Mkutano wavunjika baada ya viongozi kutoa risiti feki mkoani Arusha

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Mkutano ulioitishwa na viongozi wa mtaa wa Onjuvatian kata ya Sokoni One jijini Arusha umevunjika baada ya viongozi hao kushindwa kusoma mapato na matumizi ya fedha zao na pia kuwaonyesha risiti za vitu vilivyonunuliwa kwa fedha za michango yao.

Kabla ya mkutano huo kuvunjika wananchi hao waliwataka viongozi kuwasomea mapato na matumizi ya fedha zao walizochanga kwa muda wa miaka miwili na pia kuwaonyesha risiti ya manunuzi jambo ambalo licha ya viongozi hao kushindwa kulitekeleza walionyesha risiti bandia hali iliyoibua hasira kwa wananchi hao.

Baada ya hekaheka Mwenyekiti anayetuhumiwa Bw,Joseph Kimaro alikiri kutenda makosa hayo na akawaomba wananchi hao wamsamehe na kumpa muda wa kurekebisha makosa ombi ambalo hata hivyo wananchi hao walilikataa
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Fedha za wananchi kuchezewa? Hao viongozi wamshukuru sana Mungu maana wangepigwa kipigo cha mbwa na hao wananchi waliochanga hela!
 
Feti:- feki
Huo ni upuuz na kisheria ni kosa kughushi nyaraka.. Ili kumkomesha huyo tapeli wananchi wangechukua hatua stahiki ikiwemo kumpandisha kizimbani...
 
Nimeipata kwenye ukurasa wa ITV
itv.png
 
Jina lenyewe hilo linahakisi kweli. Ndo maana hawaaminiki kwa mkuu
 
Kawaida Arusha ukileta blah blah wananchi hawakuachi. Hii si mara ya kwanza wananchi Arusha kuwakomalia viongozi iwe wa kisiasa au hata akiyechaguliwa na watawala. Hapa unaona wananchi huku wanajua kuwajibisha viongozi sio kuogopa na kudanganywa kama mazuzu.
 
Ndio wanataka wapewe nchi kwa style hii.Hapo kwenye jina tuu unaona kabisa hapa kazi ipo.
 
Back
Top Bottom