Dr Adam Francis
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 464
- 687
Katika siasa, kaulimbiu na propaganda ndizo karata zinazounogesha mchezo wa uchaguzi. Kila mshindani wako anapochanga karata zake, timu yako lazime ichange karata zako. Hiki ndicho kilichotokea kuelekea October 2025.
Wakati CHADEMA wanaendelea na campaign ya No reform no election, CCM wamekuja na ilani ya uchaguzi inayoahidi katiba mpya ambayo kimsingi ndio reforms zinazodaiwa. Kwa lugha rahisi hili ni tamko thabiti kuwa, MKITAKA REFORMS, MKAPIGE KURA.
Sasa mpira upo kwa wapiga kura, kuhusu njia gani waitumie kupata reforms, kwa kushiriki uchaguzi kama wanavyohimizwa na CCM? Au kwa kuzuia uchaguzi kama wanavyohimizwa na CHADEMA. Nachelea kusema kama mnayo nia thabiti ya kuleta mabadiliko ya katiba, basi njia rahisi kati ya hizi ni kuchagua CCM.
Kwa faida ya wasomaji, Misingi na Malengo Kuu ya Ilani 2025-2030 ni kama ifuatavyo:
1. Kuendeleza Uchumi wa Viwanda na Biashara Ndogo (TEHAMA)
Kuimarisha mazingira ya biashara na kukuza uwezo wa viwanda vya ndani, pamoja na kuwawezesha wafanyabiashara wa TEHAMA kupitia mikakati ya kifedha na kiutawala.
2. Uboreshaji wa Huduma za Kijamii Vijijini
Kupanua upatikanaji wa maji safi, huduma za afya, elimu bora, na nishati kwenye maeneo ya vijijini kwa kuzingatia ufanisi na uendelevu.
3. Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi.
Kupanda miti milioni 100 kila mwaka ili kudumisha misitu, kudumisha mazingira, na kuongeza mvua .
4. Kuimarisha Diplomasia ya Kiuchumi na Usalama wa Taifa
Kukuza ushirikiano wa kimataifa, kulinda rasilimali za taifa (gesi, madini, misitu), na kuimarisha usalama wa ndani na nje.
5. Katiba Mpya ya Muungano
Kwa mara ya kwanza, Ilani ya CCM imeipa kipaumbele kuongoza mchakato wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano ndani ya miaka mitano ijayo, ikilenga kujibu mahitaji ya kisasa kijamii, kiuchumi, na kisiasa
Wakati CHADEMA wanaendelea na campaign ya No reform no election, CCM wamekuja na ilani ya uchaguzi inayoahidi katiba mpya ambayo kimsingi ndio reforms zinazodaiwa. Kwa lugha rahisi hili ni tamko thabiti kuwa, MKITAKA REFORMS, MKAPIGE KURA.
Sasa mpira upo kwa wapiga kura, kuhusu njia gani waitumie kupata reforms, kwa kushiriki uchaguzi kama wanavyohimizwa na CCM? Au kwa kuzuia uchaguzi kama wanavyohimizwa na CHADEMA. Nachelea kusema kama mnayo nia thabiti ya kuleta mabadiliko ya katiba, basi njia rahisi kati ya hizi ni kuchagua CCM.
Kwa faida ya wasomaji, Misingi na Malengo Kuu ya Ilani 2025-2030 ni kama ifuatavyo:
1. Kuendeleza Uchumi wa Viwanda na Biashara Ndogo (TEHAMA)
Kuimarisha mazingira ya biashara na kukuza uwezo wa viwanda vya ndani, pamoja na kuwawezesha wafanyabiashara wa TEHAMA kupitia mikakati ya kifedha na kiutawala.
2. Uboreshaji wa Huduma za Kijamii Vijijini
Kupanua upatikanaji wa maji safi, huduma za afya, elimu bora, na nishati kwenye maeneo ya vijijini kwa kuzingatia ufanisi na uendelevu.
3. Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi.
Kupanda miti milioni 100 kila mwaka ili kudumisha misitu, kudumisha mazingira, na kuongeza mvua .
4. Kuimarisha Diplomasia ya Kiuchumi na Usalama wa Taifa
Kukuza ushirikiano wa kimataifa, kulinda rasilimali za taifa (gesi, madini, misitu), na kuimarisha usalama wa ndani na nje.
5. Katiba Mpya ya Muungano
Kwa mara ya kwanza, Ilani ya CCM imeipa kipaumbele kuongoza mchakato wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano ndani ya miaka mitano ijayo, ikilenga kujibu mahitaji ya kisasa kijamii, kiuchumi, na kisiasa