Private-eye
JF-Expert Member
- Sep 8, 2013
- 1,069
- 1,211
Wadau wa uchumi wa kati- nawasalimu.
Nianze kwa kutoa pongezi za dhati sana kwa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kuanzisha mnada wa kuuza bidhaa mbalimbali mtandaoni ( Online Auction). Binafsi nimefaidika na huduma hii mara kadhaa. Kwa hakika hii ni moja ya hatua nzuri sana kwa TRA. Pongezi sana kwako Kamishna Mkuu na taasisi yote kwa ujumla.
Hata hvyo siku za karibuni nimeanza kupatwa na mashaka jinsi mnada unavyomalizika.
Kinachonitia mashaka ni muda wa mnada kuisha kabla ya wakati ulioainishwa kwenye mtandao. Mfano tarehe 12/10/2020 mnada ulifungwa dakika moja na sekunde karibu 40 kabla ya muda. Hii si sawa hata kidogo.
Jambo la mnada kuisha dakika moja au sekunde kadhaa kabla ya muda ni suala ambalo nimeliona mara kadhaa sio katika tarehe tajwa pekee.
Kinachotia shaka hapa ni kwamba, kufunga mnada kabla ya muda kunaweza kumaanisha kwamba watu wenye "connection" wanawasiliana na watu wa "IT" ndani ya TRA ambao kwa ujuzi flan flan ama wanazima network au wanasitisha mnada sekunde kadhaa kabla ya muda.....hii inapelekea mtu mwenye "connection" kushinda kabla ya kuisha mnada.....yaani yeye ndio anakuwa mtu wa mwisho wa kuweka dau.
Changamoto hii haikuwapo wakati mnada huu unaanza desemba mwaka jana. Kipindi cha nyuma mnada ulikuwa ukisemwa unaisha saa 3 kamili basi ni saa 3 kamili...sio kasoro wala nini.
Hii binafsi inanipa mashaka na pengine ni kiashiria cha janjajanja ndani ya mfumo wa mnada. Lakini pengine kuna maelezo ya kiufundi....ambayo yanaweza kuondoa mashaka haya.
Binafsi napendekeza Commission General TRA atupie jicho eneo hili. Tuwekane sawa. Fursa iwe sawa kwelikweli.
Changamoto ingine....ni swala la invoice za mtandaoni kukosa control number ya malipo. Yaani ukishinda mnada unaprint invoice unakwenda TRA- wao ndio wakupe control number. Nadhan timu ya ufundi TRA ilitizame hili jambo, invoice itoke ikiwa kamilifu ili mambo yaende kidigital kweli kweli.
Changamoto ingine ni swala la magari haya kuuzwa kabla ya kuwa na kibali cha ubora kutoka TBS. Yaani unanunua gari unalipa kila kitu kisha unaenda TBS walikague kama linafaa kuingia au kutumika nchini.
Hili swala la ukaguzi maanake ni kwamba kuna uwezekano ukanunua gari mnadani kisha TBS/NIT wakasema halifai kutumika TZ ikapelekea mteja kupata hasara.
Napendekeza kwamba, NIT/TBS wakakague mali zote zinazouzwa kisha gharama zao za ukaguzi zijumuishwe kwenye bei ya mnada....ili kuepuasha uwezekano wa mteja kupata hasara ikiwa mali aliyonunua haifai kutumika nchini.
Changamoto ingine....ambayo sijui ni ya TRA au TPA au nani. Ni swala la upigaji picha wa mali zinazouzwa hasa magari.
Kuna nyakati unaona picha hata unashangaa kama mpiga picha alikuwa ana nia ya kupiga picha au lah!!. Yaan picha zote zinaonesha eneo moja tu la gari.....ama matairi tu au pengine mbele tu nk.
Hili la picha linaambatana na taarifa zisizotosha kuhusu gari au kifaa kinachouzwa....mfano unakuta gari inauzwa ila haioneshi ni manual au auto, aina ya mafuta inayotumia, eneo ambalo gari ipo, ukubwa wa injin n.k. Nadhan hizi ni taarifa muhimu sana kwa mnunuzi. Tunaomba improvement eneo hili.
Changamoto nyingine ambayo nimeiona....ni swala la namna ya kumruhusu mtu mwingine (third party) kuchukua mali uliyokwisha kulipia kwa niaba yako.
Mfano nimeshinda na kulipia mali iliyoko Bukoba nami niko Mtwara....natumia utaratibu gan ili mtu mwingine aweze kuchukua hiyo mali kwa niaba yangu?
Nadhan hili haliko wazi sana....napendekeza liwekwe bayana sana ili tuweze kununua na mali popote TZ bila kulazimika kwenda kufanya clearence sisi binafsi.
