Mnyika kinara bungeni

Mnyika kinara bungeni

huyu kilaza labda asubiri mashindano ya kuiba wake za watu,kuvalisha mbwa bendera za vyama pinzani na kuundia watu kesi za uongo

hana tofaut na wale wa toto walio malza darasa la 7 af awajui kusoma na kuandka..pale mjengon
 
sasa kumbe watu mnapenda kuongopewa eeh! manake mimi ni miongoni mwa watu ambao niliwah kusema mnyika anataka kudumaa kisaisa kwa hli jimbo. na wakati nasema nilionekana niviroba lkn wachambuzi wa siasa walisema ni kweli.hatuwez kumtegemea amalize haya yote kwa mara mja ila kule alikofanya apewe hongera zake na siyo kuonekana kana kwamba hajatend kabisa.

Watu wakiacha ushabiki na kumueleza ukweli ataweza, manispaa ya Kinondoni ikisimamiwi vizuri na uwezo wa mbunge kuelekeza mapato kwenye kuwaletea maendeleo wananchi inawezekana. Nimeona Kigoma kaskazini ilivyowezekana.
 
Watu wakiacha ushabiki na kumueleza ukweli ataweza, manispaa ya Kinondoni ikisimamiwi vizuri na uwezo wa mbunge kuelekeza mapato kwenye kuwaletea maendeleo wananchi inawezekana. Nimeona Kigoma kaskazini ilivyowezekana.

hilo nalijua kabisa tatzo ni kwamba yeye ni mbunge na watendaji kama wakurugenzi ni chama oriented unaategemea wamsaidie katika haya ili mwishoni chama kishindwe? ngoja nikupe mfano i nimetokea kijiji ambacho upinzani ulianza zamani za vyama vingi yaani 1995. sasa jimbo letu lilibaki nyuma ukilinganisha na jaiaambo la jiran ambalo chama ndo kilitawala na apo ili kutufanya tuone upinzani si kitu wenzetu walijengewa bara bara ya lami ssi hata kituo cha afya hatukuboreshewa libidi mbunge wetu kutoa fedha mfukoni kutusaidia kuboresha kaituo cha afya na kununua gari la wagonjwa.

kwa maendelwo yaliyopatikana kwa jirani zetu uchaguzi wa 2000 tukarudisha chama madarakani mbunge wetuakaja kulala bungeni hana moja wa mbili tukachoka 2005 tukajilipua tukasema liwalo na liwe tuendeleze mapambano lol! this time madiwani wakaja juu manake wengi ni upinzani acha kabisa jimbo ni tamu ile mbaya maji hadi kwenye kila nyumba na huwez kuamini kila mwananchi ameelimishwa watuwanalipia bili zao wanafadi maji kiangazi na masika. shule zipo waalim wapo tena wengine jimbo linajitolea kuwapa motisha ukifika kijijini hadi raha kuko ama town ila ni pale ambapo wananchi alisema tunataka maendeleo wala si siasa.
 
hilo nalijua kabisa tatzo ni kwamba yeye ni mbunge na watendaji kama wakurugenzi ni chama oriented unaategemea wamsaidie katika haya ili mwishoni chama kishindwe?.

Bado unaendelea kufanya tatizo ni external. Mbona Karatu wakati Slaa ni Mbunge alikuwa amezungukwa na CCM kila kona lakini aliweza? Pamoja na hizo changamoto uwezo binafsi wa mgombea unaleta tofauti KUBWA.
 
Barabara za Kilungule ni dhoflihali! Bonyokwa hakuendeki, King'ong'o hakuna njia, Ubungo Kibangu shida!

Acha uvivu wa kusoma na kutafiti. Hiyo michango na maswali anayouliza Mnyika humo Bungeni huelekezwa kwa serikali. Sasa, usingekuwa mvivu ungegundua serikali imeambiwa mangapi ya Ubungo na huyu Mnyika kuliko wale wanaoenda kusinzia bungeni hadi wanataka TV zipigwe marufuku bungeni.
 
