Mke wa mchuchu yuko busy kunitafutia mume - imekaaje hii

Sal

JF-Expert Member
Jan 14, 2008
498
228
hanijui, simjui. tumekutana bahati mbaya kwenye salon ya mke wa boss wa mume wake. ndio salon niendayo na mchuchu alishaniambia kua kuna siku nitakutana na mkewe maana ndio salon yake nae.
siku isokua na jina ikafika. mama mwenye salon nimemzoea na tunaongea sana maana mimi ni mteja wake mzuri. nimekwenda kama kawaida yetu saa nyingine unaweza kushinda salon maana mambo mengi, kuanzia makucha, nyuso, nywele, vyote hivi mpaka uvimalize ni siku nzima. mke wa mchuchu kaingia. mimi simfahamu nae hanifahamu, mama mwenye salon kampokea, karibu mama mhina (sio jina lake) nikashtuka maana jina mhina jina la mchuchu wangu.
vile tumezoeana, mama mwenye salon katoa intro. kutana na mteja wangu mzuri sana Ms. Baltazar (not my real name), tukashikana mikono, michapo ikaanza. wote tuko around the same age. wao wameoelewa, ila mimi niko single lakini niko na Mr. Mhina kama mfadhili wangu mjini. maongezi ya masaa, tuko salon na vi wine tukaanza kunywa. kidogo Mrs. Mhina "jamani Ms Baltazar nimekuona leo tu lakini nimependa sana company yako. unaonaje tukionana tena siku nyingine for a drink. Naomba namba yako ya simu" nikataka kukataa nimpe ya uongo lakini nikahisi asije akasema ngoja nikubipu u-save yangu, kama tulivyo waswahili. ikabidi nimpe namba. miezi kadhaa ikapita, hakunipigia. muwewe wala sikumwambia, niliuchuna maana asije akadhani nilijishaua nijulikane japo ananijua sina hizo. siku nyingine tutakutana tena. ni salon yake na mimi pia ni yangu. "shoga jamani za siku nyingi, hujanitafuta?" nikamwambia nilidhani utanitafuta wewe. basi tukaongea michapo ya kimama maana wote matured ladies.
Katika maongezi mama mhina akachomekea, "jamani tuna family friend wetu, very matured guy, aliachana na mkewe some years back, anatafuta mke, jamani naomba nikuunganishe. yaani anataka mtu kama wewe"
Toba!, nikapigwa na butwaa. mama mwenye salon nae anaongezea, si kwa ajili ya Petro? anamjibu ndio. kwa kweli wata match. wana supotiana wenyewe, mie nacheka usoni lakini moyoni niko hoi.
hiyo sasa ilibidi mchuchu nimwambie kua mkeo nimekutana nae na yuko mbioni kuniunganisha na Petro. Huyo Petro nishamsikia sana mdomoni mwa mchuchu lakini simfahamu. mchuchu ananijibu, "mke wangu kaniambia amekutana na mwanamke mwema sana salon angependa tumkutanishe na Petro, ila sikujua kama ni wewe la azizi wangu"
Sasa wana JF naomba mnipe ushauri, Mr & Mrs Mhina wameandaa lunch siku ya pasaka maana pia wana kitu cha kifamilia kinakumbukwa, na ndio siku pia Mrs. Mhina anasema lazima niende nikakutane na Petro.
Petro keshanisikia sana jina langu kwa mchuchu, according to him, lakini hatujuani. Mimi sitaki hata kupeleka uso wangu huko kwao, ila mchuchu anadai eti inabidi anitambulishe kwa Petro mapema ili tujuane kabisa kua mashemeji hata kwenye easter tukionana iwe danganya toto. hapa ninapoandika Mrs. Mhina, ni kila siku napigiwa simu, ili mradi sina pa kukwepea. Natamani niumwe.
Mimi na mchuchu hatutaki kuachana. tuna miaka mitano pamoja sasa. mahusiano ya ki utu uzima.
(Imemkuta rafiki, naomba tumshauri) Akale pasaka, au aitolee nje? kama nikutoa nje, mpeni ushauri how?
 
mwambie mrs mhina kamshtukia kuwa anatembea na mume wake, na anampeleka kwa peter makusudi ili ajitulize na wakwake badala ya kung'ang'ania vya wenzake..........

