Mkuu wa wilaya anapotofautiana na mkuu wa mkoa wake.

Mnasihi

JF-Expert Member
Oct 9, 2013
7,661
6,916
Kauli za kupishana kwa jambo moja lililopo eneo moja la kazi ni mzigo kwa taifa. Hili limewezekana hapa Dar juzi.

Mkuu wa wilaya ya Kinondoni aliwaambia walimu wasiotosheka na mshahara waondoke waende unakotosha. Pia akawaagiza walimu wasiwafungie wanafunzi waliochelewa mageti. Jana mkuu wa mkoa kawatahadharisha wanafunzi kutoitumia fursa ya elimu bure vibaya.

Huu ni mpishano wa kauli. Mkuu wa mkoa anahamasisha na mkuu wa wilaya anawatisha watoa elimu na kuwatetea wanafunzi wazembe na wavivu.
Naamini, kwa mpishano huu wa kauli Dar itaangukia pua kitaaluma mwaka huu.

Walimu hii siyo mara yao ya kwanza kuisikia kauli hii kwani iliwahi tolewa na Mwamtumu Mahiza akiwa naibu waziri wa elimu na mwisho wa siku kapotezwa kwenye medani za siasa. Sasa sijui na huyu anayewatisha walimu eti wapishe ilihali wana haki za msingi kudai mshahara unaotosha sijui kajipangaje kukabiliana na walimu pindi wakiamsha hisia zao.
 
Mbona siuoni huo utofauti wa maneno? Wanasiasa wakipata audience, kama akili yako sio sawa utapanic kwa maneno yao
 
Mleta Uzi uko sawa lakn? Mkuu wa wilaya kazungumzia kuhusu mageti kufungwa na Mkuu wa Mkoa kazungumzia kutoichezea fursa ya elimu bure.Wapi wametofautiana sasa maana kila mtu kaongelea masuala tofauti.
 
Vijana wa ufipa mmefundishwa kilakitu kupinga...hadi mtapinga kuzaliwa na wazazi wenu...
 
Kwakuwa wewe mleta uzi uliangukia pua 2015 sasa utaangukia meno mwaka huu na viuzi uzi vyako ambavyo havina tija wala mashiko. Unapomuombea mama yako wa kambo kifo mara nyingi matokeo yake huwa ni kinyume chake. Unadhani Dar ikiangukia pua kielemu nani wa kuumia kama si mtoto wako au wa ndugu yako?
 
Back
Top Bottom