Mkulima Tanzania Anaonewa

Lawkeys

JF-Expert Member
Nov 16, 2009
1,118
287
Hivi karibuni nimesikia jitihada za serikali kuzuia uuzaji wa mazao ya chakula nje ya nchi. Sina shaka kwamba hatua hizo ni kinyume cha kanuni za biashara huria, na pia kwamba zina madhara ya moja kwa moja kwa mkulima kwani itamlazimu kuuza mazao kwa bei ya chini. Hakuna asiyejua jinsi sekta ya kilimo ilivyosahaulika. Wengi mashahidi, mlisha nchi mpaka kesho anatumia jembe la mkono, jua kali. Serikali makini ingesoma inadvance demand ya chakula na kuwawezesha watanzania kuzalisha ziada na wao kunufaika na kazi yao na sio kukaa chini kujadili jinsi ya kudhibiti soko la chakula.

Mimi naona hapa mkulima hatendewi haki.
 
Hayo uliyoyasema ni ukweli na ukweli mtupu. Katika zama hizi mkulima Tanzania hana chake; ukichunguza vizuri bajeti iliyopitishwa hivi majuzi haitoi unafuu wowote kwa mkulima mdogo isipokuwa imezidi kumgandamiza kwa kurejesha kodi nyingi zinazomwandama moja kwa moja na ambazo huko nyuma zilionekana hazina ufanisi. Aidha bajeti hiyo imeongeza bei ya bidhaa muimu anavyotegemea katika kuendesha maisha yake, kwa mfano mafuta ya taa. Mbali na hayo mkulimo hivi sasa hana sauti yeyote, vyama vya ushirika ambavyo ndivyo vinategemewa kuwa msemaji mkuu wa mkulima vimewekwa mfukoni na serikali, kwakuwa sheria ya ushirika inayotumika hivi sasa imempa madaraka mrajisi wa vyama vya ushirika kuamua ni nani anafaa kuwa kiongozi kwenye vyama hivyo.
 
Back
Top Bottom