Changamoto nyingine ya ziada ambayo sio ya TRA kama taasisi ....nadhan ni ya mtu binafsi, ni kuhusu utaratibu wa kukagua magari na bidhaa pale yard ya ubungo.
Pale ubungo...pana mlinzi anaitwa Wambura....huyu bwana ni mnyanyasaji wa wateja sana. Amejaa kiburi na kisirani sana. Yaani ukienda pale kukagua mali zinazouzwa hadi uruhusiwe ni shida sana.
Tunabembeleza sana kupata ruhusa ya kuingia yard ...kiasi kwamba inakuwa ni kama msaada kukagua mali wakati kanuni za mnada zinaruhusu kukagua mali kabla ya kununua.
Napendekeza kwamba huyu bwana ama afundishwe namna bora ya kuhudumia wateja au abadilishwe apelekwe eneo ambalo si lazima kukutana na wateja. Pia pawekwe ratiba maalumu ieleweke ni muda gani wateja wanaruhusiwa kuja kukagua mali badala ya kutegemea hekima ya walinzi.
Namaliza kwa kusema, licha ya changamoto zote tajwa hapo juu, bado mnada huu wa online ni bora mara 1000 zaidi ya kile kilichokuwa kinafanyika zamani.....kwa hili nawapa kongole sana.
Pamoja katika uchumi wa kati.
Asante
UPDATE:
Wanajukwaa ....nawasalamia !
Naomba kuchukua fursa hii kutoa mrejesho wa baadhi ya changamoto nilizozitoa wiki kadhaa kuhusu mnada wa TRA.
Nawapongeza sana TRA kwa kushughulikia maswala haya muhimu:
1. Hongera TRA kwa kuhakikisha kuwa control number zinatoka moja kwa moja kwenye hati ya malipo. Haya ni mafanikio makubwa sana.
Hapa mmeondoa adha ya msingi sana....iliyomtaka mnunuzi afike ofis za TRA kupata control number......hongera sana....!
2. Nimefarijika sana na mabadiliko aliyonayo bwana wambura pale yard ya ubungo. Amejirekebisha sana.....huduma yake kwa sasa ni bora mara 10 zaidi ya hapo zamani. Nina iman kwamba ataendelea kuwa na weledi huo kadri siku zonavyosonga.
Kwa sasa huu ndo uzoefu wangu mpya.....nikaona si vibaya kupongeza pale kero zinapotatuliwa.
Asante.
Nianze kwa kutoa pongezi za dhati sana kwa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kuanzisha mnada wa kuuza bidhaa mbalimbali mtandaoni ( Online Auction). Binafsi nimefaidika na huduma hii mara kadhaa. Kwa hakika hii ni moja ya hatua nzuri sana kwa TRA. Pongezi sana kwako Kamishna Mkuu na taasisi yote kwa ujumla.
Hata hvyo siku za karibuni nimeanza kupatwa na mashaka jinsi mnada unavyomalizika.
Kinachonitia mashaka ni muda wa mnada kuisha kabla ya wakati ulioainishwa kwenye mtandao. Mfano tarehe 12/10/2020 mnada ulifungwa dakika moja na sekunde karibu 40 kabla ya muda. Hii si sawa hata kidogo.
Jambo la mnada kuisha dakika moja au sekunde kadhaa kabla ya muda ni suala ambalo nimeliona mara kadhaa sio katika tarehe tajwa pekee.
Kinachotia shaka hapa ni kwamba, kufunga mnada kabla ya muda kunaweza kumaanisha kwamba watu wenye "connection" wanawasiliana na watu wa "IT" ndani ya TRA ambao kwa ujuzi flan flan ama wanazima network au wanasitisha mnada sekunde kadhaa kabla ya muda.....hii inapelekea mtu mwenye "connection" kushinda kabla ya kuisha mnada.....yaani yeye ndio anakuwa mtu wa mwisho wa kuweka dau.
Changamoto hii haikuwapo wakati mnada huu unaanza desemba mwaka jana. Kipindi cha nyuma mnada ulikuwa ukisemwa unaisha saa 3 kamili basi ni saa 3 kamili...sio kasoro wala nini.
Hii binafsi inanipa mashaka na pengine ni kiashiria cha janjajanja ndani ya mfumo wa mnada. Lakini pengine kuna maelezo ya kiufundi....ambayo yanaweza kuondoa mashaka haya.
Binafsi napendekeza Commission General TRA atupie jicho eneo hili. Tuwekane sawa. Fursa iwe sawa kwelikweli.
Changamoto ingine....ni swala la invoice za mtandaoni kukosa control number ya malipo. Yaani ukishinda mnada unaprint invoice unakwenda TRA- wao ndio wakupe control number. Nadhan timu ya ufundi TRA ilitizame hili jambo, invoice itoke ikiwa kamilifu ili mambo yaende kidigital kweli kweli.
