Mkwamo wa kuhamia Dodoma! Hili limesahaulika ama halikuzingatiwa

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,632
697,704
fuvu.jpg
Nipende kwa dhati kabisa ya moyo wangu kupongeza uamuzi wa kuhamia Dodoma kwa vitendo katika uongozi huu wa awamu ya tano...! Ni uthubutu uliomshinda hata muasisi wa Taifa hili hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere(mchonga meno)

Kutokana na ratiba iliyotangazwa mwaka jana ilitakiwa kufikia mwaka huu walau kuwe na wizara tatu ziwe tayari Dodoma

Kumekuwa na mikwamo katika hili...waziri mkuu ameweza kuhamia lakini kiuhalisia muda mwingi hakai huko, mambo mengi ya kiserikali bado yanafanyika Dar es salaam! Pengine hata mahitaji ya nyakati yamechangia
Zinaweza kutolewa sababu lukuki na visingizio si haba lakini kuna jambo muhimu sana halikuzingatiwa!!! Nalo si jingine bali ni mila na desturi! Matambiko mizimu na kuheshimu mambo ya
jadi

weirdafricantraditions.jpg

Pamoja na kuwa 'brainwashed' na imani na elimu ya wageni lakini bado mila na desturi zetu zina nguvu sana na yeyote aliyejaribu kuzidharau amepata habari yake

Dodoma pale mlimani kuna simulizi zisizokoma kuhusiana na hilo..japo watu wanasimuliana kwa kificho na kwa woga...wanasisitiza kuwa wazee wa mila mababu na mizimu hawakuombwa ruhusa, walitengwa na hawakushirikishwa ili watoe baraka na ruhusa! Wanasisitiza kuwa kuufanya mji fulani kuwa ndio kitovu na kuvikwa taji la mji mkuu wa nchi sio jambo dogo hata kidogo

Ni jambo linalohusika na mabilioni ya shilingi mwingiliano wa mila na tamaduni mbalimbali ndani na nje ya nchi, ni jambo ambayo maandalizi na utekelezaji wake unatakiwa kwenda sambamba kidunia na kiroho ....hili wanasema halikufanyika na kwa imani hata za kidini jambo lolote lisipopata baraka za kiroho katika ulimwengu usioonekana ni vigumu kutekelezeka hata katika ulimwengu wa nuru sayansi na technologia

Kama miradi ya kawaida kama madaraja barabara majengo viwanda nk vinafanyiwa matambiko sembuse mji mkuu?

Kuna kitu hakikutiliwa maanani kwenye mradi mzima wa kuhamia Dodoma..kitu hiki kikiendelea kudharauliwa kitaendelea kupukutisha watendaji wengi pale penye kitovu na kuhamia Dodoma kutabaki kuwa story za kufikirika
vifaa-300x224.jpg
 
View attachment 462075 Nipende kwa dhati kabisa ya moyo wangu kupongeza uamuzi wa kuhamia Dodoma kwa vitendo katika uongozi huu wa awamu ya tano...! Ni uthubutu uliomshinda hata muasisi wa Taifa hili hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere(mchonga meno)
Kutokana na ratiba iliyotangazwa mwaka jana ilitakiwa kufikia mwaka huu walau kuwe na wizara tatu ziwe tayari Dodoma
Kumekuwa na mikwamo katika hili...waziri mkuu ameweza kuhamia lakini kiuhalisia muda mwingi hakai huko, mambo mengi ya kiserikali bado yanafanyika Dar es salaam! Pengine hata mahitaji ya nyakati yamechangia
Zinaweza kutolewa sababu lukuki na visingizio si haba lakini kuna jambo muhimu sana halikuzingatiwa!!! Nalo si jingine bali ni mila na desturi! Matambiko mizimu na kuheshimu mambo ya jadiView attachment 462079
Pamoja na kuwa 'brainwashed' na imani na elimu ya wageni lakini bado mila na desturi zetu zina nguvu sana na yeyote aliyejaribu kuzidharau amepata habari yake
Dodoma pale mlimani kuna simulizi zisizokoma kuhusiana na hilo..japo watu wanasimuliana kwa kificho na kwa woga...wanasisitiza kuwa wazee wa mila mababu na mizimu hawakuombwa ruhusa, walitengwa na hawakushirikishwa ili watoe baraka na ruhusa! Wanasisitiza kuwa kuufanya mji fulani kuwa ndio kitovu na kuvikwa taji la mji mkuu wa nchi sio jambo dogo hata kidogo
Ni jambo linalohusika na mabilioni ya shilingi mwingiliano wa mila na tamaduni mbalimbali ndani na nje ya nchi, ni jambo ambayo maandalizi na utekelezaji wake unatakiwa kwenda sambamba kidunia na kiroho ....hili wanasema halikufanyika na kwa imani hata za kidini jambo lolote lisipopata baraka za kiroho katika ulimwengu usioonekana ni vigumu kutekelezeka hata katika ulimwengu wa nuru sayansi na technologia
Kama miradi ya kawaida kama madaraja barabara majengo viwanda nk vinafanyiwa matambiko sembuse mji mkuu?
Kuna kitu hakikutiliwa maanani kwenye mradi mzima wa kuhamia Dodoma..kitu hiki kikiendelea kudharauliwa kitaendelea kupukutisha watendaji wengi pale penye kitovu na kuhamia Dodoma kutabaki kuwa story za kufikirika View attachment 462076
Acha kuropoka ewe mtu mzima. Safari ipo pale pale
 
Mkuu kudos sana.. Japo nimebaki chenga chenga sijaelewa kabisa
Kila tunachofanya kimwili ni lazima kipate kibali cha kiroho na hufanya hivyo kwa mualiko maalum angalia kwenye milo yetu ama sherehe zetu mbalimbali ni lazima tuwasiliane na ulimwengu wa roho
Hivi hili la kuhamia Dodoma je tulishawahi kuwaalika japo viongozi wa dini zetu hizi na wananchi na kufanya dua ya pamoja huku tukishiriki mlo wa pamoja? Je kuna dua rami walau kwa imani zetu zilishawahi kusomwa na kuchagua tarehe moja maalum iwe kama ndio kifunguo rasmi cha kuhamia Dodoma? Haya mambo huwa hayafanyiki kienyeji tu kwa kutegemea elimu zetu hizi na maarifa ya kukopea
 
Kila tunachofanya kimwili ni lazima kipate kibali cha kiroho na hufanya hivyo kwa mualiko maalum angalia kwenye milo yetu ama sherehe zetu mbalimbali ni lazima tuwasiliane na ulimwengu wa roho
Hivi hili la kuhamia Dodoma je tulishawahi kuwaalika japo viongozi wa dini zetu hizi na wananchi na kufanya dua ya pamoja huku tukishiriki mlo wa pamoja? Je kuna dua rami walau kwa imani zetu zilishawahi kusomwa na kuchagua tarehe moja maalum iwe kama ndio kifunguo rasmi cha kuhamia Dodoma? Haya mambo huwa hayafanyiki kienyeji tu kwa kutegemea elimu zetu hizi na maarifa ya kukopea
Yawezekana Mkulu Magogoni yuko online anaweza akapata point hapa
 
Kunaweza kuwa na ukweli maana hatutaki kutambua matambiko yetu ya asili, wengi wetu tumetekwa na imani za kutoka ''dini zile mbili '' zenye chimbuko la kutoka Mashariki ya Kati.
 
Back
Top Bottom