Mke wangu na baba yake wanatumiana picha za uchi!

Linguistic

JF-Expert Member
Mar 16, 2021
3,671
8,237
Niko kwenye ndoa miaka 7 na mke wangu, kila kitu kilikuwa vizuri mpaka wiki mbili zilizopita, mke wangu aliniaga kuwa anaenda safari ya kikazi. Yeye anafanya kwenye kampuni ya Baba yake ambayo inahusika na ujenzi, Baba yake ni mhandisi.

Mara nyingi huwa wanasafiri pamoja na sina wasiwasi kwani nilikuwa naamini ni Baba yake hakuna shida. Lakini safari hii kuna kitu kilibadilika, mke wangu alikuwa hapokei simu, nilishikwa na wasiwasi nilitaka kumpigia Baba yake lakini nikaona haitakuwa poa.

Kwahiyo ni kama nilipiga simu ikakata, kwamaana iliita sekunde moja tu. Nikakaa kimya kwani ilikuwa ni usiku kama saa nne hivi na nilitaka kujua tu kama wamefika au la. Niliendelea kumpigia simu mke wangu ila iliita tu bila kupokea.

Usiku kwenye saa nane hivi simu yangu iliita, kwakuwa nilikuwa bado sijalala vizuri kwani bado nilikuwa na mawazo kwanini mke wangu hapokei simu nikakuta ni Baba mkwe anapiga, ninapokea nikihisi labda ananiambia kitu, lakini alikuwa haongei, ghafla nikasikia sauti ya kama watu wamelewa wanaongea vitu havieleweki.

Baadaye nasikia sauti za miguno ya mapenzi, nilisikiliza kama dakika 5 hivi nikakata nikaona hayanihusu. Asubuhi mke wangu alinipigia na kuniambia alitoka na Baba yake na rafiki zake akasahau simu nyumbani, nikamuuliza walirudi saa nngapi akaniambia kwenye saa kumi alfajiri kwani Baba yake alikunywa sana.

Nilipata shaka kwani usiku wake nilisikia vitu vya ajabu kama alikuwa na Baba yake inamaana ni yeye alikuwa anafanya mapenzi na Baba yake? Nilikaa kimya sikutaka hata kufikiria hicho kitu, lakini aliporudi nilihisi kama kuna mabadiliko, akawa hana furaha, yaani ni kama kuna kitu alikuwa anaficha.

Niliamua kuhack simu yake, kusema kweli natamani nisingefanya hivyo, nilikuta mke wangu wanatumiana picha za uchi na baba yake mzazi, uchi wa mnyama na nyingine ni kama video walichukua wakiwa kitandani uchi. Nilitaka kukaa kimya ila nilishindwa kuvumilia.

Nikaamua kumuuliza mke wangu kwanini wanatumiana picha za namna ile, nikidhani kama atashtuka aliniambia nisamehe tulilewa ndiyo tukajikuta tuko hivi ni Baba alipiga na simu yangu akaniamia nimtumie, hata hakuna kitu.

Anaongea kama vile ni kitu cha kawaida, nilimuuliza kama ana mahusiano na Baba yake akakataa katakata, utakufa na ushamba wako kwani kuna nini Baba kuniona hivyo wakati nikiwa mdogo alikua ananiogesha.

Nikikasirika na kutaka kumpiga tukaishia kusukumana akaondoka mpaka leo hajarudi, ananitumia meseji hawezi kuishi na mimi kwani nina hasira, kama unakasirika kwa vitu vidogo kama hivyo ukijua mengine si utakufa. Alinitumia meseji, ananiambia nimpe talaka yake hahitaji kuishi na mwanaume ambaye si muelewa.

Nimechanganyikiwa sijui nifanye nini? Mke wangu nampenda, tuna watoto wawili, kila kitu kilikuwa vizuri. Natamani kumuacha lakini sina uhakika kama wana mahusaino na Baba yake au la, vipi wanangu wataishije, nimekwama naomba usaidizi wako, kila nikiwaza nahisi kuchanganyikiwa.
.
Wakuu hii ni Copy and Paste Kutoka Sehemu Nyingine
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom