Mkuu wa kituo cha Polisi Milongo Mwanza

Mkuu wa kituo cha Polisi Milongo Mwanza

BenMB

Member
Joined
Jul 15, 2017
Posts
25
Reaction score
41
Nikiwa raia mwema napenda kukujulisha kuwa Kuna klabu ya pombe za kienyeji mita kumi kutoka kituoni kwako, klabu hii ipo katikakati ya Makazi ya watu, na ilipo siyo rasmi, klabu hii inahatarisha afya ya raia kwa mazingira yake machafu, na mkusanyiko ambao pia ni hatari kwa janga hili la Corona, klabu hii inafanya biashara saa 24,serikali imeweka muda wa kufungua sehemu za biashara za vinywaji kama pombe lakini huyu muhusika sheria hii haimuhusu, tafadhali usisubiri maafa yatokee ndio uchukue hatua, mi nimekujulisha kabla,Corona ni hatari tuchukue hatua zuia huu msanyiko usiokuwa wa lazima

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtoa mada sijui kama unajua wateja wakubwa wa vilabu vya pombe mara nyingi ni walinzi wa raia na mali zao.

Mwanza hata madanguro hayapo mbali na vituo vya police.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vilabu vya namna hiyo vipo kila mahali Tanzania na ni sehemu ya maafande kujichukulia mgawo wao kila siku kwa ajili ya mboga na kubrashia viatu, haitatokea vifungwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom