Mkurugenzi UDSM computing Centre (UCC )- Dr. Minja ahusishwa kashfa nzito

Mkurugenzi UDSM computing Centre (UCC )- Dr. Minja ahusishwa kashfa nzito

Bila Wachaga nchi itatikisika
Uchagga wa Mkurugenzi Minja umesaidia nini hapo kwa maendeleo ya Taifa. Kama tangu nchi ipate uhuru, ndo kumekuwa na usemi kwamba Wachagga ndo wamejaa Serikali, Je mbona bado ni nchi masikini kabsa (Nchi za ulimwengu wa 3).

Let's not be TRIBALISTS" guys. Masuala ya kabila la mtu siamini km ni chachu ya kuleta maendeleo ya nchi. Kwa sasa ni kum_judge mtu INDIVIDUALLY na sio TRIBE.

We must ask ourselves why we believe in Chagga while they have hold senior job posts in both public services and Civil services but still we are economically limping??
 
Inasemekana kufungwa kwake ni sababu binafsi..na malizote zilizokuwa mbezi beach branch zimeharibika kwa kunyeshewa na mvua plu jua
Kwahiyo na pale City Centre itakuwaje wakati tumeapply juzi juzi tu hapa?
 
Uchagga wa Mkurugenzi Minja umesaidia nini hapo kwa maendeleo ya Taifa. Kama tangu nchi ipate uhuru, ndo kumekuwa na usemi kwamba Wachagga ndo wamejaa Serikali, Je mbona bado ni nchi masikini kabsa (Nchi za ulimwengu wa 3).

Let's not be TRIBALISTS" guys. Masuala ya kabila la mtu siamini km ni chachu ya kuleta maendeleo ya nchi. Kwa sasa ni kum_judge mtu INDIVIDUALLY na sio TRIBE.

We must ask ourselves why we believe in Chagga while they have hold senior job posts in both public services and Civil services but still we are economically limping??
Hafu still haohao ndo wanajiita wapinzani wa ccm au wanataka chance la kuibomoa hii nchi vizuri
 
WACHAGA bwana! Tehe Tehe Tehe!

tatizo la ucc, ukisoma toka magazeti yaanze kuandika , shida kubwa inasemekana ni huyo Mkurugenzi Dr Minja. hiyo nafasi aliyopewa ni kama vile hana uwezo nayo. halafu inaelekea hana mahusiano mazuri na wafanyakazi..naona wanalalamika anawanyanyasa. ngoja tusubiri uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili zitahishije.
 
tatizo la ucc, ukisoma toka magazeti yaanze kuandika , shida kubwa inasemekana ni huyo Mkurugenzi Dr Minja. hiyo nafasi aliyopewa ni kama vile hana uwezo nayo. halafu inaelekea hana mahusiano mazuri na wafanyakazi..naona wanalalamika anawanyanyasa. ngoja tusubiri uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili zitahishije.
Dr. Minja na watu wa aina yake ndio binadamu wanaochangia kudidimia kimaendeleo Taifa hili.
Imefikia wakati tuwekane bayana. Watu wa aina hii ni hatari sana kwa maendeleo ya Taifa. Ubinafsi, Ukabila, Wizi na Chuki ndio misingi ya watu aina ya Dr. Minja.
Awamu hii dawa yao imepatikana na ndio maana tunawaona hata humu JF wakisambaza Chuki za Ukabila.
 
gazeti la RAI la leo nao wameandika pia kuhusu huyo mkurugenzi....inasemekana anawanyanyasa sana wafanyakazi.
Bahati mbaya sana maudhuli ya habari hiyo yako sawa katika magazeti yote mawili. Nimefuatilia kwa undani naleta taarifa toka kwa mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi UCC
 
Dr. Minja na watu wa aina yake ndio binadamu wanaochangia kudidimia kimaendeleo Taifa hili.
Imefikia wakati tuwekane bayana. Watu wa aina hii ni hatari sana kwa maendeleo ya Taifa. Ubinafsi, Ukabila, Wizi na Chuki ndio misingi ya watu aina ya Dr. Minja.
Awamu hii dawa yao imepatikana na ndio maana tunawaona hata humu JF wakisambaza Chuki za Ukabila.
 