Aende tu kwenye mlo pasaka akutane na peter ......
 
Wewe au rafiki. Acha mume wa mtu. Mtafute wako, tulia kwanza kama petro ni wako atakuja muda muafaka. Kama mumeo akiibiwa utapenda?
 
ONYO: MME/MKE wa mwenzio ni sumu....
here we go now,aende akaonane na petro kama atampenda aachane na mme wa mtu awe wa petro.....over.
 
Petro ni best friend wa mhina, haiwezekani hiyo. mume wa mtu ni sumu kwa watu kuongea tu lakini vitendo huwa hakuna.

ONYO: MME/MKE wa mwenzio ni sumu....
here we go now,aende akaonane na petro kama atampenda aachane na mme wa mtu awe wa petro.....over.
 
waume zetu wanaibiwa kutwa lakini bado tupo nao. huyo shoga sio wa kwanza na sio wa mwisho kuiba mume wa mtu anaendeleza walio anza

Wewe au rafiki. Acha mume wa mtu. Mtafute wako, tulia kwanza kama petro ni wako atakuja muda muafaka. Kama mumeo akiibiwa utapenda?
 
Petro ni best friend wa mhina, haiwezekani hiyo. mume wa mtu ni sumu kwa watu kuongea tu lakini vitendo huwa hakuna.

achana nao wote,subiri wa kwako mkuu,vya watu ni hatari atii....
 
Mke wa mchuchu wako ameshagundua uhusiano wako na mumewe. Anachokifanya ni ustaarabu wa kuvunja uhusiano wenu sasa wewe ukiwa mbishi kinachofuatia ni kuharibu hiyo reception yako kwa tindikali then tuone kama mchuchu ataendelea nawe! you have been warned, chukua tahadhari!!!
 
Jaribu kujiweka upande wa mwenzio..kwamba wewe ndio ungekuwa unafanyiwa hivyo ungejisikiaje? Ukipata jibu lake then tafakari alafu chukua hatua...
 
Mwaego vizuri kula na wenzio. Mbona wao wanakula wake za wenzao na wake zao wanaliwa na waume wenzao. Hayo maneno tu. Pasaka kaile ikiwezekana na petro kama atakufaa fresh wajoin tu.
 
waume zetu wanaibiwa kutwa lakini bado tupo nao. huyo shoga sio wa kwanza na sio wa mwisho kuiba mume wa mtu anaendeleza walio anza

wee Sal wewe....hapa umenimaliza kabisa.....
 
