Mnyaa: Ipo Kazi Kuing’oa CCM

Mnyaa: Ipo Kazi Kuing’oa CCM

Kakke

JF-Expert Member
Joined
Dec 4, 2010
Posts
1,883
Reaction score
1,482
1381.jpg



MBUNGE WA Mkanyageni, Mohamed Habib Mnyaa (CUF)
Tuesday, Desemba 16, 2014

MBUNGE WA Mkanyageni, Mohamed Habib Mnyaa (CUF), amesema ni vigumu vyama vya siasa vilivyopigania Uhuru kuondolewa madarakani kirahisi kwani vyama hivyo vina nyenzo za kushinda uchaguzi kwa gharama yoyote.

Mnyaa aliyasema hayo katika mahojiano Maalumu na Majira mwishoni mwa wiki akiwa mjini Mbeya. Alifafanua: "Ujio wa vyama vingi vya siasa katika nchi nyingi za Afrika, umegubikwa na ukiritimba wa vyama tawala kuhodhi vyombo vya dola ili viwasaidie kwenye chaguzi zinazoendelea katika nchi hizo."

Alisema fursa pekee ya ushindi kwa vyama vya upinzani ni kuondokana na ubinafsi, tamaa ya madaraka, na badala yake ni kujenga umoja utakaoweza kukiondoa chama tawala madarakani.

Alitoa mfano kuwa, nchi za Afrika zilizofanikiwa kuviondoa vyama vinavyoshika dola madarakani kama Kenya, Zambia na Malawi, vyama vya upinzani vilifanikiwa baada ya kuunda umoja wao na kuviondoa vyama vilivyopigania uhuru.

"Tumeshuhudia Kenya KANU ikianguka, Zambia UNIP kikiondolewa madarakani…hapa kwetu UKAWA ukiimarishwa CCM itaong'oka," alisema Mnyaa ambaye pia ni Mjumbe anayewakilisha Bunge kwenye Bodi ya Wakurugenzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe.

Aliongeza kuwa, tatizo la ubinafsi katika vyama vya upinzani ndilo linalosababisha vyama hivyo kuendelea kushindwa kwenye chaguzi mbalimbali zinazoendelea, hivyo upo uwezekano wa CCM kuendelea kuwepo madarakani kwa miaka mingi ijayo kama wapinzani hawatabadili mtazamo wao kwenye jamii.

"Yapo matumaini makubwa ya UKAWA kufanya vizuri, tumejipanga vyema kwa mikakati na tutasimamisha mgombea mmoja wa Urais ambaye hatutamweka hadharani kwa sasa."
"UKAWA imeweka mipango mizuri ya mgombea wa Urais ambaye hawezi kuwekwa bayana mapema ili kuepuka hujuma za chama tawala," alisema Mnyaa.

Chanzo: Majira
 
Swala sio chama tawala, tatizo in uelewa mdogo wa walio wengi. Nchi ambazo wananchi wake niwepesi kuelewa wamesha ng'oa zamani vyama tawala. Kwanzia sasa, vyama vikazane Kuelimisha watu vijijini kila kona ya nchi. Mbona watu wameanza kuelewa. Nchi lukuki zime toa madarakani vyama tawala. Mbona juzi hapa Joyce Banda katolewa madarakani? Kwaufupi elimu kwa wingi vijijini sababu ndo wengi wanaopiga kura. Na mjini kua hamasisha kujiandikisha na kupiga kura. Kwasababu wengi wao ni waelewa, ila wavivu kupiga kura kwasababu ya mishemishe nyingi. Hii ndo dawa ya chama tawala basi.
 
Swala sio chama tawala, tatizo in uelewa mdogo was walio wengi. Nchi ambazo wananchi wake niwepesi kuelewa wamesha ng'owa zamani vyama tawala. Kwanzia sasa, vyama vikazane Kuelimisha with vijijini kila kona ya nchi. Mbona with wameanza kuelewa. Nchi rukuki zime to a madarakani tayari vyama tawala. Mbona juzi hapa Joyce Banda katolewa madarakani? Kwaufupi elimi kwa wingi vijijini sababu ndo wengi wanaopiga kura. Name mjini Kuwait hamasisha kujiandikisha name kupiga kura. Kwasababu wengi mini in waelewa, ila wavivu kupiga kura kwasababu ya mishemishe nyingi. Hui ndo dawa ya chama tawala basi.

