Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,175
- 48,459
Jee Polepole mambo anayoyasema ni ya kweli au ni uongo? Kama ni uongo ukweli ni upi na una ushahidi upi?
Wakati Polepole alipokuwa kiongozi wa CCM, aliyokuwa anayafanya yalikuwa na baraka za CCM au la. Kama yalikuwa ni mambo yake binafsi CCM waliwahi kumuonya?
Zama za Magufuli mambo maovu yakitendeka na Polepole akiwa kiongozi wa CCM, jee CCM yenyewe iliwahi kukaa kikao na kutoa tamko lolote au maelekezo kwa Serikali kukomesha yaliyokuwa yanatokea?
Leo Polepole anakikosoa chama chake na kwa sehemu usimamizi wa chama chake Kwa Serikali, jee asikilizwe na kuaminiwa au ahojiwe alikuwa wapi zama za Magufuli wakati maovu kama haya yakitokea?
Kama zama za Magufuli kulikuwa kuna uovu, na Sasa Kuna mfanano wa uovu ule ule, jee ni mambo ya Magufuli na Samia ama ndivyo CCM inavyotaka mambo yawe?
Maana kama Magufuli na Samia wote ni CCM na malalamiko dhidi Yao yanafanana, inawezekanaje kuitenga mbali CCM na uovu unaotokea badala yake tuwape watu wawili tu, yaani Magufuli na Samia?
Tatizo la Polepole ni kuusema ukweli ama ni yeye pia kutuhumiwa kuwa ni sehemu ya watenda maovu ila kwa Sasa watendao huo uovu si watu wa upande wake?
Wakati Polepole alipokuwa kiongozi wa CCM, aliyokuwa anayafanya yalikuwa na baraka za CCM au la. Kama yalikuwa ni mambo yake binafsi CCM waliwahi kumuonya?
Zama za Magufuli mambo maovu yakitendeka na Polepole akiwa kiongozi wa CCM, jee CCM yenyewe iliwahi kukaa kikao na kutoa tamko lolote au maelekezo kwa Serikali kukomesha yaliyokuwa yanatokea?
Leo Polepole anakikosoa chama chake na kwa sehemu usimamizi wa chama chake Kwa Serikali, jee asikilizwe na kuaminiwa au ahojiwe alikuwa wapi zama za Magufuli wakati maovu kama haya yakitokea?
Kama zama za Magufuli kulikuwa kuna uovu, na Sasa Kuna mfanano wa uovu ule ule, jee ni mambo ya Magufuli na Samia ama ndivyo CCM inavyotaka mambo yawe?
Maana kama Magufuli na Samia wote ni CCM na malalamiko dhidi Yao yanafanana, inawezekanaje kuitenga mbali CCM na uovu unaotokea badala yake tuwape watu wawili tu, yaani Magufuli na Samia?
Tatizo la Polepole ni kuusema ukweli ama ni yeye pia kutuhumiwa kuwa ni sehemu ya watenda maovu ila kwa Sasa watendao huo uovu si watu wa upande wake?