Attachments

Someni hiyo kitu, tuache majungu ya watu wachache wanaotetea maslahi binafsi
 
Muandishi amesha pewa hongo " ili achafue watu
 
Dr. Minja na watu wa aina yake ndio binadamu wanaochangia kudidimia kimaendeleo Taifa hili.
Imefikia wakati tuwekane bayana. Watu wa aina hii ni hatari sana kwa maendeleo ya Taifa. Ubinafsi, Ukabila, Wizi na Chuki ndio misingi ya watu aina ya Dr. Minja.
Awamu hii dawa yao imepatikana na ndio maana tunawaona hata humu JF wakisambaza Chuki za Ukabila.

Ndugu yangu hata Magufuli anasemwa kama unavyomsema Minja, lakini nimefanya uchunguzi wa kina tatizo ni watu watatu tu pale ucc mmoja hana cheti cha kidato cha nne, mwingine ni dereva anayelalamika Minja anajiendesha kwa gari binafsi badala ya gari ya ofisi, kwa taarifa zisizotia shaka nilizopata kutoka kwa mtu wa karibu wa huyo dereva ni kwamba anataka awe anasafiri ili apate posho za safari na akimuendesha boss hachoki kama akifanya shughuli za kawaida za ofisi (nimekumbushwa kuwa Minja halipwi mafuta bali ameona ni mojawapo ya mbinu ya kupunguza matumizi yasiyo ya lazima. Wa mwisho ni kiongozi wa THTU ambaye magazeti yamemnukuu, ukipitia barua nilizopata toka kwa watu wake pamoja za UCC utagundua kuna uwalakini mkubwa katika mawasilisho. Pamoja na yote nadhani Ujumbe toka kwa Bodi ya Wakurugenzi inajibu hoja lukuki. Hayo ya ukabila na wizi vyombo ya usalama vihusishwe vifanye kazi yake vyema

Nawsilisha
 
Yani ukisoma humo ndani ni mparanganyo....yani ni kama mtu anatafutiwa tuhuma au makosa...
 
Hafu still haohao ndo wanajiita wapinzani wa ccm au wanataka chance la kuibomoa hii nchi vizuri
Uliona wapi wachagga wakawa wapinzani wa ccm, wapinzani wa ccm ni vyama vya siasa kama cuf, act
 
kwa wiki kadhaa naona magazeti yanaripoti madudu ya mkurugenzi wa UDSM- computing Centre
Hivi ni kwa hawamu hii watendaji wa Serikali bado wanacheza na mali za uma
Inasemekana mali ya mamilion ya walipa kodi zimeharibika huku shule watoto bado wanakaa chini
Uongozi wa chuo kikuu unabidi utolee maelezo juu ya tuhuma hizi nzito kwa taasisi kubwa kama hiyo

Mkurugenzi UCC ahusishwa kashfa nzito


Na Alex Kazenga
Dar es Salaam
Wafanyakazi zaidi ya 30 wa Kituo cha Mafunzo ya Kompyuta (UCC), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wamo hatarini kupoteza kazi baada ya kituo hicho na matawi yake yote nchini kutakiwa kufungwa kwa kile kinachoelezwa kuwa ni mbinu zinazoratibiwa na menejimenti kukiua kituo hicho.
Anayetuhumiwa kufanya mbinu hizo ni Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho, Dk. Ellinami Minja, kwa manufaa binafsi pamoja na baadhi ya watu walio karibu naye.

Uchunguzi uliofanywa na Gazeti la JAMHURI umebaini baadhi ya matawi ya kituo hicho tayari yamefungwa likiwemo Tawi la Mbezi Beach na City Center, yote ya jijini Dar es Salaam.
Pamoja na kufungwa kwa matawi hayo, vitendea kazi vyote vimehamishiwa makao makuu ya kituo hicho (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam) ambako vimetelekezwa na vingine kuharibiwa kwa makusudi.
Kuharibiwa kwa vitendea kazi hivyo ambavyo ni pamoja na kompyuta, viti, viyoyozi (AC), vifaa vya kuzimia moto na meza, ambavyo vimegharimu mamilioni ya shilingi za walipa kodi, inaelezwa kuwa ni mkakati mahususi ulioandaliwa na Dk. Minja ili kuvinufaisha vyuo binafsi vinavyotoa mafunzo ya kompyuta vinavyomilikiwa na baadhi ya walimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Hata hivyo mkakati huo unaofanywa kwa usiri mkubwa tayari unatajwa kuwakosesha masomo ya kompyuta zaidi ya wanafunzi 300 waliokuwa wakisoma katika matawi hayo.
Wakati mkakati huo haramu ukifanyika, athari zake zitawagusa zaidi ya wafanyakazi 30 wakiwemo walimu, wahasibu na watumishi wengine wa kada mbalimbali ambao tayari menejimenti imetishia kuwafuta kazi.

Sababu nyingine ya kufunga matawi hayo ni kile kinachoelezwa kuwa ni agizo la Rais John Magufuli kwamba taasisi zote za umma zisiendeshe shughuli zake katika majengo ya watu binafsi nje ya maeneo yanayomilikiwa na kituo hicho.

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (THTU), Salifius Mligo, ameliambia Gazeti la JAMHURI kwamba ni kweli menejimenti ya kituo hicho inanyanyasa wafanyakazi wake, hasa walio wanachama na kwamba imetoa tangazo la kupunguza wafanyakazi wake.
Uchunguzi wa Gazeti la JAMHURI umebaini kwamba migogoro katika kituo hicho imedumu kwa miaka miwili, migogoro hiyo inachangiwa na uongozi wa Dk. Minja na Makamu wake, Dk. Elias Mturi, ambao wamekuwa wakiendesha kituo hicho jinsi wanavyotaka bila kuzingatia maadili wala sheria.
Mligo anasema kutokana na tangazo hilo la kufukuza wafanyakazi, Chama cha Wafanyakazi chuoni hapo (THTU) kimeandika barua ya kuomba ufafanuzi kwa vielelezo kwanini menejimenti inataka kuwafukuza wafanyakazi.

Ubaguzi unaotajwa kuendelea kushika kasi katika kituo hicho ambapo wanachama wa Chama cha Wafanyakazi (THTU) hubaguliwa na menejimenti, unatokana na Dk. Minja kuhisi kwamba chama hicho kinaingilia masilahi yake, hivyo ili kuepuka kusumbuliwa na chama hicho huwalazimisha wafanyakazi kujitoa kwenye chama ama kuacha kazi.
“UCC ni mali ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambacho ni mali ya serikali, kwa hiyo kwa namna moja au nyingine watumishi wa kituo hiki ni watumishi wa umma, sisi watumishi wa umma tuna miiko na maadili yetu.

Hata hivyo mwenyekiti huyo amehoji kwanini kituo hicho kinasema hakina fedha za kujiendesha wakati jamii ya Watanzania kwa asilimia kubwa ina imani na mafunzo yanayotolewa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na inatamani watoto wao kupata mafunzo katika kituo hicho.
Mligo anasema sababu za kukosa wanafunzi wanaojiunga na mafunzo ya kompyuta katika kituo hicho ni za uongo, kwani jina na sifa za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam vinakibeba kituo hicho.
Anasema kama menejimenti imeshindwa kuendesha kituo hicho kulingana na mahitaji ya soko yaliyopo kwa sasa viongozi wanatakiwa kujiuzulu ili wengine wenye ujuzi wakiongoze kituo hicho kuliko kuwasumbua wafanyakazi.

