Anselm
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 1,710
- 291
Can U imagine bila usajili wa Mshambuliaji Mrisho Ngassa na beki kisiki Mbuyi Twite mkutano wa wana Msimbazi leo ungekuwaje...issue ya kula rambirambi za Mafisango(RIP) (kwani wako wana Simba wengi tu hawakubaliani na kitendo kile),kuboronga kwa team kwenye Kagame huku wakipata fedheha mbele ya kadamnasi kwa kuchapwa kipigo cha Mbwa mwizi 3-1 na ndugu zao Azam,uzembe uliosababisha beki wao Kelvin Yondan achomoke na kutua Yanga,sakata la Okwi kutoelewekaeleweka amefuzu/hajafuzu Austria na vipi habari za kusema anakaribia kutua Brazil ya Tanzania (Yanga),hesabu za mauzo ya Samatta,Ochan na Mgosi,mapato na matumizi etc.....wallah ninavyowajua Wanachama wa Simba bila usajili huu wa kuwafumba midomo Wana'Simba leo pangechimbika pale bwalo la Maafisa wa polisi Oysterbay.
Bila shaka Viongozi wa Simba wamejua kucheza na akili za Wanachama wao na leo hii asilimia kubwa ya Wanachama wa team hiyo watasahau mambo hayo ya msingi niliyoya'list hapo na watabakia kumimina pongezi kwa Majemedari wao Maha-Rage na Kabur-i kwa kufanikisha usajili wa wachezaji hawa wawili wakiizidi kete Yanga.
Nawatakia kilalaheri wana'Simba katika mkutano mkuu wao wa leo.
Bila shaka Viongozi wa Simba wamejua kucheza na akili za Wanachama wao na leo hii asilimia kubwa ya Wanachama wa team hiyo watasahau mambo hayo ya msingi niliyoya'list hapo na watabakia kumimina pongezi kwa Majemedari wao Maha-Rage na Kabur-i kwa kufanikisha usajili wa wachezaji hawa wawili wakiizidi kete Yanga.
Nawatakia kilalaheri wana'Simba katika mkutano mkuu wao wa leo.