Godzzo, kitendo cha kutamkiwa kuwa hao watoto sio wako inaonyesha tatizo ni kubwa sana na wew ndio tatizo kuliko hata mkeo. Kama anaweza diriki kutamka hivyo na hapo hapo kukufanyia jeuri na dharau ni moja ya kiashiria kikubwa kuwa yeye ndio kavaa suruali humo ndani.
Ninaposema kuvaa suruali nina maana yawezekana yeye ndio kwa kiasi kikubwa anaendesha maisha humo ndani kwa asilimia kubwa sana hadi kukulea wewe. Suala hili la mke kubeba majukumu kuliko mume in some cases ndio matokeo yake haya. Anajua hata akifanya dharau.. Hata akikutamkia watoto sio wako na kufanya vitimbi vingine vingi huna ubavu wa kuchukua maamuzi yoyote na hata ikitokea uondoke na kumuacha hakuna anachopungukiwa.
Ni muhimu saana akina baba kushika na kubeba familia zao ipasavyo kuweza kuleta a bit of balanceit ndani ya nyumba na pia kuweza kuwa a bit in control hata kama mwaishi na mkeo kama equal patners.
Kama si hivyo nilivyogusia, ni vema ukaeleza wewe wadhani nini chanzo cha tatizo. All in all pole sana.