochote mfano kuna wakuu wa Wilaya wapya zaidi ya 40 ni vijana kabisa.
 
Hadi mwishoni mwa mwezi Aprili, 2014 uwezo wa mitambo yote ya kufua umeme (total installed capacity) ulifikia MW 1,583 (maji - asilimia 35, gesi asilia - asilimia 34 na mafuta - asilimia 31). Uwezo huo wa mitambo yote ni sawa na ongezeko la asilimia 78 ikilinganishwa na MW 891 zilizokuwepo mwaka 2005 wakati Serikali ya Awamu ya Nne inaingia madarakani. Hili ni jambo la kujivunia kwa Serikali ya Chama cha Mapinduzi.
 
Hadi mwishoni mwa mwezi Aprili, 2014 uwezo wa mitambo yote ya kufua umeme (total installed capacity) ulifikia MW 1,583 (maji - asilimia 35, gesi asilia - asilimia 34 na mafuta - asilimia 31). Uwezo huo wa mitambo yote ni sawa na ongezeko la asilimia 78 ikilinganishwa na MW 891 zilizokuwepo mwaka 2005 wakati Serikali ya Awamu ya Nne inaingia madarakani. Hili ni jambo la kujivunia kwa Serikali ya Chama cha Mapinduzi.

Na zile bajaji 400 amezikamilisha..??
 
Anaanzisha mchakato wa katiba unaotumia mabilioni, halafu mwishoni unatokea wizi wa wazi mchana kweupe wa kuiba kura kupitisha katiba, yeye badala ya kukemea upuuzi huo, ndio yuko mstari wa mbele kuitetea hiyo katiba ya wizi ! Huku si kulitafutia taifa laana ?.

Siwezi kumsifia mtu mpuuzi kiasi hiki !. Nimemdharau sana !
 
Na zile bajaji 400 amezikamilisha..??


Kituo kikubwa na cha aina yake cha matibabu ya maradhi ya moyo hapa nchini. Huduma za kisasa za uchunguzi na matibabu ya maradhi ya moyo ambazo zamani zilikuwa zinapatikana nje ya nchi sasa zinaweza kupatikana hapa hapa nchini. Kwa kuwa na vitanda 100 vya kulaza wagonjwa, Watanzania wengi wataweza kuhudumiwa na maisha yao kuokolewa.



Katika kituo hiki watu wanaweza kufanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo (open heart surgery), uwekaji wa mashine ya kuongezea nguvu kwenye moyo (pacemaker), uwekaji wa vyuma vidogo katika mishipa ya damu ya moyo ambayo imebanana (stent). Tangu kituo kianze kazi rasmi tarehe 30 Aprili, 2013 mpaka sasa watu 347 wamefanyiwa upasuaji wa moyo na watu watatu wamewekewa pacemaker tangu huduma hiyo ianze Novemba, 2013. Mapema mwakani kituo kinatarajiwa kuanza huduma ya kuweka stent.


 
Rais Kikwete ni mojawapo ya marais bora kutokea katika jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Nasema hivyo nikiwa na reflect hali ilivyokua kutoka kipindi cha Mwinyi, Mkapa na mpaka sasa anamalizia Kikwete.

Ni suala lililo wazi na linaloonekana kua katika kipindi hiki tumeshuhudia maendeleo makubwa tu ambayo yanamgusa mtanzania wa kawaida moja kwa moja. Miundombinu imeboreshwa kwa kiasi kikubwa hasa barabara, viwanja vya ndege na hata reli japo kwa kiasi kidogo. Tumeshuhudia barabara mbali mbali zikijengwa kwa ubora wa hali ya juu including ile ya Dodoma Arusha, Ruaha mbuyuni Iringa, Dar mwanza na nyingine nyingi tu ambazo wewe msomaji unazijua.

