Mkalimani ‘feki’ katika hafla ya kumbukumbu ya mandela aomba radhi, adai aliugua ‘schizopheria’ jukw

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,883
155,860
[h=3]MKALIMANI ‘FEKI’ KATIKA HAFLA YA KUMBUKUMBU YA MANDELA AOMBA RADHI, ADAI ALIUGUA ‘SCHIZOPHERIA’ JUKWAANI NA KUPOTEZA ‘NETWORK[/h]

Mkalimani wa alama za viziwi katika hafla ya kumbukumbu ya Mandela iliyofanyika Jumanne wiki hii (Dec 10) afahamika. Anaitwa Thamsanqa Jantjie, 34. Mkalimani huyo ameomba radhi kwa kile kilichotokea baada ya kushtukiwa kuwa ishara alizokuwa anazitoa wakati wa hotuba za viongozi hazikuwa na maana yoyote bali alikuwa anarusha mikono tu.

Kwa mujibu wa Mail Online, Jantjie (34) amesema anaiweza vizuri kazi hiyo lakini siku ya kumbukumbu ya Mandela alianza kusikia makelele kichwani kwake yaliyosababisha aanze kutoa ishara zisizo na maana wakati wa hafla hiyo.

Mr Jantjie ameomba radhi kwa tukio hilo na kuongeza kuwa hakujua kilichosababisha hali hiyo imtokee,lakini amekiri kuwahi kulazwa hospitali ya vichaa kwa zaidi ya mwaka mmoja.


“’There was nothing I could do. I was alone in a very dangerous situation. I tried to control myself and not show the world what was going on. I am very sorry. It’s the situation I found myself in.” Mr Jantjie aliliambia gazeti la Star newspaper la Johannesburg.
Aliongeza kuwa “What happened that day, I see angels come to the stadium … I start realizing that the problem is here. And the problem, I don’t know the attack of this problem, how will it comes. Sometimes I react violent on that place. Sometimes I will see things that chase me,”.

Jantjie akizunguzma nyumbani kwake Bramfischerville, South Africa, jana (Dec. 11, 2013)

Ameongeza kuwa licha ya kujigundua alikuwa kwenye hali ngumu, lakini alijitahidi asipanic kutokana na ulinzi mkubwa uliokuwa umemzunguka, kwasababu hakutaka kuiaibisha nchi yake.
Mkalimani huyo amedai kwamba alifanya kazi na kampuni iitwayo SA Interpreters iliyopewa kazi na ANC kwa ajili ya hafla ya kumbukumbu ya Mandela, iliyohudhuriwa na viongozi wa mataifa mbalimbali akiwezmo Rais wa Marekani Barrack Obama katika uwanja wa FNB, Johannesburg Jumanne wiki hii.
Shirika la habari la AP lilipojaribu kumuonesha video clip ya tukio hilo wakati anatafsiri katika memorial service ya Mandela, Jantjie alisema hakumbuki chochote alichooneshwa katika video hiyo licha ya kuwa ni yeye aliyekuwa anakalimani,”I don’t remember any of this at all”, alisema.

Mr Jantjie amesema alilipwa dola 85 (135,000 Tsh) kwaajili ya kukalimani siku hiyo. Mr Jantjie amedai kuwa ukalimani ndiyo kazi yake ya kila siku inayomuingizia kipato.

SOURCE: MAIL ONLINE
 
Sijui kwa nini mtu aliyetoka kuugua maradhi ya ukichaa alipewa nafasi hiyo??
Safi lakini amechekesha msibani. Ni moment ya kipekee sana maadui wakubwa wakikutana. Machozi na tabasamu
 
hapa penye red, kuwa alijitahidi asiibishe nchi yake sijajua kama katika kujitahidi huko aliweza . kusimama na obama si mchezo. chezea obama weye....
 
hajui tu, Obama ni kama Pope huwa analindwa na malaika hivyo ana upako mwingi xana, :tape: inahitaji akaombewe... chezea Obama.......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…