kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
MKURUGENZI Mtendaji (DED) wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro, Ephrem Kalimalwendo, ametangaza kumburuza mahakamani mkuu wa wilaya hiyo, Halima Dendego kwa madai kuwa, amemzulia tuhuma za uongo za kununua Power Tillers zenye thamani ya Sh milioni 225 ambazo hazina ubora.
Kalimalwendo amempa siku 21 DC huyo kutoa vielelezo vya namna alivyohusika kwenye ununuzi wa power tillers hizo na iwapo atashindwa kufanya hivyo, atalazimika kujisafisha kwa kutumia vyombo vya sheria.
Amesema, atafanya hivyo kwa kuwa taarifa hizo ni nzito na zimemwaibisha na kumvunjia heshima mbele ya umma wa Watanzania hadi nje ya nchi.
Dendego alipotafutwa kwa simu yake ya mkononi ili kutoa ufafanuzi juu ya tuhuma alizozitoa dhidi ya DED wake, ilikuwa imefungwa muda wote.
Akifafanua juu ya tuhuma hizo, Kalimalwendo alisema Aprili 13, mwaka huu DC Dendego alitoa tuhuma za yeye (DED) kwa kushirikiana na watumishi wengine waliingia mkataba wa kununua power tillers 50 kutoka kwa Kampuni ya Millystel Distributors ya Dar es Salaam kwa bei ya Sh milioni 4.5 kila moja.
Anadaiwa kusema kuwa power tillers zilizonunuliwa hazina ubora, zinafifia rangi na baadhi ya vifaa havikuwepo, kitendo kilicholeta kasoro katika vifaa hivyo na kuisababishia hasara Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa.
Kwa kauli yake, Dendego aliagiza mimi na watumishi wengine tukamatwe na kufunguliwa kesi ya wizi na taarifa hizi zilitangazwa na vyombo vya habari, alisema Kalimalwendo.
Amesema, alipokea taarifa hizo kwa masikitiko kwa sababu hahusiki na chochote katika ununuzi wa power tillers hizo. Alikiri halmashauri hiyo kuingia mkataba na kampuni hiyo wa ununuzi wa matrekta hayo 50.
Alisema Kampuni ya Millystel Distributors ilishinda zabuni kihalali kwa vigezo vyote vilivyopo kwenye Sheria ya Manunuzi ya Mwaka 2004 na kanuni zake ilizingatiwa.
Hata hivyo, alisema kwa kuzingatia masharti ya mkataba, halmashauri yake ililazimika kuvunja mikataba yote miwili na yeye Kalimalwendo kwa nafasi yake kama DED, alilazimika kutekeleza hilo kwa barua ili kutoa fursa ya kupata mzabuni mwingine.
Alisema kuanzia Novemba 3, 2010 alilazimika kuwa nje ya ofisi na alifanya makabidhiano yote kama inavyotakiwa. Licha ya kuwa hakueleza alikoenda, lakini DED huyo alienda kugombea ubunge katika majimbo ya Mkoa wa Rukwa.
Alisema akiwa ameondoka ofisini, nyuma yake kwa taarifa alizozipata Kampuni ya Millystel Distributors ilipeleka matrekta hayo.
Utaratibu uliotumika siujui kwani mimi niliishia hatua ya kuvunja mkataba na kukabidhi ofisi, alieleza.
Hivyo alisema anashindwa kuelewa namna alivyohusishwa na mchakato wa ununuzi wa matrekta hayo na kwa nini DC amwite mwizi na kumtangaza kwenye vyombo vya habari wakati hakuhusika na ununuzi huo.
Kalimalwendo amempa siku 21 DC huyo kutoa vielelezo vya namna alivyohusika kwenye ununuzi wa power tillers hizo na iwapo atashindwa kufanya hivyo, atalazimika kujisafisha kwa kutumia vyombo vya sheria.
Amesema, atafanya hivyo kwa kuwa taarifa hizo ni nzito na zimemwaibisha na kumvunjia heshima mbele ya umma wa Watanzania hadi nje ya nchi.
Dendego alipotafutwa kwa simu yake ya mkononi ili kutoa ufafanuzi juu ya tuhuma alizozitoa dhidi ya DED wake, ilikuwa imefungwa muda wote.
Akifafanua juu ya tuhuma hizo, Kalimalwendo alisema Aprili 13, mwaka huu DC Dendego alitoa tuhuma za yeye (DED) kwa kushirikiana na watumishi wengine waliingia mkataba wa kununua power tillers 50 kutoka kwa Kampuni ya Millystel Distributors ya Dar es Salaam kwa bei ya Sh milioni 4.5 kila moja.
Anadaiwa kusema kuwa power tillers zilizonunuliwa hazina ubora, zinafifia rangi na baadhi ya vifaa havikuwepo, kitendo kilicholeta kasoro katika vifaa hivyo na kuisababishia hasara Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa.
Kwa kauli yake, Dendego aliagiza mimi na watumishi wengine tukamatwe na kufunguliwa kesi ya wizi na taarifa hizi zilitangazwa na vyombo vya habari, alisema Kalimalwendo.
Amesema, alipokea taarifa hizo kwa masikitiko kwa sababu hahusiki na chochote katika ununuzi wa power tillers hizo. Alikiri halmashauri hiyo kuingia mkataba na kampuni hiyo wa ununuzi wa matrekta hayo 50.
Alisema Kampuni ya Millystel Distributors ilishinda zabuni kihalali kwa vigezo vyote vilivyopo kwenye Sheria ya Manunuzi ya Mwaka 2004 na kanuni zake ilizingatiwa.
Hata hivyo, alisema kwa kuzingatia masharti ya mkataba, halmashauri yake ililazimika kuvunja mikataba yote miwili na yeye Kalimalwendo kwa nafasi yake kama DED, alilazimika kutekeleza hilo kwa barua ili kutoa fursa ya kupata mzabuni mwingine.
Alisema kuanzia Novemba 3, 2010 alilazimika kuwa nje ya ofisi na alifanya makabidhiano yote kama inavyotakiwa. Licha ya kuwa hakueleza alikoenda, lakini DED huyo alienda kugombea ubunge katika majimbo ya Mkoa wa Rukwa.
Alisema akiwa ameondoka ofisini, nyuma yake kwa taarifa alizozipata Kampuni ya Millystel Distributors ilipeleka matrekta hayo.
Utaratibu uliotumika siujui kwani mimi niliishia hatua ya kuvunja mkataba na kukabidhi ofisi, alieleza.
Hivyo alisema anashindwa kuelewa namna alivyohusishwa na mchakato wa ununuzi wa matrekta hayo na kwa nini DC amwite mwizi na kumtangaza kwenye vyombo vya habari wakati hakuhusika na ununuzi huo.