Mlimani TV: Leo tutakuwa na Humphrey Polepole

Mlimani TV: Leo tutakuwa na Humphrey Polepole

Mlimani TV

Member
Joined
Oct 13, 2014
Posts
12
Reaction score
12
Katika kipindi cha keki ya taifa kinachorushwa kila Jumatatu saa mbili na nusu mpaka tatu na nusu hapa MLIMANI TV (chanel 114 startimes) leo tutakuwa na mjumbe wa iliyokuwa tume ya mabadiliko ya katiba ndugu Humphrey Polepole,atatizama kwa makini utofauti kati ya rasimu ya pili ya katiba pamoja na katiba pendekezwa.

Je, ungependa kusikia nini? Unaweza tuma maoni yako hapa na hapo saa mbili na nusu wakati wa kipindi yatasomwa moja kwa moja.

Mlimani TV elimu kwanza.
 
mimi nawashauri hawa wanaharakati kupigana mstari wa mbele wasiwe kama wanasiasa kwani wanasiasa si waaminifu wakifutwa chemba tu wanageuka.
 
Hivi huyu Polepole kazi yake ni majungu tu? Namhurumia sana ni kijana mdogo ila anaburuzwa na wazee akina Warioba
 
mimi nawashauri hawa wanaharakati kupigana mstari wa mbele wasiwe kama wanasiasa kwani wanasiasa si waaminifu wakifutwa chemba tu wanageuka.
Cha kushangaza ni kwamba wanaharakati wamekuwa vibarua wa wanasiasa
 
Kwa sasa sioni kama maoni yatasaidia.
 
Tanzania hakuna kitu kitakacho badilika hadi Watanganyika tujitambue ! Tumwombe Mungu aendelee kuwapa nguvu Wazanzibar waikatae katibu hii ya kifisadi
 
Ninavyoamini mim Zanzibar haishindwi kuchangia muungano ila kwa muundo ulivyo sasa imekoma kuchangia, ni vema tukaelewa mantiki ya Zanzibar na kuheshimu mahitaji ya muungano wa serikali tatu. Ni kuionea sana Tanganyika na KUWAFEDHEHESHA wanzibar kuendelea kuwa na serikali ya zanzibar ile hali Tanganyika haipo, mambo ya Tanganyika yakisimamiwa na Muungano Zanzibar inabaki yatima kiaina fulani hivi.
 
Ningependa Polepole aniambie kama kuna ukweli katika Kauli ya Mwenyekiti wa Kamati ya Uandishi katika Bunge la Katiba Mtemi Andrew Chenge kwamba KATIBA INAYOPENDEKEZWA imebeba asilimia 81 ya mambo ambayo yalikuwamo katika RASIMU YA PILI YA KATIBA iliyokabidhiwa na Jaji Warioba kwa Rais Kikwete.

Jambo hili pia liliungwa mkono na Rais Kikwete wakati alipopokea Katiba inayopendekezwa mjini Dodoma kuwa ni kweli asilimia 81 ya yale yaliyokuwemo katika Rasimu ya Warioba yamo pia katika hii ninayoiita mia 'Katiba ya Sitta'. Kuna ukweli kiasi gani katika hili?

Ngoja nichape kazi kisha nitakuja na maswali zaidi kwa Polepole na nitakiangalia kipindi chenu niweze kupiga simu maana mmesema kitakuwa moja kwa moja (LIVE)
 
Hivi huyu Polepole kazi yake ni majungu tu? Namhurumia sana ni kijana mdogo ila anaburuzwa na wazee akina Warioba

sema kweli Polepole anaiyumbisha sana CCM na kwa kiasi kikubwa mchango wake unasaidia sana ccm kushindwa kuchukua dola 2015.
 
Hivi huyu Polepole kazi yake ni majungu tu? Namhurumia sana ni kijana mdogo ila anaburuzwa na wazee akina Warioba
unaonekana una kipaji cha kuimba taarabu mtafute mzee Yusufu huenda ukapata ajira
ccm ni wapuuzi sana
 
Tuko pamoja katika kuikataa katiba ya Sitta name Chenge sababu mambo yote muhimu wameyafuta. Hoja ya asilimia haina mashiko yenyewe waisema ili kuuhadaa umma wa watanzania. Wameifuta Tanganyika, wamefuta tunu za taifa, wamefuta ukomo wa wabunge, wamefuta wabunge kuwajibishwa na waliowachagua, wamefuta wabunge kutokuwa mawaziri, wamebariki madaraka makubwa kwa raisi, wamebariki kuendelea na wakuu wa wilaya na mikoa. Wameondoa mambo yote yenye kuweka check and balance. Walichokiacha kama sio makapi ni nini?
 
1. Mr Humphrey polepole, unadhani/unaamini 2/3 ilipatikana bila kuchakachua?
2. Mchakato uliharibikia wapi? kwenye sheria ya mabadiliko,uteuzi wa wajumbe au sehemu ipi?
 
Mimi nauliza hasa ile tume ya Warioba ilikuwa na mamlaka gani maana katika mchakato huu naona ile tume ya Warioba ilikuwa kanyaboa tu maana sisi tulitoa maoni mbele ya tume na tukaambiwa kuwa tume hiyo ndio ilikuwa na mamlaka ya kukusanya maoni pekee na kutoa rasimu ya 1 na 2 sasa haya waliyoyatia wao wameyatoa wapi?.Mimi sielewi kabisa maana siku hiyo niliacha kazi zangu na kupanga foleni kwenye jua kusubiri zamu yangu sasa kama walijua kitakachotokea je haikuwa makusudi kutupotezea muda na kuharibu pesa za umma?
 
Swali kwa Polepole

1. Baada ya mapito yote ambayo Katiba inayopendekezwa imepitia, ni kweli kuna mwelekeo wa kuipata katiba halisi ya Tanzania ambayo itadumu kwa miaka mingine 50 ijayo ama tunafunika kombe ili mwanaharamu apite?

2. Polepole na wajumbe wenzako wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, mlikuwa mnajisikiaje pale Jaji Warioba alipokuwa akishambuliwa binafsi na baadhi ya Wajumbe wa Bunge la Katiba huku nyie mkiachwa pembeni kana kwamba Warioba alijifungia kuandika Rasimu ya Katiba peke yake?
 
Swali kwa polepole: kama imedhihirika kweli 2/3 ya znz imechakachuliwa; kuna uwezekano wowote wa kuhoji uhalali wa mchakato huo mahakamani? Na kutafuta kuubatisha kabla ya kupiga kura.?
 
Back
Top Bottom