chizcom
JF-Expert Member
- Jul 31, 2016
- 7,581
- 15,722
Bahati nzuri kuishi kwenye uhuni ndio nimekulia na kila siku nawapa code ngumu kumeza. Wafanya biashara wa kuku wa kienyeji waliopo sokoni asilimia kubwa ni wajanja sana.
Embu fikiria kuku wametoka vijijini mpaka kufika sehemu ya soko mfano mijini lazima kuna kuku watakufa, wamechoka na wangine hawajanona kama mnavo waona bandani.
Hii tabia ipo sana, yaani mtu anabanda pale sokoni wewe unachagua kuku mnapatana bei na utataka uchinjiwe. Usipokuwa makini akienda huko kuchinjwa bora aje na manyoa utaweza kujua kuliko kuja kanyonyolewa na tayari kashakatwa. Hapa utakuwa umepewa kibudu au tofauti na yule uliyemuona bandani.
Ukitoka anarudishwa tena ili wateja wafike bei. Hii ni sample ya kuku tu, kwenye machinjio huko acha ni nyamaze tuendelee kula nyama.
Embu fikiria kuku wametoka vijijini mpaka kufika sehemu ya soko mfano mijini lazima kuna kuku watakufa, wamechoka na wangine hawajanona kama mnavo waona bandani.
Hii tabia ipo sana, yaani mtu anabanda pale sokoni wewe unachagua kuku mnapatana bei na utataka uchinjiwe. Usipokuwa makini akienda huko kuchinjwa bora aje na manyoa utaweza kujua kuliko kuja kanyonyolewa na tayari kashakatwa. Hapa utakuwa umepewa kibudu au tofauti na yule uliyemuona bandani.
Ukitoka anarudishwa tena ili wateja wafike bei. Hii ni sample ya kuku tu, kwenye machinjio huko acha ni nyamaze tuendelee kula nyama.