Mkurugenzi wa Lonmin ajiuzulu

Mkurugenzi wa Lonmin ajiuzulu

Sumasuma

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2011
Posts
342
Reaction score
110
120920090723_marikana_workers_144x81_bbc_nocredit.jpg

Mkurugenzi mkuu wa kiwanda cha kuchimba madini ya platinum ya Lonmin amejiuzulu, miezi minne baada ya mgomo wa wafanyakazi katika mgodi wake wa Marikani nchini Afrika Kusini, iliyosababisha vifo vya watu 44.
Ian Farmer hajakuwa ofisini tangu mwezi Agosti baada ya kulazwa hospitalini.
Afisa mkuu anayesimamia masuala ya ya fedha Simon Scott, ataendelea kuhudumu kama kaimu afisa mkuu mtendaji wa kampuni hiyo, hadi mridhi wa Bwana Farmers, atakapoteuliwa.
Mgomo wa Marikani uliongeza shinikizo kwa kampuni hiyo ambayo tayari ilikuwa inakabiliwa na kuongezeka ka gharama za utendaji na kushuka kwa bei ya madini ya Platinum.
Kampuni hiyo ambayo imeorodheshwa kwenye masoko ya hisa ya Johannesburg na London, ililazimika kuomba fedha zaidi dola milioni 817 kutoka kwa wenye hisa wake, ili ilishindwe kulipa madeni yake na kukiuka sheria na masharti ya mikopo.
Tarehe kumi na sita mwezi wa nane mwaka huu wafanyakazi 34 wa kampuni hiyo walipigwa risasi na polisi, tukio ambalo lilitajwa kuwa mbaya zaidi tangu kumalizika kwa utawala wa ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini mwaka wa 1994.
Wengine kumi, wakiwemo maaafisa wawili wa polisi waliaga dunia katika maandamano hayo ya wafanyaakazi wa migodi
 
Back
Top Bottom