Kumekua na comparisons nyingi tu za watu Kumkejeli kwa kushindwa kuwashughulikia vigogo wala rushwa, na kasi ya ukuaji uchumi. Itakumbukwa kua katika kipindi cha Mkapa kulikua na kasi nzuri ya ukuaji wa uchumi lakini uchumi huo ukawa ni wa baadhi ya watu. Mwananchi wa kawaida wa kule mbinga vijijini na Lupa tinga tinga haukumsaidia kwa lolote.

Anayebeza haya abeze tu lakini kimoyomoyo anashuhudia kua

1. Wafanyakazi wa ndani wamekua adimu sana na mishahara yao imepanda kisa ni shule za kata(japo zilipondwa sana
mwanzoni)

2. Wachangiaji wengi na waropokaji humu wamesoma katika shule na vyuo ambavyo vimepatikana ndani ya uongozi wa Kikwete

3. Bodi ya mikopo kwa wanafunzi, sekretarieti ya ajira pamoja na ukuaji mkubwa wa viwanda hapa Dar ni chini ya uongozi wake..

Kuna mambo mengi sana ambayo kwa kweli jamaa amejitahidi ukizingatia kua amekua katika kipindi ambacho serikali inafuatiliwa kwa umakini na watu wake.

Kuna mapungufu ambayo rais kikwete anayo ambayo ni kushindwa kukemea baadhi ya matatizo kama ufisadi na rushwa. Haya ni mapungufu ambayo tunategemea raisi ajaye kwanza atutoe hapa tulipo lakini atufikishe juu zaidi ya hapa.

Mi najua kua kama binadamu wa kawaida anayo mapungufu yake na haya ndio mapungufu makubwa ya rais wetu huyu, simlaumu kwa sababu kila binadamu ana mapungufu na hata wewe msomaji unayo yako kwa mfano inawezekana kuna demu mmoja unamhonga sana na anakufanyia vitimbi lakini bado uko naye na kumuacha unashindwa japo hupendi vitendo vyake. Matatizo mengine ni ya kimfumo zaidi na nadhani katiba ndio ilibidi iwe suluhu japo uongozi wake imeichakachua.

Suala ni kuhakikisha kua raisi ajaye awe na positive side sifa zoote za rais kikwete na negative side sifa ziwe chache...!Any way mi naishia hapa ila Big up Kikwete you stood for what you do bilieve na umeachive so Hongera...

Waropokaji na wasiokupenda watabwabwaja tu ila hata wao wakikalia hiko kiti chako hapo cha kwanza watataka wajaze matumbo yao.Is human nature hakuna malaika humu.
:A S crown-1::A S crown-1::A S crown-1::A S crown-1:

View attachment 193525 View attachment 193526
Ni kweli amewazidi Nyerere, Mwinyi na Mkapa kwani katika utawala wao hawakuwa na Muda wa kuyafanya haya.
 
Credits zangu kwa JK ni:

1. Ujenzi wa UDom, ingawa ujenzi wake unafilisi mifuko ya Hifadhi za Jamii kwa gharama ya Wafanyakazi

2. Ujenzi wa daraja la Kurasini-Kigamboni, ingawa ni ufujaji mwingine wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii NSSF ambao tayari umedhoofishwa na Ujenzi wa Jengo la Bunge na UDom

3. Ujenzi wa Daraja la Mto Malagarasi ( hii ni credit kubwa sana maana ni pesa za Serikali na Wafadhili)

3. Ujenzi wa barabara ingawa ni kwa gharama ya reli, hasa ya Kati. Angeweka nguvu nyingi kuimarisha reli ya Kati ambayo Mkapa aliipuuza, angepata sifa nyingi na kitu cha kukumbukwa kwacho maana barabara sifa anagawana na Mkapa aliyeanzisha miradi ya barabara na kutelekeza Reli.

4. Kuanzisha mchakato wa Katiba mpya ingawa yeye binafsi ndiye ameuvuruga na kutupotezea muda na mapesa mengu sana.

Mabaya ya Kikwete ni:-
1. Kufumbia macho wizi wa malu za umma na ufisadi- EPA, Meremeta, IPTL nk

2. Deni la Taifa kupaa badala ya kupungua au ku maintain.

Vv
 
Rais Kikwete ni mojawapo ya marais bora kutokea katika jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Nasema hivyo nikiwa na reflect hali ilivyokua kutoka kipindi cha Mwinyi, Mkapa na mpaka sasa anamalizia Kikwete.

