Mnanenepa sana wadada

Tatizo hili ni kwa wanaume mpaka wanawake, wazee kwa vijana. Kuna watu wanakula mchana utadhani hana uhakika wa kula baadaye. Kula kula kula ndo mavitambi hayo!

Mazoezi jamani kwa mji wa Dar yataka moyo. Wengi watu wa kawaida hawawezi kuweka mashine za mazoezi nyumbani. Una chumba kimoja nyumba imejaa ndi hata pa kuruka kamba hakuna. Uswazi mashimo barabarani!
Tabu nyingine foleni ukitoka kazini saa 11 unafika nyumbani saa mbili usiku na unalala unaondoka saa 11 asubuhi. Mazoezi tunayoyazungumzia jamani ni yepi? Na msiseme ya kufanyia chumbani.

Uduni na umasikini wa ki TZ na mazoezi wengi hawawezi. Jamaa mmoja aliamua ku jog mtaani kwako. Barabara mashimoooo. Si akaingia kwenye shimo alianguka na kitambi chake pwaaaa. Zaidi ya hayo MOI wakampokea na kumpa POP. Hajarudia!

Cha muhimu-watch your diet!



Mkuu. Lakini si kuna mwisho wa juma? Tumia mwisho wa juma kufanya mazoezi hata kwa saa 1 kwa siku. Inasaidia sana.

Pia hata siku za kazi unaweza kubadili mienendo kidogo. Punguza kutumia chombo cha usafiri kwa eneo ambalo unaweza kutembea kwa miguu. Pia tumia ngazi badala ya escalators.

Hayo pia uendana na lishe yenye kuzingatia virutubisho muhimu tu kwa mwili.
 
Loh mi nimenenepa balaa, miez kadhaa niliumwa nikakoonda, watu wakasema hata sipendez, mara ooh umekuwa mbaya..n.k nimepona na kutokana na lishe ya kubalance mwil nimenenepa balaa nina kilo 77, mpaka boy wangu anasema nipungue, siku izi kama wiki sasa nimeanza mazoez ya kutembea mwendo mrefu mana hela ya gym sina bt huwez amini leo nimekutana na shem wangu ananiambia mbona unanenepa ivo, na nguvu zimeisha nimetaman hata kulia, kuingia JF, ili kutuliza mawazo nakutana na masimango mengne, loh mwaka nimeuwanza vibaya, lol.
 
yani unakuta jitu linajinenepea kama kimbofa, afu akianza kusaidiwa huko nje na "wanaojua kuiweka miili yao fit" linaanza kulalamika
 
nani kakudanganya kuwa kuwa wenye vitambi hawana mvuto? Hujajua raha ya kitambi cha binti wewe... Sie wengine ndo ugonjwa wetu huo
duh kweli, ''people differ in taste and preference'' kama ndo hivi.
 
kwel watu tunatofautiana, mie nina kg45 mbaya zaid cyo mrefu na nina kababy face basi naonekana ka mtoto yan nakula mpaka ila haka kamwili kamegoma nataman kunywa hata mafuta yan nautaman unene kwa kwel
 
kwel watu tunatofautiana, mie nina kg45 mbaya zaid cyo mrefu na nina kababy face basi naonekana ka mtoto yan nakula mpaka ila haka kamwili kamegoma nataman kunywa hata mafuta yan nautaman unene kwa kwel

Unautamani unene? Nenepa kidogo tu ndugu, ukinenepa sana si ndo utakuwa mfupi zaidi!!
 
Unautamani unene? Nenepa kidogo tu ndugu, ukinenepa sana si ndo utakuwa mfupi zaidi!!

hahaha na kwel ntakuwa pipilo... ila atlist nifike 50kg jaman maana now ni kama katoto cha darasa la 5
 
Back
Top Bottom