“Dk. Minja amekuwa na tabia ya kuwafukuza wafanyakazi anavyotaka yeye, sisi tukimuuliza anaona kama tunamnyima uhuru.
Hata hivyo Dk. Minja anatuhumiwa kuwabagua wanawake katika kituo hicho, imebainika kuwa wapo walionyimwa fursa za kwenda masomoni na wengine kunyimwa haki ya kupanda vyeo kwa sababu anazozijua yeye mwenyewe.

“Yupo aliyeomba kwenda masomoni akamruhusu kwa kumpa dhamana ya barua, lakini ulipofika muda wa kwenda alimnyima kibali, hata alipoomba kupewa likizo bila malipo ili aweze kwenda masomoni napo pia alikataa kwamba hana vigezo,” anasema Mligo.
JAMHURI limemtafuta Dk. Minja kwa ajili ya kutoa ufafanuzi wa tuhuma zinazomhusu, hata hivyo alitoa maelekezo kwamba apatiwe barua yenye maswali na kutumiwa kwa njia ya barua pepe (e-mail) na kwa mkono, huku ikiwa imesainiwa.

Maelekezo hayo yalifuatwa, Gazeti la JAMHURI liliandika barua na kuifikisha ofisini kwake Agosti 27, lakini cha kushangaza tangu barua hiyo ifike ofisini kwake ushirikiano ulipungua, kwani hakusema ni lini anaweza kukutana na mwandishi wa Gazeti la JAMHURI ili kutoa ufafanuzi wa tuhuma hizo.
JAMHURI limefika Ofisi ya Makamu Mkuu wa Chuo cha Dar es Salaam, Prof. William Anangisye, kwa lengo la kupata ufafanuzi wa tuhuma hizo, ambaye ameelekeza ofisi ya mawasiliano ya chuo hicho itoe ufafanuzi kwa niaba yake.

Ofisa Habari wa chuo hicho, Jackson Isdory, ameliambia Gazeti la JAMHURI kwamba tuhuma hizo zimefika kwenye uongozi wa chuo na kwamba imeundwa tume kwa ajili ya kufanya uchunguzi, huku akiahidi kwamba baada ya uchunguzi dhidi ya tuhuma za UCC na Dk. Minja kukamilika uongozi wa chuo utatoa taarifa kwa umma.

CHANZO: GAZETI LA JAMHURIView attachment 872345
Kuna walimu wawili hapo UCC na majina yao yamefanana. Mmoja anaitwa Mtui na mwingine Mturi. Hawa watu wana knowlegde kali kwenye mambo ya Programming (hasa kwenye UNIX). Yaani knowledge yao huwa naitamani kama ningekuwa nayo mimi, wakati huu ningekuwa niko NASA au APPLE. Yaani ni wabaya hakuna mfano. Mungu awabariki!
 
Uchagga wa Mkurugenzi Minja umesaidia nini hapo kwa maendeleo ya Taifa. Kama tangu nchi ipate uhuru, ndo kumekuwa na usemi kwamba Wachagga ndo wamejaa Serikali, Je mbona bado ni nchi masikini kabsa (Nchi za ulimwengu wa 3).

Let's not be TRIBALISTS" guys. Masuala ya kabila la mtu siamini km ni chachu ya kuleta maendeleo ya nchi. Kwa sasa ni kum_judge mtu INDIVIDUALLY na sio TRIBE.

We must ask ourselves why we believe in Chagga while they have hold senior job posts in both public services and Civil services but still we are economically limping??
Nenda popote tz ukimkosa mchaga usikae hilo eneo halifai kabisa !!!vilevile ukiona mtu anawatenga hawa jamaa subiria anguko lake linanukia ,,Kama tunapoelekea sasa huna haja ya kutoa povu subiri tu utaona Muda ni mwalimu mzuri!!! They are blessed but poorers and stupids hate them
 
Nenda dunia hii yote ukimkosa mchaga ondoka japafai kushi
 
Mchaga kwa tz ukimlaani umefungiwa duniani ni sawa na Mimi ninyooshe mkono kwa mwisrael
 
Back
Top Bottom