Mkapa: Najuta

Alikuwa jeuri na mbabe sana huyu... msamaha empty tu utasaidia nn...? I don't accept...!! NBC asidanganye watu, MWALIMU ALIPINGA sana sana... na watu wengi wasomi walipinga.. ila yeye alibinafsisha nakuwapa makaburu rafiki zake..!! Kama ana uchungu na nchi hii AKAUZE HOTEL YA KIMATAIFA ILE PALE DURBAN South Africa aliyojengewa na matajiri kama asante... na siku ya ufunguzi wa hotel hiyo ya KIFAHARI, alimwalika Mh. Nelson Mandela na ALIKATAA NA KUMUONA HAFAI, sbb MANDELA ALIJUA NI RUSHWA HIYO na kumwambia pamoja umehongwa na nchi yenu maskini na umepewa asante na matajiri si basi UNGEJENGA HATA KWENU TZ watu wako wapate ajira..!!

Huyu nae ni walewale..!!
 
Ashatu......................Kwa miaka yote ijayo halafu anatuomba msamaha.Kama anajuta amefanya nini kuhusu hilo.Bado juzi kati kaita watu malofa . simuelewi.
 

Afunguliwe mashtaka kwa katiba ipi....!???
 
Huyu nae atuache Watanzania,atatuomba msamaha kwa mangapi?
Unafiki tu.

Alikuwa wapi miaka yote hiyo?

Anataka kututumia Watanzania kama jukwaa la kumfikishia madongo aliyemkabidhi kijiti miaka hiyo.
 
Y
Hivi Mkapa anaweza kutuhakikishia kwamba Mwalimu aliukubali ubinafsishwaji wa NBC?
Huyu jamaa ni muongo, na ndiyo maana kila kukicha nafsi inamhukumu kwa matendo aliyoyafanya akiwa Rais.
Yani hapa ndio kaniacha hoi-afu bado anasema anajuta kosa kwa kuendelea kisema uongo
 
Mkapa ni mtu aliyetumia IQ ndogo ya Watanzania kutawala nchi na kutuingiza matatani
 

Sio kwamba watanzania walikosa hoja sema ktk kipindi hicho watanzania walikuwa mbumbumbu alitumia uwezo mdog po wa kifikira wa watanzania kutatawala atakavyo
 

1. Watu wengi waliathirika na ubunafsishaji wa baadhi ya mashirika ya umma kwa mfn pale TRC idadi kubwa walipoteza ajira.

Mkapa anajua mateso ya kukosa ajira?

2. Sekta za reli na bandari zimekufa au kuzorota na kuathiri uchumi wa nchi vibaya sana. Je Mkapa anajua hasara ya jambo hili?

3. Uamuzi wake wa kubinafsisha mashirika hayo ulihusu pia uuzaji wa ardhi (viwanja) na nyumba za wafanyakazi wa mashirika hayo!

Mkapa anasema nini kuhusu makosa haya na atafanya mini ili nyumba na ardhi hizo zirudishwe ili mashirika hayo yasiathirike kiuendeshaji kwa kukosa nyumba za wafanyakazi na maeneo ya ardhi ambayo yangetumika kwa mahitaji mengine?

4. Hivi kubinafsisha Kongolo Quarry ya TAZARA na Tura Quarry ya TRC ili mashirika haya yanunue mawe yaani kokoto kwa mwekezaji; kwa akili ya kawaida tu, na hili Mkapa anaona lilikuwa jambo la busara?

Kwa mtazamo makini, huwezi kukwepa uwezekano wa 'vimelea' vya ufisadi kwenye zoezi zima la ubinafsishaji wa sekta hizi; kiasi kwamba haitoshi kwa Mkapa kusema tu kuwa anakubali makosa. Labda aseme mwenyewe atawajibika vipi kwa madhambi haya?

Hawezi kusema anakiri makosa halafu anakuwa mkali na kukemea wanaofuatilia mambo haya kwamba 'wasiwe walalamikaji' au wasiwajadili watu binafsi nk. nk.; Ukiwa Rais wa nchi lazima tukujadili we we binafsi kwasababu Ikulu ni mahali PATAKATIFU. Sio sehemu ya kwenda kujaribu au kubahatisha mambo yako kwa gharama ya uhai wa taifa zima!
Halafu ukiulizwa Katiba mpya ilikwama vipi unakwepa swali! Lakini wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu ulionekana unapanda majukwaani kuwatetea wana CCM wenzako waliozima harakati za katiba mpya!

