Tunaweza kudhani kaomba msamaha katika hali ya kawaida ya majuto ya kibinadamu, tunaweza kudhani kwamba kaamua kuwa muungwana na kufanya kitubio ili abaki na amani LAKINI katika picha pana ni salamu kwa Jakaya ni salamu za kutaka naye ajitokeze na kukiri pale alipokosea....halafu?
Ni salamu pia kwa Magufuri kwamba a jifunze kutokana na makosa ya watangulizi wake na kikubwa ASIKILIZE maoni ya wengine ASIKILIZE wananchi wanataka nini kwakuwa huko tuendako hakutakuwa na nafasi ya kuomba msamaha ukiwa jukwaani umevaa suti unasikilizwa bila kuhojiwa huku ukipigiwa makofi..!