Mkopo ngazi ya Diploma 2018/2019

Mkopo ngazi ya Diploma 2018/2019

Kalemataka

Member
Joined
Aug 19, 2017
Posts
48
Reaction score
10
Wale Wote wanaotarajia kuomba mkopo ili kupata ufathili wa masomo katika ngazi ya diploma uzi huu ni special Kwa ajili yako . Uliza swali ujibiwe
 
Kuna dogo Anataka kusoma diploma ya clinical medicine
 
Weka link ya bodi ilikupata huo mkopo kwa watu wa diploma
 
huo mkopo kwa coz zipi na ufaulu upi
 
ngoja mm nianze jifua kuutafuta huo mkopo maana walisema Kwa diploma ndo wana set kombora zao zikiwa tayari watazidropisha
 
hisije kuwa ndo njia ya serikali kukusanya kodi alafu mkopo wa kakosa
 
USITISHA MIKOPO KWA WANAFUNZI WA STASHAHADA (DIPLOMA)
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inapenda kuutaarifu umma kuwa imesitisha mpango wa kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaosoma stashahada (Diploma) kuanzia mwaka wa masomo 2018/2019 kama ilivyotangaza awali.

Itakumbukwa kuwa tarehe 10 Mei mwaka huu, HESLB ilitoa mwongozo unaosimamia utoaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2018/2019. Mwongozo huo, pamoja na mambo mengine, unaeleza kuwa HESLB itaanza kutoa mikopo kwa wanafunzi wa stashahada na kuwa mwongozo kuhusu utaratibu wa kuomba mikopo hiyo ya wanafunzi wa stashahada ungetolewa baadae.

Hatua hii imechukuliwa ili kuhakikisha kuwa kiasi chote cha TZS 427.5 bilioni zilizotengwa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi kwa mwaka 2018/2019 zinaelekezwa kwa wanafunzi wenye mikopo hivi sasa na waombaji wapya wahitaji ambao wana sifa za kujiunga na kozi za shahada tu ambao ndiyo walengwa wakuu.

Hivyo basi, tunatoa wito kwa wanafuzi wote wenye sifa za kujiunga na masomo ya shahada katika taasisi za elimu ya juu na ambao ni wahitaji wa mikopo kuhakikisha wanasoma kwa makini mwongozo wa utoaji mikopo na kuuzingatia.

Kwa takwimu za mwaka 2017/2018, takribani maombi 10,027 ya mikopo yaliyowasilishwa Bodi ya Mikopo yalikuwa na upungufu kama vile kutosainiwa, kutokuwa na viambatanisho sahihi n.k.

HESLB ilianzishwa kwa mujibu wa sheria mwaka 2004 na kuanza kazi rasmi mwezi Julai, 2005 ili kutoa mikopo kwa wanafunzi wahitaji na pia kukusanya mikopo iliyoiva kutoka kwa wanufaika.



Imetolewa na:

Abdul-Razaq Badru
Mkurugenzi Mtendaji
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
DAR ES SALAAM
Jumapili, Juni 3, 2018
 
Back
Top Bottom