Mke wangu anasema hanitaki nifanye nini?

Mke wangu anasema hanitaki nifanye nini?

Godzzo

Member
Joined
Dec 18, 2011
Posts
11
Reaction score
2
Wakuu,

Mke hanitaki nifanyeje?

Tayari tumejaaliwa watoto wawili, ingawa husema kuwa watoto siyo wa kwangu. Hua ananiletea kiburi na jeuri na hata hataki kufanya usafi wa mafazi yangu.

Naombeni ushauri.
 
Godzzo, kitendo cha kutamkiwa kuwa hao watoto sio wako inaonyesha tatizo ni kubwa sana na wew ndio tatizo kuliko hata mkeo. Kama anaweza diriki kutamka hivyo na hapo hapo kukufanyia jeuri na dharau ni moja ya kiashiria kikubwa kuwa yeye ndio kavaa suruali humo ndani.

Ninaposema kuvaa suruali nina maana yawezekana yeye ndio kwa kiasi kikubwa anaendesha maisha humo ndani kwa asilimia kubwa sana hadi kukulea wewe. Suala hili la mke kubeba majukumu kuliko mume in some cases ndio matokeo yake haya. Anajua hata akifanya dharau.. Hata akikutamkia watoto sio wako na kufanya vitimbi vingine vingi huna ubavu wa kuchukua maamuzi yoyote na hata ikitokea uondoke na kumuacha hakuna anachopungukiwa.

Ni muhimu saana akina baba kushika na kubeba familia zao ipasavyo kuweza kuleta a bit of balance ndani ya nyumba na pia kuweza kuwa a bit in control hata kama mwaishi na mkeo kama equal patners.

Kama si hivyo nilivyogusia, ni vema ukaeleza wewe wadhani nini chanzo cha tatizo. All in all pole sana.
 
Last edited by a moderator:
Mie nadhani na naamini "ana-mimba ya mtoto wa tatu"..coz wengi wao wakiwa -wajawazito huwa wanamabadiliko ya mifumo ya hormones/vichocheo mwilini...tena atazaa mtoto wa kiume.

ushauri;-

usimpige wala usimfanye kitu...mchukuwe mpeleke hospital kampime mimba..na ukikuta ana-mimba, anza kuwa unachelewa kurudi na uwe unasafiri mara kwa mara...mimba yake imekuchukia...na anza kununua nguo za mtoto wa kiume..na atafanana na wewe kila kituuuuu.
 
wanaume wengine kama wewe huwa siwaelewi!jiangalie,labda ushawekwa kwenye chupa!
 
Wakuu,

Mke hanitaki nifanyeje?

Tayari tumejaaliwa watoto wawili, ingawa husema kuwa watoto siyo wa kwangu. Hua ananiletea kiburi na jeuri na hata hataki kufanya usafi wa mafazi yangu.

Naombeni ushauri.

Kabla sijazungumza chochote, unaweza kunijibu yafuatayo?
  • Malalamiko haya kwamba hakutaki yamenza lini, tangu mlipofunga ndoa au siku chache zilizopita?
  • Kulikuwa na migogoro yoyote kabla ya kauli hizi kuanza?
  • Mkeo anafanya kazi gani na wewe pia unajishughulisha na nini?
  • Wazazi, Ndugu, jamaa au marafiki wa karibu wana taarifa zozote kuhusu ugomvi wenu? Waliamua nini?
  • Mkeo anatoa sababu gani anaposema kuwa hakutaki?