Niseme tu, jamani! Nahisi kwamba Mkapa hajutii makosa yake wala hana muda na vitu kama Demokrasia ya vyama vingi, Utawala Bora au Ukweli na Uwazi aliouhubiri enzi zake. Bali kwake ni lazima CCM yake iendelee kutwawala, na kwa gharama yoyote.

Ndiyo maana nadiriki kusema Mkapa hawezi kusema kitu kuhusu mgogoro wa Zanzibar. Kwake kilichofanyika huko ni demokrasia. Tena nadhani akiulizwa jambo kuhusu hilo atakuwa mkali kweli kweli!
Mimi namsamehe.
 


Jamani tunahitaji katiba mpya...Huyu Mkapa si wa kutuomba msamaha wala kuongea hadharani kwani ilibidi akamatwe kitambo kwa kuifilisi nchi na wizi alioufanya yeye na mkewe kipindi akiwa rais. Eti leo anatuomba msamaha? Huyu anatusanifu tu, inabidi akamatwe haraka sana.
 
Huyu nae atuache Watanzania,atatuomba msamaha kwa mangapi?
Unafiki tu.
Alikuwa wapi miaka yote hiyo?
Anataka kututumia Watanzania kama jukwaa la kumfikishia madongo aliyemkabidhi kijiti miaka hiyo.
Kijiti akamuachia Vasco Da Gama.... the discoverer of new lands overseas....

masikini...

Mi nasema MAGUFULI aongeze tu udictator.. maradufu.
 
crocodile tears... Machozi ya mamba ni ya unafiki sio kwamba anakuonea huruma kama haujui mamba anapootea mnyama au mtu na kumkamata pale anapokuwa anamtafuna huwa anatafuna mpaka anatokwa na machozi lakini ndo anafurahia utamu hivyo, ni sawa na hawa vigogo waliojilimbikizia mali za watanzania alafu wanajifanya kutuonea huruma mambo yanavyozidi kuwa magumu
 
Tubadili katiba watu kama hawa wakaozee jela tu...huwezi kuisababishia nchi hasara halafu eti uombe msamaha kirahisirahisi
 
NBC inaniuma mpaka leo.......na mkapa asitudanganye eti hata mwalimu alitaka NBC iuzwe....wakati nyerere mpaka anakufa analalamikia kuhusu nbc.....tunamuomba awe mkweli........mwalimu mpaka aliuliza kuwa "can nbc open a branch in new york"?...
Katika utawala wake alibinafsisha ziwa Victoria kwa miaka 99 kitu ambacho kimewafanya wananchi kuishi ka maskini kwenye nchi yao wakati Mungu aliwapa ziwa liwakomboe. Leo wanaishia kuogelea tu na kupiga picha basi lakini kuhusu kitoweo haipo tena, wanakula mabaki tu na mifupa. Katika hili kamwe siwezi kumsahau mkapa
 
Nani wa kumfunga paka kengele? mswada upelekwa bungeni wa rais mstaafu kushitakiwa akiwe ameboronga, je?nan hataupeleka huo mswada???
 
Wengi hawatomsamehe
 
Na inaniuma kwa mauaji yaliyotokea Mwembechai na Zanzibar wakati wa Utawala wake kwa kweli inauma sanaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Mimi namkumbuka tu Mkapa kama kiongozi aliyekosa mbinu za kuinua uchumi na kupata fedha za kuendesha nchi, jambo lililosababisha aamue kuuza nyumba 8000 na kuuza mashirika zaidi ya 360 kwa bei chee ili apate pesa za kuendesha nchi.
Namkumbuka sana kwa huu usanii na ukosefu wa mipango wa kuinua uchumi hata kwa kukodisha au kupangisha zile nyumba za umma zilizouzwa kwa bei ya kodi ya kupangisha kwa mwaka mmoja tu.

Watanzania inabidi tumsamehe tu mana sisi ndio tuliamua wenyewe kumpa nchi na katiba inayomfanya aiendeshe nchi kama mali yake binafsi.
Aliitendea haki katiba yake na kuwafanya wananchi waisome namba.
Mpaka leo bado tunaendelea kuwapa watu wale wale madaraka kwa kutumia katiba ile ile yenye mambo yale yale chini ya chama kile kile na idadi kubwa ya wabunge wa chama kile kile.

Wakiwa madarakani wanazungukwa na wapambe wengi wa kuwakingia kifua ili wasikosolewe lakini wanapoondoka ndipo tunaanza kuwaomba waje kuomba msamaha kwa mambo ambayo walikua wameshaonywa na kuambiwa kuwa wanakosea wakakaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…