Mliowahi kuishi vijijini

Mliowahi kuishi vijijini

Kiti cha uvivu.......siju kwanini tulikiita hivyo???

Pole Elli;
Una miaka mingapi weye?? Kiliitwa kwa lugha yetu hivi; Kitima kya ufifu. Si kweli walikiita ka ulivyosema.
 
Sio kweli kwamba kilitumiwa ba babu zetu enzi hizo, hata sisi tumekikuta tjmekitumia na mpaka leo bado vipo kwa baadhi ya watu.

Bi viti imara na vizuri sana.
 
Hicho kiti sio kigeni kabisa Moyoni mwangu!
 
Kiti cha uvivu.......siju kwanini tulikiita hivyo???

mpwa kitu cha uvivu ni kile walikuwa wanaweka either gunia au kitambaa ndio sehemu ya kukalia.
 
ni kweli hiki kiti kilikuwepo ila sikuwahi kulisikia jina lake
 
Sio kweli kwamba kilitumiwa ba babu zetu enzi hizo, hata sisi tumekikuta tjmekitumia na mpaka leo bado vipo kwa baadhi ya watu.

Bi viti imara na vizuri sana.

Sasa Unachobisha Ni Nini Wakati Wewe Ulikuwa Mtoto Kwa Wakati Huo
 
kiti kimeniangusha sana iko nikiwa mdogo,ukikaa kwa mbele(kwa ajili ya ufupi)kinabinuka then kile kiegamio kinapiga kichwani!umenikumbusha mbali sana mzee!

Kinaitwa kiti cha muegamo, kimenipiga sana kichwani, home vimebaki viwili, nitakupa kimoja
 
kiti kimeniangusha sana iko nikiwa mdogo,ukikaa kwa mbele(kwa ajili ya ufupi)kinabinuka then kile kiegamio kinapiga kichwani!umenikumbusha mbali sana mzee!

Umenichekesha na kunikumbusha mbali sana mkuu, kwani hayo uliyoandika ndo yaliyokua yakinikuta hata mimi. Mbaya zaidi kuna wakati kiliniangusha tukiwa tunaota moto wa mkaa kwenye kigae na kunifanya niungue sehemu za magoti, bahati nzuri kulikua na wakubwa na kwa sababu nilikua mtoto makovu yake kwa sasa yanaonekana kwa mbali sana.
 
Kiliitwa kiti cha marimba nitarudi kijijini nikakitafute kiti cha marehem babu,,,
 
Back
Top Bottom