Samson Ernest
JF-Expert Member
- Aug 28, 2014
- 1,118
- 1,565
Yon 2:7 SUV
[7] Roho yangu ilipozimia ndani yangu, Nalimkumbuka BWANA; Maombi yangu yakakuwasilia, Katika hekalu lako takatifu.
Sisemi siku nyingine tukiwa katika raha tusimkumbuke Mungu wetu, ninachomaanisha hapa ni kwamba hata ile siku ya tabu yako kumbukumbu zako zisije zikafikiria kutafuta msaada sehemu nyingine nje na Mungu.
Yona anasema roho yake ilipozimia, alimkumbuka Mungu wake, hii inaonyesha vile tunapaswa kufanya pale tunapokutana na shida/changamoto yeyote ile.
Tunapokutana na mambo magumu, tunapaswa kuelekeza maombi yetu kwa MUNGU, na hupaswi kuzimia moyo wako katika mapito yako.
Usikate tamaa mpaka ukafika mahali ukaona Mungu hana msaada kwako, hata kama unaona kila kitu kimeanguka, mkimbilie Mungu ndiye ana jawabu lako.
Imani yako haipaswi kutoka kwa Mungu, bila kujalisha uzito wa jambo unalopitia au lililokupata, endelea kusimama imara katika BWANA.
Soma neno ukue kiroho
Liwe jua iwe mvua soma biblia na kutafakari
Mungu akubariki sana
[7] Roho yangu ilipozimia ndani yangu, Nalimkumbuka BWANA; Maombi yangu yakakuwasilia, Katika hekalu lako takatifu.
Sisemi siku nyingine tukiwa katika raha tusimkumbuke Mungu wetu, ninachomaanisha hapa ni kwamba hata ile siku ya tabu yako kumbukumbu zako zisije zikafikiria kutafuta msaada sehemu nyingine nje na Mungu.
Yona anasema roho yake ilipozimia, alimkumbuka Mungu wake, hii inaonyesha vile tunapaswa kufanya pale tunapokutana na shida/changamoto yeyote ile.
Tunapokutana na mambo magumu, tunapaswa kuelekeza maombi yetu kwa MUNGU, na hupaswi kuzimia moyo wako katika mapito yako.
Usikate tamaa mpaka ukafika mahali ukaona Mungu hana msaada kwako, hata kama unaona kila kitu kimeanguka, mkimbilie Mungu ndiye ana jawabu lako.
Imani yako haipaswi kutoka kwa Mungu, bila kujalisha uzito wa jambo unalopitia au lililokupata, endelea kusimama imara katika BWANA.
Soma neno ukue kiroho
Liwe jua iwe mvua soma biblia na kutafakari
Mungu akubariki sana