Changamoto ingine ni swala la magari haya kuuzwa kabla ya kuwa na kibali cha ubora kutoka TBS. Yaani unanunua gari unalipa kila kitu kisha unaenda TBS walikague kama linafaa kuingia au kutumika nchini.
Hili swala la ukaguzi maanake ni kwamba kuna uwezekano ukanunua gari mnadani kisha TBS/NIT wakasema halifai kutumika TZ ikapelekea mteja kupata hasara.
Napendekeza kwamba, NIT/TBS wakakague mali zote zinazouzwa kisha gharama zao za ukaguzi zijumuishwe kwenye bei ya mnada....ili kuepuasha uwezekano wa mteja kupata hasara ikiwa mali aliyonunua haifai kutumika nchini.
Changamoto ingine....ambayo sijui ni ya TRA au TPA au nani. Ni swala la upigaji picha wa mali zinazouzwa hasa magari.
Kuna nyakati unaona picha hata unashangaa kama mpiga picha alikuwa ana nia ya kupiga picha au lah!!. Yaan picha zote zinaonesha eneo moja tu la gari.....ama matairi tu au pengine mbele tu nk.
Hili la picha linaambatana na taarifa zisizotosha kuhusu gari au kifaa kinachouzwa....mfano unakuta gari inauzwa ila haioneshi ni manual au auto, aina ya mafuta inayotumia, eneo ambalo gari ipo, ukubwa wa injin n.k. Nadhan hizi ni taarifa muhimu sana kwa mnunuzi. Tunaomba improvement eneo hili.
Changamoto nyingine ambayo nimeiona....ni swala la namna ya kumruhusu mtu mwingine (third party) kuchukua mali uliyokwisha kulipia kwa niaba yako.
Mfano nimeshinda na kulipia mali iliyoko Bukoba nami niko Mtwara....natumia utaratibu gan ili mtu mwingine aweze kuchukua hiyo mali kwa niaba yangu?
Nadhan hili haliko wazi sana....napendekeza liwekwe bayana sana ili tuweze kununua na mali popote TZ bila kulazimika kwenda kufanya clearence sisi binafsi.
Changamoto nyingine ya ziada ambayo sio ya TRA kama taasisi ....nadhan ni ya mtu binafsi, ni kuhusu utaratibu wa kukagua magari na bidhaa pale yard ya ubungo.
Pale ubungo...pana mlinzi anaitwa Wambura....huyu bwana ni mnyanyasaji wa wateja sana. Amejaa kiburi na kisirani sana. Yaani ukienda pale kukagua mali zinazouzwa hadi uruhusiwe ni shida sana.
Tunabembeleza sana kupata ruhusa ya kuingia yard ...kiasi kwamba inakuwa ni kama msaada kukagua mali wakati kanuni za mnada zinaruhusu kukagua mali kabla ya kununua.
Napendekeza kwamba huyu bwana ama afundishwe namna bora ya kuhudumia wateja au abadilishwe apelekwe eneo ambalo si lazima kukutana na wateja. Pia pawekwe ratiba maalumu ieleweke ni muda gani wateja wanaruhusiwa kuja kukagua mali badala ya kutegemea hekima ya walinzi.
Namaliza kwa kusema, licha ya changamoto zote tajwa hapo juu, bado mnada huu wa online ni bora mara 1000 zaidi ya kile kilichokuwa kinafanyika zamani.....kwa hili nawapa kongole sana.
Pamoja katika uchumi wa kati.
Asante
UPDATE:
Wanajukwaa ....nawasalamia !
Naomba kuchukua fursa hii kutoa mrejesho wa baadhi ya changamoto nilizozitoa wiki kadhaa kuhusu mnada wa TRA.
Nawapongeza sana TRA kwa kushughulikia maswala haya muhimu:
1. Hongera TRA kwa kuhakikisha kuwa control number zinatoka moja kwa moja kwenye hati ya malipo. Haya ni mafanikio makubwa sana.
Hapa mmeondoa adha ya msingi sana....iliyomtaka mnunuzi afike ofis za TRA kupata control number......hongera sana....!
2. Nimefarijika sana na mabadiliko aliyonayo bwana wambura pale yard ya ubungo. Amejirekebisha sana.....huduma yake kwa sasa ni bora mara 10 zaidi ya hapo zamani. Nina iman kwamba ataendelea kuwa na weledi huo kadri siku zonavyosonga.
Kwa sasa huu ndo uzoefu wangu mpya.....nikaona si vibaya kupongeza pale kero zinapotatuliwa.
Asante.