Mke anampenda mama zaidi yangu

Mke anampenda mama zaidi yangu

esitena tetena

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2015
Posts
1,747
Reaction score
1,082
nimeoa mke na tunaishi jirani na mama mzazi.nimegundua kuwa:-

1.mke wangu hana mapenzi ya dhati na mimi, bali alikubali tu kwa kuwa nilimpa ujauzito kabla ya kumuoa.

ananiletea kiburi na nikimkaripia ananiambia nimrudishe kwao. ninapopeleka mashtaka kwa mama anamkingia kifua maana wanapendana sana na kwa kweli anamhudumia vizuri sana mama yangu.

2. ana tabia ya uongo sana na nimejitahidi kumrekebisha bila mafanikio.

3. ana tabia ya uchafu kuanzia nguo hadi nyumbani, ameshindwa kabisa kujibadilisha hadi nimejiachia kumuelimisha.

nashindwa kumuacha maana ni kipenzi cha mama yangu na naogopa laana ya mama na nimetumia wazee lakini mama hataki kunielewa.

nifanyeje?
 
mwanamke akiahakuwa hakutaki kweli kutoka miyoni mwake utachoka sana kumbasilisha hata hapati hamu yakupamba nyumba yake, muulize kama bado anapenda kuwa nawe akisema hapendi basi mruhusu aondoke
 
Kosea kuoa/kuolewa uone ugumu WA maisha ulivyo wakat unaoa ulimua kwa lengo gani? Kumhudumia mzazi Wako alipaswa afanye hayo maana mama ndo aliokuzaa bila ya yy hata hizo dharau angezifanyia wapi?
 
Pole sana kwa kupata mke mchafu. I can't imagine
 
MKUU, WEWE UMESHENA WIVU !! HEBU PUNGUZA KUMCONTROL HUYO BINTI!! MPE NAFASI AFANYE KAZI MOJA BAADA INGINE.... ( yaani akutunze wewe, angalie usafi wa nyumba, amhudumie mama,achati, aongee na jirani...mmmmh ) happo kazi tu !! "give her a break!!
 
Mpe mama huyo mke,wewe oa mwingine. Easy..
Halafu laana haiji kirahisi hivyo wajameni,kungekuwa na wengi sana walioathirika na hiyo kitu kama ingekuwa inatoka kinamna hiyo.
 
2. Kama ni muongo uchukulie ni udhaifu...au weee huna madhaifu?

3. Hapo kwenye usafi ushajua mwenzio zero si ufanye? Au wewe ndio aina ya wanaume ambao mnataka kufanyiwa kila kitu? Maana ya kuwa wawili ni nini kama hamuwezi kuchukuliana na kusitiriana?

1...........kuna wenzio wao na mama wakwe ni paka na panya.......ngoja waje watakushauri
 
MKUU, WEWE UMESHENA WIVU !! HEBU PUNGUZA KUMCONTROL HUYO BINTI!! MPE NAFASI AFANYE KAZI MOJA BAADA INGINE.... ( yaani akutunze wewe, angalie usafi wa nyumba, amhudumie mama,achati, aongee na jirani...mmmmh ) happo kazi tu !! "give her a break!!

sikukataa yeye kumhudumia mama,ila anatakiwa awajibike zaidi kwangu mume wake au kwa mama?kwani nami nisingemuoa mama angemuonea wapi?na huyo mke si amemfahamu mama kupitia mimi?na uchafu na uongo je?
 
Na kushauri kaa vizur na mama yako ongea nae vizur amuelekeze mke wako. ujue ni bahat sana kupa mke ambaye anapenda na mama yako na isitoshe umesema ana mapenz zaid kwa mama yako bado una uwezo wa kumrudisha na akawa mke bora kwako.kama kwel yeye na mama yako zinaiva sana ongea na mama tu amueleweshe then na ww uwe unajitahidi hata kumsaidia vikaz vidogo vidogo huku mna eleweshana mambo madogo madogo then onyesha kumjal kumpenda na kumthamin kuna mtu alisema kama muongo uchukulie kama udhaif wake. Na swala la usaf jitah muwe mnasaidiana. Pia usiwe na hasira pindi unapokuwa unaongea nae tumia hekima tu na hope atakuelewa kumbuka mapenz ni ya wawil kama alikukubalia ukampa mimba ni rahisi na yeye akabadilika kama utakuwa na ww unachangia ktk malez ya familia. hope umepata kidogo ambacho kitakusaidia.
 
Yani mwanamke akishakua mchafu tu,sitamani hata kumuangalia.
 
Lazima yy na mama yk wana siri kubwa ambayo ww hauijui na hauto ijua mpk nikwambie.mama yk na mkeo ni wachawi kwa hy luck hufanya kazi pa 1 na hatoweza watenganisha acha woga. Fanya maamuzi yk alafu wao waache wafanye yao
 
Back
Top Bottom