Tuwekewe na takwimu za wanaoongoza kwa kuomba miongozo
 
sasa kumbe watu mnapenda kuongopewa eeh! manake mimi ni miongoni mwa watu ambao niliwah kusema mnyika anataka kudumaa kisaisa kwa hli jimbo. na wakati nasema nilionekana niviroba lkn wachambuzi wa siasa walisema ni kweli.hatuwez kumtegemea amalize haya yote kwa mara mja ila kule alikofanya apewe hongera zake na siyo kuonekana kana kwamba hajatend kabisa.

Mimi namuamini Mnyika kwa hoja zake lakini angekuwa mbunge wa Taifa (Zamani walikuwepo hawa/Viti maalum) na si mbunge wa jimbo hasa jimbo lenyewe Ubungo! Mnyika anafanya vyema sana Bungeni kwa hoja zake (kasoro alipojichanganya na kumudhihaki Rais) zenye masilahi kwa nchi lakini ukirudi kwa waliompeleka huko Bungeni hali ni tete! Ana Madiwani wengi Jimboni lakini naona madiwani nao wameanza kuchoka; siku hizi simuoni Diwani Manota. Nilidhani alipopata gari angekuwa anawatembelea wapiga kura wake kumbe afadhali wakati ule ana pikipiki!
 
Mimi namuamini Mnyika kwa hoja zake lakini angekuwa mbunge wa Taifa (Zamani walikuwepo hawa/Viti maalum) na si mbunge wa jimbo hasa jimbo lenyewe Ubungo! Mnyika anafanya vyema sana Bungeni kwa hoja zake (kasoro alipojichanganya na kumudhihaki Rais) zenye masilahi kwa nchi lakini ukirudi kwa waliompeleka huko Bungeni hali ni tete! Ana Madiwani wengi Jimboni lakini naona madiwani nao wameanza kuchoka; siku hizi simuoni Diwani Manota. Nilidhani alipopata gari angekuwa anawatembelea wapiga kura wake kumbe afadhali wakati ule ana pikipiki!

Mnyika anahitaji marafiki kama wewe Kimbunga, wengi wa wanaomzunguka ni washabiki na si marafiki.
 
Acha uvivu wa kusoma na kutafiti. Hiyo michango na maswali anayouliza Mnyika humo Bungeni huelekezwa kwa serikali. Sasa, usingekuwa mvivu ungegundua serikali imeambiwa mangapi ya Ubungo na huyu Mnyika kuliko wale wanaoenda kusinzia bungeni hadi wanataka TV zipigwe marufuku bungeni.

Acha wewe. wewe umetafiti nini? Amesema nini kuhusu Ubungo? Jimboni Mnyika ni mtupu mimi nalijua hilo kwa kuwa Mnyika ni Mbunge wangu. Mimi nimewahi kusema hapa Mnyika aitumie Ilani ya CCM kuwakandamiza sijui hataki kuisoma? Sijasikia akiwakumbusha watekeleze ahadi lukuki za barabara za jimboni Ubungo. Akisimamia hilo na barabara zile zikatengenezwa mbona atapeta tu mwaka 2015 lakini kinyume na hapo huenda akausikia Ubunge kwenye Bomba. Nyie mdanganyeni mkidhani mnamsaidia kumbe mnampoteza ati kinara; kinara wakati jimbo lake hali inatisha? wewe umewahi kupita barabara ya Kimara Mwisho kuelekea Kisukuru/segerea? Hali inatisha. Unaijua Bonyokwa wewe, Golani je, unaifahamu Kibangu ama King'ong'o au Kilungule. Utadhani hawakupiga kura hawa.

Najua hana pesa za kuleta maji wala barabara lakini hata kelele na kuwahamasisha watu wake. Mnyika ahamasishe tu barabara zile hazihitaji pesa nyingi na watu wa kule hawana makuu wewe pata grader la manispaa watajaza mafuta lichonge barabara. Awahakikishie watu kwamba atawaletea grader la manispaa waao wajitolee mafuta watu watatoa hela za mafuta na barabara zitachongwa; watu wa huko hawalalilii lami wao wanataka passability tu.
 
Nguvu ya hoja za Mnyika na Tundu Lissu bungeni ni zaidi ya wabunge wote kutoka magamba + Nape +Kinana + Dhaifu
 
Acha wewe. wewe umetafiti nini? Amesema nini kuhusu Ubungo? Jimboni Mnyika ni mtupu mimi nalijua hilo kwa kuwa Mnyika ni Mbunge wangu. Mimi nimewahi kusema hapa Mnyika aitumie Ilani ya CCM kuwakandamiza sijui hataki kuisoma? Sijasikia akiwakumbusha watekeleze ahadi lukuki za barabara za jimboni Ubungo. Akisimamia hilo na barabara zile zikatengenezwa mbona atapeta tu mwaka 2015 lakini kinyume na hapo huenda akausikia Ubunge kwenye Bomba. Nyie mdanganyeni mkidhani mnamsaidia kumbe mnampoteza ati kinara; kinara wakati jimbo lake hali inatisha? wewe umewahi kupita barabara ya Kimara Mwisho kuelekea Kisukuru/segerea? Hali inatisha. Unaijua Bonyokwa wewe, Golani je, unaifahamu Kibangu ama King'ong'o au Kilungule. Utadhani hawakupiga kura hawa.

Najua hana pesa za kuleta maji wala barabara lakini hata kelele na kuwahamasisha watu wake. Mnyika ahamasishe tu barabara zile hazihitaji pesa nyingi na watu wa kule hawana makuu wewe pata grader la manispaa watajaza mafuta lichonge barabara. Awahakikishie watu kwamba atawaletea grader la manispaa waao wajitolee mafuta watu watatoa hela za mafuta na barabara zitachongwa; watu wa huko hawalalilii lami wao wanataka passability tu.

Mkuu wewe siku zote hakuna jema analofanya Mnyika...Mimi ni mkazi wa Ubungo na huyu ndiye mbunge bora ukilinganisha na wabunge wengine kwa kipindi cha miaka 20
 
Mnyika anahitaji marafiki kama wewe Kimbunga, wengi wa wanaomzunguka ni washabiki na si marafiki.

Mkuu watu wana ushabiki kama watoto vile bila kupambanua. Mimi nazijua siasa za Ubungo. Tunajua Mnyika alishinda kivipi na sababu za ushindi wake. Wacha tu wamdanganye kwamba mambo huko ni shwari, hatutakuwa na hata sababu ya kwenda kukesha Loyola kwa kuwa tutakuwa tayari tunajua matokeo.
 
Mimi namuamini Mnyika kwa hoja zake lakini angekuwa mbunge wa Taifa (Zamani walikuwepo hawa/Viti maalum) na si mbunge wa jimbo hasa jimbo lenyewe Ubungo! Mnyika anafanya vyema sana Bungeni kwa hoja zake (kasoro alipojichanganya na kumudhihaki Rais) zenye masilahi kwa nchi lakini ukirudi kwa waliompeleka huko Bungeni hali ni tete! Ana Madiwani wengi Jimboni lakini naona madiwani nao wameanza kuchoka; siku hizi simuoni Diwani Manota. Nilidhani alipopata gari angekuwa anawatembelea wapiga kura wake kumbe afadhali wakati ule ana pikipiki!

Mkuu laiti Mnyika angekuwa CCM ungemsifia vibaya sana....
 
Kamanda mnyika chapa kz kwa faida ya taifa,kitu ambacho nadra sana kwa wabunge vilaza wa ccm.
 
Back
Top Bottom