hanijui, simjui. tumekutana bahati mbaya kwenye salon ya mke wa boss wa mume wake. ndio salon niendayo na mchuchu alishaniambia kua kuna siku nitakutana na mkewe maana ndio salon yake nae.
siku isokua na jina ikafika. mama mwenye salon nimemzoea na tunaongea sana maana mimi ni mteja wake mzuri. nimekwenda kama kawaida yetu saa nyingine unaweza kushinda salon maana mambo mengi, kuanzia makucha, nyuso, nywele, vyote hivi mpaka uvimalize ni siku nzima. mke wa mchuchu kaingia. mimi simfahamu nae hanifahamu, mama mwenye salon kampokea, karibu mama mhina (sio jina lake) nikashtuka maana jina mhina jina la mchuchu wangu.
vile tumezoeana, mama mwenye salon katoa intro. kutana na mteja wangu mzuri sana Ms. Baltazar (not my real name), tukashikana mikono, michapo ikaanza. wote tuko around the same age. wao wameoelewa, ila mimi niko single lakini niko na Mr. Mhina kama mfadhili wangu mjini. maongezi ya masaa, tuko salon na vi wine tukaanza kunywa. kidogo Mrs. Mhina "jamani Ms Baltazar nimekuona leo tu lakini nimependa sana company yako. unaonaje tukionana tena siku nyingine for a drink. Naomba namba yako ya simu" nikataka kukataa nimpe ya uongo lakini nikahisi asije akasema ngoja nikubipu u-save yangu, kama tulivyo waswahili. ikabidi nimpe namba. miezi kadhaa ikapita, hakunipigia. muwewe wala sikumwambia, niliuchuna maana asije akadhani nilijishaua nijulikane japo ananijua sina hizo. siku nyingine tutakutana tena. ni salon yake na mimi pia ni yangu. "shoga jamani za siku nyingi, hujanitafuta?" nikamwambia nilidhani utanitafuta wewe. basi tukaongea michapo ya kimama maana wote matured ladies.
Katika maongezi mama mhina akachomekea, "jamani tuna family friend wetu, very matured guy, aliachana na mkewe some years back, anatafuta mke, jamani naomba nikuunganishe. yaani anataka mtu kama wewe"
Toba!, nikapigwa na butwaa. mama mwenye salon nae anaongezea, si kwa ajili ya Petro? anamjibu ndio. kwa kweli wata match. wana supotiana wenyewe, mie nacheka usoni lakini moyoni niko hoi.
hiyo sasa ilibidi mchuchu nimwambie kua mkeo nimekutana nae na yuko mbioni kuniunganisha na Petro. Huyo Petro nishamsikia sana mdomoni mwa mchuchu lakini simfahamu. mchuchu ananijibu, "mke wangu kaniambia amekutana na mwanamke mwema sana salon angependa tumkutanishe na Petro, ila sikujua kama ni wewe la azizi wangu"
Sasa wana JF naomba mnipe ushauri, Mr & Mrs Mhina wameandaa lunch siku ya pasaka maana pia wana kitu cha kifamilia kinakumbukwa, na ndio siku pia Mrs. Mhina anasema lazima niende nikakutane na Petro.
Petro keshanisikia sana jina langu kwa mchuchu, according to him, lakini hatujuani. Mimi sitaki hata kupeleka uso wangu huko kwao, ila mchuchu anadai eti inabidi anitambulishe kwa Petro mapema ili tujuane kabisa kua mashemeji hata kwenye easter tukionana iwe danganya toto. hapa ninapoandika Mrs. Mhina, ni kila siku napigiwa simu, ili mradi sina pa kukwepea. Natamani niumwe.
Mimi na mchuchu hatutaki kuachana. tuna miaka mitano pamoja sasa. mahusiano ya ki utu uzima.
(Imemkuta rafiki, naomba tumshauri) Akale pasaka, au aitolee nje? kama nikutoa nje, mpeni ushauri how?

Umeng'ang'ania "mchuchu mchuchu"
DEFINE MCHUCHU?_____________
 
Kwa nilivyokuanalyse inaonesha we age imekwenda kidogo(si sana usiogope)..

Haya faida unazopata:
company ya 'mchuchu'(what is mchuchu anyway?),
pesa(yani mke mtu angejua mumewe ndo anagharamikia uwepo wenu wawili hapo saloon!),
usafiri(labda)

Hasara:
-Only a matter of time before tindikali meets your reception
-You will grow old lonely
-Your dignity kwa jamii inagaragara kwenye vumbi as we speak
-God hates your, parents hates you, rafiki zako wanaspeak behind your back(kwa kifupi u have a whole bunch of people hating you. Rafiki zako wenyewe wanakuogopa manake ww mtaalamu wa kuruka na visivyo vyako).
-Wewe ni adui wa jamii coz pesa jamaa angetakiwa awape gud education watoto wake ili waikomboe nchi hii unakula wewe bila aibu..(We are Jamii forum by the way so to us Jamii comes first)

Question:
How do you go to sleep at night?
 
kumbe mume wa mtu mtamu eeh.. but sal kasema rafiki yake ndiyo mwenye hilo tatizo, mbona mnamkomalia yeye sasa?
 
Mi ningekushauri kwanza jitahidi kupunguza mawasiliano na huyo mke wa hawara yako, potezea kabisa. Na pili fanya kila mbinu usiende nyumbani kwake, usiende kabisa.

Ku-intertain mawasiliano na huyo dada wakati unanijua wewe ni nyoka kwake ni ufedhuli uliopitiliza kabisa.

Na mwisho achana na mume wa mtu ili Mungu akupe wa kwako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom