hazole1
JF-Expert Member
- Jan 3, 2015
- 4,319
- 3,911
Mkuu wa wilaya ya Kilombero, James Ihunyo amepiga marufuku mtu yeyote kufanya sherehe bila kibali kutoka kwa mtendaji wa eneo husika ikiwa ni pamoja na kuuza chakula kiholela kama njia ya kuthibiti utumiaji hovyo wa chakula.
Ihunyo amesema ameamua kupiga marufuku hiyo ili kuthibiti utumiaji hovyo wa chakula kilichopatikana msimu huu wa mavuno na kujikinga na baa la njaa katika wilaya yake.
Mkuu wa wilaya hiyo ya Kilombero akiongea leo kwenye kikao cha baraza la madiwani la mji wa Ifakara Ihunyo amesema serikali yake ya wilaya imejipanga kuhakikisha sherehe zisizo za lazima hazifanyiki na kuwataka Watendaji na Madiwani kushirikiana kukemea vitendo hivyo.
Mbali na hilo Diwani wa Kata ya Viwanja Stini amelalamika ucheleweshaji wa fedha kutoka serikali kuu na kudai jambo hilo linakuwa linakwamisha mipango ya maendeleo katika halmshauri hiyo na kata zake.
Awali kabla ya kikao hicho kuanza Mbunge viti maalum mkoa wa Morogoro kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) mchungaji Getruda Lwakatare aliapishwa kuwa mjumbe kamili wa baraza hilo la madiwani.
My take:
Hawa wakuu wa wilaya wamekuwa kama mzigo kwa wananchi. kwa maagizo yasiyo isha na hii yote hii ni kutokana hawajui machungu ya kuchaguliwa na wananchi.
na ndio maana wamekuwa walopokaji isivyo kawaida.
Kama imgewezekana hii nafasi ya ukuu wa wilaya ingefutwa kabisa kwa sababu hamna kitu wanacho wasaidia wananchi.
Embe fikiria kwa akili ya kawaida tu.mtu ukitaka kumuwekea mtoto happy birthday. mkuu wa wilaya anakuambia hadi ukachukue kibali serikalini.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ihunyo amesema ameamua kupiga marufuku hiyo ili kuthibiti utumiaji hovyo wa chakula kilichopatikana msimu huu wa mavuno na kujikinga na baa la njaa katika wilaya yake.
Mkuu wa wilaya hiyo ya Kilombero akiongea leo kwenye kikao cha baraza la madiwani la mji wa Ifakara Ihunyo amesema serikali yake ya wilaya imejipanga kuhakikisha sherehe zisizo za lazima hazifanyiki na kuwataka Watendaji na Madiwani kushirikiana kukemea vitendo hivyo.
Mbali na hilo Diwani wa Kata ya Viwanja Stini amelalamika ucheleweshaji wa fedha kutoka serikali kuu na kudai jambo hilo linakuwa linakwamisha mipango ya maendeleo katika halmshauri hiyo na kata zake.
Awali kabla ya kikao hicho kuanza Mbunge viti maalum mkoa wa Morogoro kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) mchungaji Getruda Lwakatare aliapishwa kuwa mjumbe kamili wa baraza hilo la madiwani.
My take:
Hawa wakuu wa wilaya wamekuwa kama mzigo kwa wananchi. kwa maagizo yasiyo isha na hii yote hii ni kutokana hawajui machungu ya kuchaguliwa na wananchi.
na ndio maana wamekuwa walopokaji isivyo kawaida.
Kama imgewezekana hii nafasi ya ukuu wa wilaya ingefutwa kabisa kwa sababu hamna kitu wanacho wasaidia wananchi.
Embe fikiria kwa akili ya kawaida tu.mtu ukitaka kumuwekea mtoto happy birthday. mkuu wa wilaya anakuambia hadi ukachukue kibali serikalini.
Sent using Jamii Forums mobile app