Mkapa ni makini bila shaka amestushwa na agizo la professa la kupiga marufuku majoho kuvaliwa na wanaomaliza diploma na wengineo kama mkakati wa serikali kuboresha ubora wa elimu!
Kumekuwa na matamko yanayotolewa na watu/mtu binafsi yanayosemekana kwamba yanalenga kuleta ubora wa elimu,ki ukweli yako too personal/yamejikita katika hisia,mihemko,jaziba,mitazamo na jitihada za watu/mtu binafsi kuonekana kwamba wanachapa kazi kupitia media coverage.Tunahitaji maamuzi yanayojumuisha mawazo ya wengi hasa wanataaluma na wadau wa elimu ambayo yatajikita katika kuweka elimu yetu kuendana na mahitaji na uelekeo wa taifa letu katika kutimiza mikakati ya kisera na maendeleo.
Ubora wa elimu hauletwi na tamko au agizo lililo nyuma ya mtazamo au hisia binafsi za mtu mmoja.