Ni suala lililo wazi na linaloonekana kua katika kipindi hiki tumeshuhudia maendeleo makubwa tu ambayo yanamgusa mtanzania wa kawaida moja kwa moja. Miundombinu imeboreshwa kwa kiasi kikubwa hasa barabara, viwanja vya ndege na hata reli japo kwa kiasi kidogo. Tumeshuhudia barabara mbali mbali zikijengwa kwa ubora wa hali ya juu including ile ya Dodoma Arusha, Ruaha mbuyuni Iringa, Dar mwanza na nyingine nyingi tu ambazo wewe msomaji unazijua.

Kumekua na comparisons nyingi tu za watu Kumkejeli kwa kushindwa kuwashughulikia vigogo wala rushwa, na kasi ya ukuaji uchumi. Itakumbukwa kua katika kipindi cha Mkapa kulikua na kasi nzuri ya ukuaji wa uchumi lakini uchumi huo ukawa ni wa baadhi ya watu. Mwananchi wa kawaida wa kule mbinga vijijini na Lupa tinga tinga haukumsaidia kwa lolote.

Anayebeza haya abeze tu lakini kimoyomoyo anashuhudia kua

1. Wafanyakazi wa ndani wamekua adimu sana na mishahara yao imepanda kisa ni shule za kata(japo zilipondwa sana
mwanzoni)

2. Wachangiaji wengi na waropokaji humu wamesoma katika shule na vyuo ambavyo vimepatikana ndani ya uongozi wa Kikwete

3. Bodi ya mikopo kwa wanafunzi, sekretarieti ya ajira pamoja na ukuaji mkubwa wa viwanda hapa Dar ni chini ya uongozi wake..

Kuna mambo mengi sana ambayo kwa kweli jamaa amejitahidi ukizingatia kua amekua katika kipindi ambacho serikali inafuatiliwa kwa umakini na watu wake.

Kuna mapungufu ambayo rais kikwete anayo ambayo ni kushindwa kukemea baadhi ya matatizo kama ufisadi na rushwa. Haya ni mapungufu ambayo tunategemea raisi ajaye kwanza atutoe hapa tulipo lakini atufikishe juu zaidi ya hapa.

Mi najua kua kama binadamu wa kawaida anayo mapungufu yake na haya ndio mapungufu makubwa ya rais wetu huyu, simlaumu kwa sababu kila binadamu ana mapungufu na hata wewe msomaji unayo yako kwa mfano inawezekana kuna demu mmoja unamhonga sana na anakufanyia vitimbi lakini bado uko naye na kumuacha unashindwa japo hupendi vitendo vyake. Matatizo mengine ni ya kimfumo zaidi na nadhani katiba ndio ilibidi iwe suluhu japo uongozi wake imeichakachua.

Suala ni kuhakikisha kua raisi ajaye awe na positive side sifa zoote za rais kikwete na negative side sifa ziwe chache...!Any way mi naishia hapa ila Big up Kikwete you stood for what you do bilieve na umeachive so Hongera...

Waropokaji na wasiokupenda watabwabwaja tu ila hata wao wakikalia hiko kiti chako hapo cha kwanza watataka wajaze matumbo yao.Is human nature hakuna malaika humu.
:A S crown-1::A S crown-1::A S crown-1::A S crown-1:

Tatizo lake yeye JK ni kwamba huwa haongei sana au hajui kutetea jitihada zake kwa sababu anajua kuwa kila mtu anaona jitihada zake, kumbe baadhi yetu tunawza tukawa hatuoni Universities pia zimefurika, no one qualified missses a placement in one o the universities we have today. Usikute kuna baadhi yake hadi zinaweza kuwa zinakosa wanafunzi wa kudahili!
 
