Mkapa na Mzee Mwinyi hamuitendei haki nchi

Mkapa na Mzee Mwinyi hamuitendei haki nchi

fisi 2

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2010
Posts
3,284
Reaction score
4,652
Kukaa Kwao kimya wakati NCHI ipo kwenye mitikisiko, kuacha kukemea mapungufu ya wazi haswa rushwa na ufisadi. Miezi 4 Kabla ya uchaguzi mkuu wananchi hawajui nini kitakuwa namna gani. Come on wazee wetu. Jitokezeni mtoe mwongozo kwa NCHI.
 
Aliye msafi awe wa kwanza kumnyoshea mwenzake kidole
 
Hata kama sio wasafi tunataka tuone upendo wao na nchi hii...
 
Na sisi wagumu kuwasikiliza wazee tunaona wamepitwa na wakati. Tunafanya tunavyotaka wenyewe sasa maji yako shingoni tunawageukia wao na kuwalaumu kabisa too late! Ngoja yatukute!
 
Aliye msafi awe wa kwanza kumnyoshea mwenzake kidole

Mimi nadhani haujamuelewa mtoa mada,yeye anasema watoe neno,hapo inaweza kuwa ni ushauri,au maoni yao au chochote kile ili mradi tu neno hilo liwe lina lenga ktk kupata mwelekeo bora kwa taifa.Na kutoa neno hata km ni karipio haina maana kuwa umemnyoshea kidole au umemhukumu km ingalikuwa kwamba mwenye makosa hatakiwi kumkosoa mwingine basi binadamu tusingelikosoana,kwa kuwa duniani hakuna asiye na mapungufu.
 
Na sisi wagumu kuwasikiliza wazee tunaona wamepitwa na wakati. Tunafanya tunavyotaka wenyewe sasa maji yako shingoni tunawageukia wao na kuwalaumu kabisa too late! Ngoja yatukute!

Kamanda,tatizo ujuaji mwingi.
 
Kukaa Kwao kimya wakati NCHI ipo kwenye mitikisiko, kuacha kukemea mapungufu ya wazi haswa rushwa na ufisadi. Miezi 4 Kabla ya uchaguzi mkuu wananchi hawajui nini kitakuwa namna gani. Come on wazee wetu. Jitokezeni mtoe mwongozo kwa NCHI.

Jamani mbona huwa wanasema!,tena juzi tu nimemsikia mzee Mkapa akitoa ushauri fulani kwenye mambo ya uwekezaji,sema wabongo tunajifanya much know!,tunaona kuwa wazee wamepitwa na wakati,nao wanakata tamaa ya kutushirikisha busara zao.
 
Mimi nadhani haujamuelewa mtoa mada,yeye anasema watoe neno,hapo inaweza kuwa ni ushauri,au maoni yao au chochote kile ili mradi tu neno hilo liwe lina lenga ktk kupata mwelekeo bora kwa taifa.Na kutoa neno hata km ni karipio haina maana kuwa umemnyoshea kidole au umemhukumu km ingalikuwa kwamba mwenye makosa hatakiwi kumkosoa mwingine basi binadamu tusingelikosoana,kwa kuwa duniani hakuna asiye na mapungufu.

Hakuna mwenye ubavu huo, nyerere alikua anakupa wazi, ushauri wa mkeo ofisini
 
Sitaki kusikia lolote kuhusu hawa mafisadi. Sana sana kama wana cha kuongea basi watubu hadharani kwa ufisadi wao mkubwa walioufanya wakiwa Ikulu na kutuomba radhi Watanzania na kurudisha mali yote waliyojipatia kwa njia haramu, vinginevyo wakae kimya tu.

Wenyewe sio wasafi hawawezi kumnyoshea kidole mwenzao.
 
Mkuu umenena chukua LIKE yang
Haah haah mleta mada katoa ushauri mzuri sana.Tangu uchaguzi wa Arumeru mzee Mkapa alinywea baada ya kuingia kwenya 18 za Chadema.Vicent Nyerere alimuumbua mbaya,basi mpaka leo akiona siasa anatamani ardhi ipasuke immeze.Chezea vijana weye!!
 
Haah haah mleta mada katoa ushauri mzuri sana.Tangu uchaguzi wa Arumeru mzee Mkapa alinywea baada ya kuingia kwenya 18 za Chadema.Vicent Nyerere alimuumbua mbaya,basi mpaka leo akiona siasa anatamani ardhi ipasuke immeze.Chezea vijana weye!!

Hahaha na akome
 
Kukaa Kwao kimya wakati NCHI ipo kwenye mitikisiko, kuacha kukemea mapungufu ya wazi haswa rushwa na ufisadi. Miezi 4 Kabla ya uchaguzi mkuu wananchi hawajui nini kitakuwa namna gani. Come on wazee wetu. Jitokezeni mtoe mwongozo kwa NCHI.


Hao uliowataja unafikiri watasema au kumpa nini Kikwete ushauri ikiwa wao wenyewe ni wezi kupindukia? Nyoka anaweza zuia mwanaye asiume mtu? Mkapa na Mwinyi waliiba sana na hakuna asiyejua hii kitu, ufisadi na rushwa chini ya hao uliowataja ulikuwa hatari sana na walifungia macho kisha leo hii waje kutoa ushauri au kukemee kweli?
 
Ccm na serikali yao wote lao moja hakuna wa kumshauri mwenzake...wote wameoza
 
Back
Top Bottom