Mkulima wa zao la mahindi awezeshwe sasa ili Tanzania iweze kuhudumia Africa mashariki na pembe ya Africa badala ya kufikiria kushusha bei

mkaliman

JF-Expert Member
Dec 18, 2014
878
1,108
Kwa habari ya bei ya mahindi kupanda nami nitoe maoni; Kwanza mkulima wa Tanzania ameshateseka sana, wakati wewe na mimi tukiwa mjini tunakula ugali na kusaza.

Tunapiga kelele bei ya mahindi imepanda lakini hatuzungumzii kupanda kwa bei za huduma mbalimbali na bidhaa za kiwandani kama sukari na kadhalika. Pia bei ikishuka ndo tunashangilia kuendelea kumnyonya huyu mkulima!

Hakuna aliyezaliwa mkulima, anayeona bei imepanda sana akalime full stop.

Mimi siyo team kusifia ila penye tija nasema! Big up mh. Rais JP. Magufuli kwa hili.
 
Mkuu majority wanaoumizwa na Bei ya mahindi NI hao unaofikiri unawatetea ,kimsingi Tanzania kwa Sasa Kuna Uhaba wa chakula.
Dalili zake NI kupanda kws mahindi...wanaonufaiks NI wafanya Biashara na wakulima wachsche mno.

Hizi ni Siasa za Korosho
 
Mkuu majority wanaoumizwa na Bei ya mahindi NI hao unaofikiri unawatetea ,kimsingi Tanzania kwa Sasa Kuna Uhaba wa chakula.
Dalili zake NI kupanda kws mahindi...wanaonufaiks NI wafanya Biashara na wakulima wachsche mno.

Hizi ni Siasa za Korosho
Tunataka boost kwenye uzalishaji, acha tuone kama demand inaweza kuboost uzalishaji, maeneo mengi ya umwagiliaji yanafaa sana kwa mahindi kwa kuwa hayashambuliwi sana na magojwa ukilinganisha na mbogamboga lakini watu wanalazimisha mbogamboga kwa sababu ya bei chini ya mahindi, Tz tunatakiwa tuzalishe mahindi × 2 ya sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…