= lukuki.

Dah, hayo mengine badilisha mwenyewe. Mpaka Kuwait walipiga kura za Tanzania, maajabu haya. Au jamani tuna Kuwait ya Tanzania ambayo siijuwi?
 
Ahsante kwa marekebisho, a cha nifanye edit. Wajua hii simu inaleta spelling zake nimegundua muda huu. Kwa mfano ukiandika neno" zake" linabadilika ina andika"sake"
 
= lukuki.

Dah, hayo mengine badilisha mwenyewe. Mpaka Kuwait walipiga kura za Tanzania, maajabu haya. Au jamani tuna Kuwait ya Tanzania ambayo siijuwi?

We mwenyewe mbona michapio kibao tu, hebu rudi usome ulichoandika.
 
Mpango mzima nikuikataa rasimu ya katiba, bila hivyo watanzania tutazidi kuchezewa kama mazuzu na familia za watawala..1. Unafiki kuhusu aina gani ipi ya muungano tuufuate, nimewasikia watu wenye busara zao, wakishindana kwa jazba mate yakiwatoka, ni aina ipi ya serikali tuufuate? Jibu la watu walio na kweli ndani yao, jibu ni rahisi. Tuwe na serikali moja, ya watu wamoja, wanaopendana, tuwe na taifa lisilo na mipaka, raisi mmoja, zanzibar uwe ni mkoa ktk Taifa la jamuhuri ya Tanzania.Kwa kuli zenu za serikali mbili, tatu au nne. Hakuna muungano, kuna siku mtatengana tu, maana hakuna ukweli ndani yenu. Kuna siku kila mmoja wenu ataamua kwenda njia yake. Kwa maana ukichunguza sana utaona kila nchi inahitaji uhuru wake. Wanashindwa kusema ukweli kwa ajili yakutokuwa wawazi. Jibu sahihi kama kweli tunataka muungano tuwe na serikali moja, tuache unafiki.2. Kuhusu maadili ya uongozi, katiba ni kwa manufaa ya Watanzania. Tuunde katiba itakayowafanya watawala wawe makini na waadilifu katika uongozi wao kwa miongo yote ya utawala Tanzania.Katiba itamke wazi kuwa. Serikali yoyote itakayokuwa madarakani kwa kipindi chochote kile. Ikionyesha madhaifu yoyote yakukiuka katiba ya nchi, ubadhilifu, rushwa au serikali ikionyesha hali inayoleta mashaka kwa kutumia madaraka vibaya ya kukandamiza uhuru wa raia wake. Basi katiba itamke wazi kwamba Watanzania wote wenye umri wa miaka 18 nakuendelea, wafanye maandamano ya Amani kwa idadi ya watu isiyo na kikomo, hadi makao makuu ya nchi kushinikiza serikali kujiuzulu. Hii itasaidia kuzuia viongozi kufanya wanavyotaka, kujinufaisha binafsi na kuisababishia taifa hasara. Kung'ang'ania madarakani na kujifanya miungu watu. Bila mambo haya kukubaliwa watanzania tuikatae katiba hii maana katiba pendekezwa ni kwa ajili yakunufaisha familia za viongozi walioko madarakani pekee.
 
= lukuki.

Dah, hayo mengine badilisha mwenyewe. Mpaka Kuwait walipiga kura za Tanzania, maajabu haya. Au jamani tuna Kuwait ya Tanzania ambayo siijuwi?

Da unapitia comment ya mtu nukta kwa nukta wemwalim et? nakupongeza kuendelea na msimamo wa taaluma yako maana wengine hawapendi kujionyesha kua wao ni waalim
 
Back
Top Bottom