Mmarekani, Mhaya na Mjapani walikutana ndani Sauna kwenye Hotel ya Hilton Manhattam Jijini New York. Wote wakiwa uchi wakifurahia unyunyuunyunyu wa kwenye Sauna. Ghafla Mmarekana akafanya kama anapangusa mdomo akasikika akisema "hallo Honey....." Wakamuuliza inakuwaje, akasema anawasiliana na mkewe aliyeko London kwa njia ya simu ambayo simu kadi yake imeweka ndani ya kiganja chake cha mkono. Wakaendelea kula kimvuke cha sauna mara ghafla Mjapani naye akanyoosha mkono kama anajifanyia manicure akaonekana anasoma kitu kama picha na mafaili kwenye kucha zake, wakamuuliza vipi, akajibu akasema anadownload file la mkutano lililotumwa na Boss wake toka Tokyo kutoka kwenye iPad2 yake iliyochimbiwa chini ya kucha yake. Mhaya akasema hapa sasa mimi nionyeshe advertsement gani? Akaondoka kwa hasira akaenda WC aliporudi akawa ameecha Toilet Papers inaninginia matakoni mwake. Wenzake wakamuuliza vipi, akawajibu akasema "Napokea Fax toka kwa Professa Rutahindirwa wa Havard School of Law"