Mnavundika! Kwani hilo embe?

Lonestriker

JF-Expert Member
Oct 8, 2010
640
241
Mnavundika.jpg Mnavundika.jpg

Wakati fulani nikiwa mdogo baba yangu alirudi nyumbani na suruali nzuri sana ya dangrizi kama zawadi yangu katika sherehe yangu ya kuzaliwa zaidi ya miezi miwili mbele.

Marufuku ilitoka nisijaribu kuivaa kwa namna yoyote ile kabla ya siku lengwa kuwadia. Yalikuwa mateso makubwa ya Kisaikolojia , nilibaki kuikodolea macho kila uchao .

Nilikuwa nikiwaza muonekano wangu na mikogo mbalimbali kwa ndugu na rafiki zangu. Mashabiki, wanachama na wadau wa Yanga SC wameingia katika umbwe hili juu ya usajili iliofanywa na klabu yao juu ya mlinzi wa kati toka nchini Togo, Vicente Bossou.
Si lazima kila anayesajiliwa aingie kikosi cha kwanza nakuanza kuvuma lakini vilevile shaka huja pale unapomsajili mchezaji na kumweka kando kwa takribani mechi tano mfululizo katika ligi ukizingatia thamani ya mchezaji .


Usajili kiufundi, mbinu na kimfumo hufanyika kukidhi hitaji fulani la timu kwa mashindano yaliyopo ili kutengeneza maelewano mazuri ya timu kiushindani.

Ina maana mtogo huyo hakuwa chaguo la kocha? Au ni usajili kwa mahitaji ya baadae? Au bado embe hilo halijakomaa vyema basi linaendelea kuvundikwa?

Mwisho wa siku mwalimu ndio atakuwa na majibu sahihi lakini tujiulize, Nadir , Yondani, Twite na Pato Ngonjani hawa wote ni walinzi wazuri wa kati.
Kuna nafasi ya mtogo huyo kucheza na ilihali tuliona uzito wake katika mechi za kirafiki? Hata hivyo, jibu linalotoka vinywani mwa viongozi mwa Yanga ni kuwa bado utimamu wake wa mwili hauko sawa.

Lakini hapo nawaza miili ya Ngoma na Kamusoko ilikuja na viongeza-nguvu gani kiasi cha kufunguka moja kwa moja? Tuendelee kuisubiri suruali yetu , siku ya sherehe ikifika tutaivaa .

Ikitupwaya tukae kimya, ikitubana tunyamaze kabisa lakini ikitutosha vyema tuinue bega moja kwa mikogo.

Chanzo soka360
 
1.Tunachotaka ni ushindi ambao hadi sasa tumefanikiwa kwa hilo katika mechi tulizocheza.

2.safu yetu ya ulnzi imeruhusu bao moja tu tangu kuanza kwa ligi jambo ambalo hatuoni sababu ya kutafuta ulinzi mbadala .(ili kupunguza makosa gani?)

3.Yanga ina wachezaji 24 ambao wote wanaweza kucheza kikosi cha kwanza.na wanaotakiwa uwanjani ni 11 tu, hivyo hatuoni sababu ya kupangua kikosi wakati hicho kinachoanza kinatupa matokeo tunayoyahitaji.

4.siku nyingine ulizia pia na CHIDEBELE, KAVUMBAGU, AGBAN..au hawa hawalipwi mshahara?
 
Bado ligi ni mbichi kabisa. Safu iliyopo inafanya vizuri. Tatizo liko wapi?

Ubora wa timu nin pamoja na kuwa na benchi la uhakika. Akiumia mchezaji mmoja, anayechukua nafasi awe na kiwango pia. Unatoa kitu, unaweka kitu.

Maoni mengine yangefaa mwisho wa msimu wa ligi.
 
Back
Top Bottom