Mkulima wa Tanzania, August 2011

LENGEJU BOB

Member
Nov 1, 2010
53
29




Aliandaa shamba kwa panga, fyekeo na jembe la mkono, akapanda bila mbolea kwakuwa viongozi wa serikali ya kijiji na mawakala wa pembejeo walichakachua mbolea ya ruzuku. Mvua haikunyesha pamoja na maombi ya mkesha msikitini na makanisani, mazao kidogo yaliyochomoza yalishambuliwa na magonjwa na wadudu. Kipande cha robo eka alichopanda nyanya kimemzalishia tenga noja la nyanya (kama kilo 80 hivi) kwa mchumo wa kwanza. Bei ya soko ni Tsh. 6,000 kwa tenga, 500 atampa kijana aliyemsaidia kuchuma nyanya na 500 atamlipa kijana aliyemsaidia kubeba tenga la nyanya mpaka sokoni.
Kufika sokoni, kabla ya kuuza atadaiwa Tsh 1000 ya ushuru, (analazimika kukopa kwa jirani) na baada ya kuuza na kulipia deni la ushuru anabakiwa na 4000. Anaskia kiu, njaa na uchovu, lakini anatakiwa kutembea km 10 kutoka sokoni kurudi nyumbani, akiwa n ash. 4,000 mkononi. Mkewe nyumbani amejaa taraja,anajua baba ametoka kuuza mazao, ameandaa orodha ya mahitaji nyumbani

1. Mahitahi ya lazima ya nyumbani

SUKARI 2,500/KG

CHUMVI 1,000/KG

MAFUTA YA TAA 2,100/LITA

MAFUTA YA KUPIKIA 400/ROBO

JUMLA 6,000



2. Mahitaji ya watoto shuleni (vinginevyo mtoto atafukuzwa shule

DATFARI 1,000

MCHANGO WA JENGO 1,000

MADAWATI 1,000

MITIHANI 1,000

JUMLA 4,000



3. Michango ya kijisi (vinginevyo atasombwa na mgambo na kulazwa ofisi za Kijiji)


ULINZI SHIRIKISHI 1,000

ZAHANATI 1,000

JUMLA 2,000


JUMLA KUU 1+2+3 = 12,000 (-4000) = 8,000 DENI!

MARA mkulima anakumbuka robo nyingine ya ekari aliyolima mahindi, na anapata taarifa kuwa mjini mahindi yana bei nzuri kidogo, haraka anaenda shamba, kwa kazi ya siku nzima anafanikiwa kuvuna gunia tano! Anaweka tatu ghalani kwa ajili ya chakula, anafikiria kuuza mbili kupata pesa za kujikimu. Anakodi mkokoteni, kichwani anawaza ukombozi, anajua akiuza mahidi atapata pesa kidogo ya sukari, chumvi, michango ya shule na kijiji…………….


GHAFLA anakutana na kizuizi njiani “NI MARUFUKU KUUZA MAZAO YA CHAKULA” Mgambo wanamuamuru arudi na mkokoteni wake haraka kabla hawajataifisha na mahindi yake!.. Amechanganyikiwa, anapoteza uwezo wa kuona, kufikiri na hata kusikia, kwa mbaaaali anasikia tangazo la wizara ya afya, likihimiza watu wale mayai, kuku, nyama….Tangazo linasisitiza kuwa watanzania ni wavivu wa kula nyama na maziwa……..sauti hizo zinachanganyika na kile kibwagizo alichokisikia miaka ile ya uchaguzi………Maisha bora kwa kila Mtanzania………

Machozi yanasombwa na Jasho!



TAFAKARI, AMUA CHUKUA HATUA……………………….
 
Mkuu maneno yako ni msumari juu ya mbao, asee Dagama unawapeleka wapi watanzania?
 
Aliandaa shamba kwa panga, fyekeo na jembe la mkono, akapanda bila mbolea kwakuwa viongozi wa serikali ya kijiji na mawakala wa pembejeo walichakachua mbolea ya ruzuku. Mvua haikunyesha pamoja na maombi ya mkesha msikitini na makanisani, mazao kidogo yaliyochomoza yalishambuliwa na magonjwa na wadudu. Kipande cha robo eka alichopanda nyanya kimemzalishia tenga noja la nyanya (kama kilo 80 hivi) kwa mchumo wa kwanza. Bei ya soko ni Tsh. 6,000 kwa tenga, 500 atampa kijana aliyemsaidia kuchuma nyanya na 500 atamlipa kijana aliyemsaidia kubeba tenga la nyanya mpaka sokoni.
Kufika sokoni, kabla ya kuuza atadaiwa Tsh 1000 ya ushuru, (analazimika kukopa kwa jirani) na baada ya kuuza na kulipia deni la ushuru anabakiwa na 4000. Anaskia kiu, njaa na uchovu, lakini anatakiwa kutembea km 10 kutoka sokoni kurudi nyumbani, akiwa n ash. 4,000 mkononi. Mkewe nyumbani amejaa taraja,anajua baba ametoka kuuza mazao, ameandaa orodha ya mahitaji nyumbani

1. Mahitahi ya lazima ya nyumbani

SUKARI 2,500/KG

CHUMVI 1,000/KG

MAFUTA YA TAA 2,100/LITA

MAFUTA YA KUPIKIA 400/ROBO

JUMLA 6,000



2. Mahitaji ya watoto shuleni (vinginevyo mtoto atafukuzwa shule

DATFARI 1,000

MCHANGO WA JENGO 1,000

MADAWATI 1,000

MITIHANI 1,000

JUMLA 4,000



3. Michango ya kijisi (vinginevyo atasombwa na mgambo na kulazwa ofisi za Kijiji)


ULINZI SHIRIKISHI 1,000

ZAHANATI 1,000

JUMLA 2,000


JUMLA KUU 1+2+3 = 12,000 (-4000) = 8,000 DENI!

MARA mkulima anakumbuka robo nyingine ya ekari aliyolima mahindi, na anapata taarifa kuwa mjini mahindi yana bei nzuri kidogo, haraka anaenda shamba, kwa kazi ya siku nzima anafanikiwa kuvuna gunia tano! Anaweka tatu ghalani kwa ajili ya chakula, anafikiria kuuza mbili kupata pesa za kujikimu. Anakodi mkokoteni, kichwani anawaza ukombozi, anajua akiuza mahidi atapata pesa kidogo ya sukari, chumvi, michango ya shule na kijiji…………….


GHAFLA anakutana na kizuizi njiani “NI MARUFUKU KUUZA MAZAO YA CHAKULA” Mgambo wanamuamuru arudi na mkokoteni wake haraka kabla hawajataifisha na mahindi yake!.. Amechanganyikiwa, anapoteza uwezo wa kuona, kufikiri na hata kusikia, kwa mbaaaali anasikia tangazo la wizara ya afya, likihimiza watu wale mayai, kuku, nyama….Tangazo linasisitiza kuwa watanzania ni wavivu wa kula nyama na maziwa……..sauti hizo zinachanganyika na kile kibwagizo alichokisikia miaka ile ya uchaguzi………Maisha bora kwa kila Mtanzania………

Machozi yanasombwa na Jasho!



TAFAKARI, AMUA CHUKUA HATUA……………………….


eti ni wavivu wa kula nyama na maziwa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Wanazo hizo hela za kununulia nyama na maziwa?
 
Back
Top Bottom