PreGE2025 Mkitaka reforms mkapige kura

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Dr Adam Francis

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2011
Posts
464
Reaction score
687
Katika siasa, kaulimbiu na propaganda ndizo karata zinazounogesha mchezo wa uchaguzi. Kila mshindani wako anapochanga karata zake, timu yako lazime ichange karata zako. Hiki ndicho kilichotokea kuelekea October 2025.

Wakati CHADEMA wanaendelea na campaign ya No reform no election, CCM wamekuja na ilani ya uchaguzi inayoahidi katiba mpya ambayo kimsingi ndio reforms zinazodaiwa. Kwa lugha rahisi hili ni tamko thabiti kuwa, MKITAKA REFORMS, MKAPIGE KURA.

Sasa mpira upo kwa wapiga kura, kuhusu njia gani waitumie kupata reforms, kwa kushiriki uchaguzi kama wanavyohimizwa na CCM? Au kwa kuzuia uchaguzi kama wanavyohimizwa na CHADEMA. Nachelea kusema kama mnayo nia thabiti ya kuleta mabadiliko ya katiba, basi njia rahisi kati ya hizi ni kuchagua CCM.

Kwa faida ya wasomaji, Misingi na Malengo Kuu ya Ilani 2025-2030 ni kama ifuatavyo:
1. Kuendeleza Uchumi wa Viwanda na Biashara Ndogo (TEHAMA)
Kuimarisha mazingira ya biashara na kukuza uwezo wa viwanda vya ndani, pamoja na kuwawezesha wafanyabiashara wa TEHAMA kupitia mikakati ya kifedha na kiutawala.

2. Uboreshaji wa Huduma za Kijamii Vijijini
Kupanua upatikanaji wa maji safi, huduma za afya, elimu bora, na nishati kwenye maeneo ya vijijini kwa kuzingatia ufanisi na uendelevu.

3. Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi.
Kupanda miti milioni 100 kila mwaka ili kudumisha misitu, kudumisha mazingira, na kuongeza mvua .

4. Kuimarisha Diplomasia ya Kiuchumi na Usalama wa Taifa
Kukuza ushirikiano wa kimataifa, kulinda rasilimali za taifa (gesi, madini, misitu), na kuimarisha usalama wa ndani na nje.

5. Katiba Mpya ya Muungano
Kwa mara ya kwanza, Ilani ya CCM imeipa kipaumbele kuongoza mchakato wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano ndani ya miaka mitano ijayo, ikilenga kujibu mahitaji ya kisasa kijamii, kiuchumi, na kisiasa
 
Kuna mjinga mmoja wa CCM miaka ya nyuma alishawahi kusema kama wewe ni mpinzani na unategemea hayo makaratasi ya kura yaweze kuleta mabadiliko katika nchi hii utasubiri sana hadi Yesu arudi.

Ni kweli jamaa alikuwa sahihi 100%

Njia pekee ni moja tu - No Redorms No Elecrion.
 
Akili za ng'ombe ni za ng'ombe tu,hv mwaka jana nchi ilikuwa kwenye nn sio kwenye uchaguzi? nn kilitokea ww mwenye mtindio wa ubongo,naona kama vile umeweka kichwa pembeni umegeuza mnduku wako ndio unautumia kufikiri.Mm nakwambia NO REFORMS NO ELECTION ni muhimu hata kwako na kizazi chako ambacho naamini ipo siku kitakulaumu na kusikitika kwa ugonjwa ulioupata unaosababisha ww kunatumia mnduku kufikiri NO REFORMS NO ELECTION itakusaidia ili siku Moja Ukatibiwe India baada ya kuathirika na ugongwa unaoitwa CCM.Wenye Masters wanaambiwa hawajui kusoma kwenye uchaguzi ila wanaotumia minduku ndio wanajua kusoma ila CCM ni janga kamili kabisa kwa Taifa.
 
Kwa usimamizi upi

Expecting results from what you know
 
Ahadi ya katiba mpya ndio imekukera hivi? Kwani kwenye No reforms No election unadai nini?
 
Huyu hafai kunasibishwa na CCM. Mm nakubaliana na ww, watu wenye mawazo kama hayo ni wajinga. CCM inaamini katika demokrasia ya ushindani ya vyama vingi vya siasa. Sasa kama kuna mroho wa madaraka anatoa matamko ambayo hayapo kwenye misaafu ya CCM huyo amepotoka.
 
Hayo manadiliko yafanyike kwanza ndo uchaguzi ufanyike, msitufanye watanzania wajinga sana. Reforms kwanza ndo tuende kwenye uchaguzi. Hatuwezi kwenda kwenye mechi ambayo watu wameshajitangazia ushidi kwa sababu marefa na washika vibendera wote ni watu wao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…