Msulibasi
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 5,957
- 8,005
Tukiwa tuna kumbukumbu ya chaguzi serekali za mitaa na tukiwa tuaelekea katika uchaguzi mkuu urais wabunge na madiwani tujikumbushe baadhi ya kauli za viongozi wa serekali katika mikutano mbalimbali iwe ya kisiasa ama ya kijamii.
Kauli hii ni ile ya kwamba mukichagua wapinzani amani itatoweka ,tutakuwa kama Rwanda .Somalia na nchi nyingine zilizowahi kuwa na vita.Kauli hii ilikuwa na nguvu sana katika chaguzi za mwaka 1995,2000 na 2005 na dakika za mwisho za uchaguzi 2015.
Hoja hapa ni kwa kiwango gani ni halali kutamka hivyo katika kampeni na mikutano,ya pili hii kauli ina maanisha nani ataanzisha vita?Ukichagua wapinzani CCM itaanzisha fujo ? Inawezekanaje mtu achaguliwe kisha aanzishe vita ?.Hoja ya tatu ni namna gani wapinzani wameweza kuipangua hii hoja maana ndio hoja kuu ya kuwamaliza,Ama nisadiki kuwa wapinzani wataleta shida?
Nasubiri miezi haipiti miwili kauli hii tutaisikia kwa wakuu wa wilaya,wakuu wa mkoa ,mawaziri, wabunge hata wanahabari.Lisemwalo lipo?
Kauli hii ni ile ya kwamba mukichagua wapinzani amani itatoweka ,tutakuwa kama Rwanda .Somalia na nchi nyingine zilizowahi kuwa na vita.Kauli hii ilikuwa na nguvu sana katika chaguzi za mwaka 1995,2000 na 2005 na dakika za mwisho za uchaguzi 2015.
Hoja hapa ni kwa kiwango gani ni halali kutamka hivyo katika kampeni na mikutano,ya pili hii kauli ina maanisha nani ataanzisha vita?Ukichagua wapinzani CCM itaanzisha fujo ? Inawezekanaje mtu achaguliwe kisha aanzishe vita ?.Hoja ya tatu ni namna gani wapinzani wameweza kuipangua hii hoja maana ndio hoja kuu ya kuwamaliza,Ama nisadiki kuwa wapinzani wataleta shida?
Nasubiri miezi haipiti miwili kauli hii tutaisikia kwa wakuu wa wilaya,wakuu wa mkoa ,mawaziri, wabunge hata wanahabari.Lisemwalo lipo?