Saa nyingine si vyema kubeza maneno ya mke, hususan mkeo anapotamka maneno mazito kama haya kuwa hukutaki na hata watoto si wako. Ni vyema kufanya uchunguzi wa kina kujua tatizo hasa, na kisha kufuatilia hata hizo kauli kwa kufanya vipimo vya DNA. Kwa upande wangu, kauli na kiburi anachoonyesha kwako ni dalili ya kuwa kuna kitu kwenye mahusiano yenu ambacho kimemchosha sana mpaka kashindwa kuvumilia na ndoa yenu anaiona haina maana tena ....!
 
hata hataki kufanya usafi wa mafazi yangu.
Yani katika grievances zako zoote umeona tatizo ni kufanyiwa "usafi wa mafasi yangu." Duu, nashukuru Mungu na wazazi niliokuwa nao nilijifunza kamwe kutotegemea mwanamke eti anifanyie "usafi wa mafasi yangu." I mean, just go wash your draws man!
 

wewe ndio utakua na shida
mke akukatae bila sababu?
kua muwazi ushauriwe uzuri!!
 
na we mwambie SIKUTAKI too!
maisha yenyewe mafupi hiv,unakuwa na mke anakuletea maneno ya jeuri jeuri kiasi hicho unakuja kushtaki JF!
VAA SURA YA KAZI!!!!!kuwa mume ni swala moja,lakini kuwa mume mwanaume its quite something else!
 
Wakuu,

Mke hanitaki nifanyeje?

Tayari tumejaaliwa watoto wawili, ingawa husema kuwa watoto siyo wa kwangu. Hua ananiletea kiburi na jeuri na hata hataki kufanya usafi wa mafazi yangu.

Naombeni ushauri.

Mwache aende kwa mme mwenzio alio zaa nao watoto, wewe unamng'ang'aniaje mwanamke asiye kupenda wanaume wengine mabwege sana
 
Wakuu,

Mke hanitaki nifanyeje?

Tayari tumejaaliwa watoto wawili, ingawa husema kuwa watoto siyo wa kwangu. Hua ananiletea kiburi na jeuri na hata hataki kufanya usafi wa mafazi yangu.

Naombeni ushauri.

Japo maelezo yako yanatoa wigo mwembamba wa mtu kukushauri lakini kwa haraka haraka kuna jambo dogo la kufanya; nalo ni hili: chukua muda wa kutosha, hakikisha hauna mawazo magumu/mazito yaani no stress halafu jitathimini vya kutosha wewe mwenyewe na pia mtathimini vya kutosha huyo mke wako, naamini kuna mmoja ambae ndie chanzo cha tatizo! ndoa ya watoto wawili halafu mwenzako anapata ujasiri wa kukuambia watoto si wako kidogo inataka maelezo yenye afya!! mmoja wenu aweza kuwa ndie chanzo cha tatizo na ndie chanzo cha utatuzi wa tatizo!

pole sana!
 
umemkasirishatu, watoto ni wako, wangu alikua ananifukuza hataki hata kunisogelea when she was preg lakini and that happens only when i was spraying a perfume, siwezi jua kua na huyo wako pia, kama vp pimeni, kama hanayo, umemboa tu..rekebisha
 
Embu jibu kwanza maswali ya wadau kwanza ndio uweze kupewa ushauri wa manufaa. Kuwa mwanaume hata kama mkeo ameshaanza kigongesha nje. Jitathimini kwanza wewe inawezekana ikawa wewe ndiye chanzo cha tatizo
 
Kama anakwambia watoto so wako basis huo ndio ukweli wenyewe halafu kumbe anakwambia kabisa tambua kuna jamaa ndo anampa kiburi weww temana naye
 
sasa km hakutak unataka ss tufanye akutake??ww unalelewa wtt sio wako sasa hapo unataka nn.sepa tuu umechokwa braza
 
Wakuu,

Mke hanitaki nifanyeje?

Tayari tumejaaliwa watoto wawili, ingawa husema kuwa watoto siyo wa kwangu. Hua ananiletea kiburi na jeuri na hata hataki kufanya usafi wa mafazi yangu.

Naombeni ushauri.

Mwambie akupe talaka kama kweli yupo serious
 
Mbona mada ya longi sana hii,nina mashaka kwamba ukiona mada ya longi imefufuliwa na mtu ambae hakuianzisha basi ni mtu yule yule id tofauti.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom