lifeofmshaba
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 867
- 219
25th June 2011
Bpe
Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo
Serikali imesema suala la kuondolewa kwa posho za vikao kwa wabunge linawezekana isipokuwa mchakato ni lazima uanzie katika kamati ya uongozi ya Bunge.
Kauli hiyo ilitolewa juzi jijini Dar es Salaam na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa magari 15 yaliyotolewa na Uingereza kwa ajili zoezi la Sensa ya watu na makazi itakayofanyika mwakani.
Mkulo alisema suala la posho za wabunge limekuwa kubwa na kujikita katika vichwa vya watu katika siku za hivi karibuni na kusema kuwa suluhisho lake ni kamati ya uongozi ya Bunge ambayo kama itaona zinafaa kuondolewa zitaondolewa bila kikwazo chochote.
"Unajua hizi kanuni na taratibu za Bunge zinasimamiwa na kamati ya uongozi ambayo ina jukumu la kuamua kuzibadilisha ama kuziacha zikiwemo hizi za kuwalipa wabunge posho," alisema.
Bpe
Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo
Serikali imesema suala la kuondolewa kwa posho za vikao kwa wabunge linawezekana isipokuwa mchakato ni lazima uanzie katika kamati ya uongozi ya Bunge.
Kauli hiyo ilitolewa juzi jijini Dar es Salaam na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa magari 15 yaliyotolewa na Uingereza kwa ajili zoezi la Sensa ya watu na makazi itakayofanyika mwakani.
Mkulo alisema suala la posho za wabunge limekuwa kubwa na kujikita katika vichwa vya watu katika siku za hivi karibuni na kusema kuwa suluhisho lake ni kamati ya uongozi ya Bunge ambayo kama itaona zinafaa kuondolewa zitaondolewa bila kikwazo chochote.
"Unajua hizi kanuni na taratibu za Bunge zinasimamiwa na kamati ya uongozi ambayo ina jukumu la kuamua kuzibadilisha ama kuziacha zikiwemo hizi za kuwalipa wabunge posho," alisema.
CHANZO: NIPASHE