Moana
Senior Member
- Jan 18, 2021
- 103
- 137
Msingi wa tatizo la mke wake uko hapa, yupo/wapo waliowahi kumtamkia maneno mabovu huyu bidada juu ya muonekano wake,
Nakumbuka ilinitokea mimi nikiwa kwenye umri wa balehe mlezi wangu siku moja katika mazungumzo tu akasema mwanangu wewe Ni mrembo ila tu hiyo midomo/lips imezidi unene, kauli ilinitesa sana ile, nikawa nikiongea mbele za watu najiziba midomo yangu, ulipoingia msimu wa smartphones nikawa napiga picha kwa kuachia tabasamu hata pasipo hitajika lkn Siri yake nyuma ya Hilo tabasamu ilikuwa ni kuficha unene wa lips zangu, (japo nilipendezea kutabasamu),, ajabu Sasa watu wengi walikuwa wakisifia lips zangu zilivyo nzuri hata wanafunzi wa kike walikuwa wakinipaka lipstick ili tu nilaze lips katika barua za maboyfriend zao, lakini bado haikunipa confidence ya midomo yangu
Hili tatizo limeisha hivi karibuni tu baada ya mada moja humu kuzungumzia aina ya lips zangu, nikasoma comments za wadau na wote walisifia lips aina hii niliyonayo hapo ndipo nilipoamua kuipuuza kauli ya aunt yangu aliyonitolea zaidi ya miaka 10 iliyopita na hata picha zangu za hivi karibuni nyingi nimepiga pasipo tabasamu nimezipokea na kuzipenda rasmi lips zangu na kwa hakika ninazo lips nene very sexy lips
Hiki ndicho anatakiwa kufanya mtoa mada kwa mkewe sidhani km mkeo Ni mbaya kwa kila pahala, atoe kizuri chake akazanie hapo hapo kumsifia anaweza hata kutafuta mada ama picha akawa anamuonyesha mkewe vile alivyobarikiwa nk, yaweza kuwa miguu, umbo, macho,pua nk
Yeah watu wa karibu kama walikukosoa ulivyoumbwa inakua vigumu kusahau
Mimi mama yangu mzazi aliniambia nina kichwa kidogo nikawa najiona kama abnormal nikawa nikisuka nasuka nywele nyungiii miaka nenda rudi siku moja nikajisemea tu ebu nisuke yebo kama nikichekesha basi huwezi amini rafiki zangu wakanambia manywele hayakupendezi zaidi ya hizi nikaendelea badae nikanyoa kabisa kumbe nipo kichwa normal tu bwana..mama alinitamkia vile cjui alikua anatania lakini nililibeba sana moyoni