Kiukweli kupata wafanyakazi wa ndani siku hizi ni shida.
 
Rais Kikwete ni mojawapo ya marais bora kutokea katika jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Nasema hivyo nikiwa na reflect hali ilivyokua kutoka kipindi cha Mwinyi, Mkapa na mpaka sasa anamalizia Kikwete.

Ni suala lililo wazi na linaloonekana kua katika kipindi hiki tumeshuhudia maendeleo makubwa tu ambayo yanamgusa mtanzania wa kawaida moja kwa moja. Miundombinu imeboreshwa kwa kiasi kikubwa hasa barabara, viwanja vya ndege na hata reli japo kwa kiasi kidogo. Tumeshuhudia barabara mbali mbali zikijengwa kwa ubora wa hali ya juu including ile ya Dodoma Arusha, Ruaha mbuyuni Iringa, Dar mwanza na nyingine nyingi tu ambazo wewe msomaji unazijua.

Kumekua na comparisons nyingi tu za watu Kumkejeli kwa kushindwa kuwashughulikia vigogo wala rushwa, na kasi ya ukuaji uchumi. Itakumbukwa kua katika kipindi cha Mkapa kulikua na kasi nzuri ya ukuaji wa uchumi lakini uchumi huo ukawa ni wa baadhi ya watu. Mwananchi wa kawaida wa kule mbinga vijijini na Lupa tinga tinga haukumsaidia kwa lolote.

Anayebeza haya abeze tu lakini kimoyomoyo anashuhudia kua

1. Wafanyakazi wa ndani wamekua adimu sana na mishahara yao imepanda kisa ni shule za kata(japo zilipondwa sana
mwanzoni)

2. Wachangiaji wengi na waropokaji humu wamesoma katika shule na vyuo ambavyo vimepatikana ndani ya uongozi wa Kikwete

3. Bodi ya mikopo kwa wanafunzi, sekretarieti ya ajira pamoja na ukuaji mkubwa wa viwanda hapa Dar ni chini ya uongozi wake..

Kuna mambo mengi sana ambayo kwa kweli jamaa amejitahidi ukizingatia kua amekua katika kipindi ambacho serikali inafuatiliwa kwa umakini na watu wake.

Kuna mapungufu ambayo rais kikwete anayo ambayo ni kushindwa kukemea baadhi ya matatizo kama ufisadi na rushwa. Haya ni mapungufu ambayo tunategemea raisi ajaye kwanza atutoe hapa tulipo lakini atufikishe juu zaidi ya hapa.

Mi najua kua kama binadamu wa kawaida anayo mapungufu yake na haya ndio mapungufu makubwa ya rais wetu huyu, simlaumu kwa sababu kila binadamu ana mapungufu na hata wewe msomaji unayo yako kwa mfano inawezekana kuna demu mmoja unamhonga sana na anakufanyia vitimbi lakini bado uko naye na kumuacha unashindwa japo hupendi vitendo vyake. Matatizo mengine ni ya kimfumo zaidi na nadhani katiba ndio ilibidi iwe suluhu japo uongozi wake imeichakachua.

Suala ni kuhakikisha kua raisi ajaye awe na positive side sifa zoote za rais kikwete na negative side sifa ziwe chache...!Any way mi naishia hapa ila Big up Kikwete you stood for what you do bilieve na umeachive so Hongera...

Waropokaji na wasiokupenda watabwabwaja tu ila hata wao wakikalia hiko kiti chako hapo cha kwanza watataka wajaze matumbo yao.Is human nature hakuna malaika humu.
:A S crown-1::A S crown-1::A S crown-1::A S crown-1:

unajua source ya mapato ya kufanya hayo ni kutoka kwa wadhamini na mikopo....unajua kikwete kaiingiza nchi kwenye utumwa wa madeni miaka 200 ijayo.
 
View attachment 193525 View attachment 193526
Ni kweli amewazidi Nyerere, Mwinyi na Mkapa kwani katika utawala wao hawakuwa na Muda wa kuyafanya haya.
images
 
Back
Top Bottom