Mkakati wa kuing'oa C.W.T

Mkakati wa kuing'oa C.W.T

Mmiskiry

Member
Joined
Mar 1, 2018
Posts
55
Reaction score
21
#NIMEITOA_KWENYE_GROUP_MOJA_HUKO.

MKAKATI WA KUIN'GOA CWT KISHERIA NA KUWARUDISHIA WALIMU PESA ZAO WALIZOIBIWA NA CWT PAMOJA NA FIDIA

Nimepitia mijadala mingi na malalamiko mengi ya WALIMU dhidi ya CWT, Hotuba ya Rais Magufuli na Mkuu wa Wilaya wa Hai dhidi ya madudu ya CWT.

Nashauri,CWT nigenge la ajabu na Haliwezi kukoma kuwepo bila ya KUTUMIA njia ya Mahakama.

Ni Mahakama pekee ndio inaweza kumkomboa Mwalimu hivyo nashauri tufungue kesi ya kudai yafuatayo (briefly)

1. Viongozi wa CWT watupatie majina ya WALIMU waanzilishi wa CWT pamoja na nakala ya CERTIFICATE OF REGISTRATION-sababu ni haki ya WALIMU kupatiwa

2. CWT watupatie nakala ya "Authorized Budjet"ya miaka mitano-kama sheria inavyoelekeza kuwa Mwalimu anatakiwa apate nakala hizo for five years consecutively if needed. Authorised Budget ndio document inayotakiwa kuonyesha mapato na matumizi,kiasi cha pesa kilichopo,assets, liabilities,idadi ya wanachama, wafanyakazi, budget ya mishahara, idadi ya walimu wanaokatwa agency fees, kodi zinazolipwa, n.k

3.C WT watupatie "company profile" ya Tanzania Teachers Development Co.Ltd (TDCL) Kampuni hii ndio inayomiliki shares katika BENKI YA WALIMU, na pia inamiliki vitega uchumi. Ukienda kwenye soko la hisa Dar es Salaam utaijua zaidi.

4. CWT watupatie taarifa ya kesi aliyofungua mama Hellen Mbezi na wakili Tarimo dhidi yao pale MCA mwaka 2013. Kesi hii ni muhimu sana kwa mstakabali wa maisha ya MWALIMU Tanzania, but it was cooked behind teachers ignorance.

5. Ufafanuzi wa kisheria juu ya application of the law of agency fees in Tanzania, sababu walimu wamekua wakiibiwa kwa kutumia misapplications.

6. CWT watupatie Anual Financial Reports za Mwalimu Bank maana ni haki ya wanahisa.

7.CWT watupe maelezo ya kisheria yanayoonyesha Walimu ndio wamiliki wa MWALIMU BANK,na nafasi ya walimu katika maamuzi ya Benki hiyo

8. CWT watueleze iwapo wao ni trade union au professional body ya walimu, ili kuondoa utata uliopo kwenye documents zao, wanazijua hizi.

9. CWT wamekuwa wakipokea zaidi ya DOLA ELFU 90 KILA MWAKA kutoka Denmark kwaajili ya kusaidia WALIMU "professional awareness", watuonyeshe mchanganuo wa pesa hizi--wao wanazijua walianza kuzivuna ruzuku hizi mwaka 1998.

10. CWT watupe majibu ya AUDITING ILIYOFANYWA NA PROFESA ASSAD MWAKA 2017

11. TUMTAKE MSAJILI wa vyama Tanzania Mama Uisso atueleze kwanini hajakifuta chama cha CWT mpaka sasa wakati HAWAJAWAHI kutoa "Authorised Budget" kama inavyoelekeza na sheria, na yeye kapewa kazi yakuvifuta vyama visivyofata sheria.

HAYO NI MACHACHE TU..MWALIMU HAWEZI KUJIBIWA HAYA BILA KUTUMIA MAHAKAMA ILIYO HURU NA HAKI,it is very wrong and falacy to take these things easy !!

NASHAURI KUUNDA TIMU YA WANASHERIA ILI KUDAI HAYA. NA GHARAMA YAKE TUNAWEZA KUTUMIA MILIONI 50, yaani kila Mwalimu achangie Shilingi 500/=, walimu laki moja wanatosha.

TOA MAONI YAKO!

Imeandikwa na Farai Alfred


IMG-20200518-WA0020.jpg
IMG-20200518-WA0023.jpg
IMG-20200518-WA0024.jpg
IMG-20200518-WA0027.jpg

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We jamaa umeandika hoja nzito sana. Sijajua kama ni valid sababu sijui katiba ya chama cha walimu na sheria iliyotumika kuanzisha.sijui ni society act au sijui ni ipi

Ila pia nilikuwa najiuliza kwani hiv ni lazima kuwa mwanachama wa chama cha wafanyakazi chochote.na je utaratibu ukoje mtu ukitaka kujitoa?

Maana vyama vyote vya wafanyakazi hata tanzania ni uzushi tuu.yaani huwezi vitofautisha na serikali.viongozi wake ni waoga kuwahi kutokea.wafanyakazi wengi wana madai yao ya malimbikizo kama naul za likizo,mapunjo ya mishahara etc.lakini pia sijui hata wanatembeleaje wanachama kuwauliza kero.

Yaani Tughe,Talgw hivi ni kati ya vyama ambavyo ni viongozi ndiyo wananufaika sana.wanachama wake hakuna wanachonufaika.Hakuna maslahi yoyote zaidi ya tshirt za Mei Mosi.

Anzeni waalimu tutafuata na sisi wa vyama vingine.Tuna wanasheria wengi Nguri sana wako tayari kusaidi kujitolea tuu.
 
Viongozi wa CWT watupatie majina ya WALIMU waanzilishi wa CWT pamoja na nakala ya CERTIFICATE OF REGISTRATION-sababu ni haki ya WALIMU kupatiwa
Kwa nini msiende kwa.msajili,kila kitu kipo
Kama kuna ubadhirifu kwa.nini msipeleke ushahidi takukuru
 
We jamaa unapiga kampeni Acha uhun dogo
Hao wanaogombea wengine ni viongoz hadi Sasa
Je wamefanya mabadiliko gani?? Wakiwa viongoz?

Nyie ni wanyonyaji mpo hapo Kwa maslahi yenu mle mjaze matumbo yenu
Huo ni ujinga

Eti mabadiliko Nyie ni wakuleta mabadiliko gani mzee??

Uliyo andika hapo ulikua huyajui?? Acha unafiki

Huu ujinga hatuutaki mpo kupiga dili tuu
Chama hakina regulatory body kama sekta za afya

Ebu tuelezen jambo mlishafanya la maana?

Faida ya mwalimu bank, kod za majengo, vitega uchumi vyote hivo Bado mnamkata mwalimu hela yake kila Mwez

Mnafanyia nini hizo pesa?? Zinaenda wapi??
Yaan mpo Kwa ajili ya matumbo yenu tuu


Sent by IPhone
 
Adui mkubwa ni CCM hao ni vibaraka tu,,,,hata mkiiondoa CWT mkaweka Mkurabita bado itapewa limbwata na kuminywa na CCM hakuna jipya ila kuna watu wanataka ulaji na umarufu tu hapo
 
Kitendo cha kushusa gawio kwenye matawi na kufika asilimia 9 hapo hamtapata kura na mjue chama kinajengwa na waliochini sasa mkipewa nafasi mnawasahau waliowapa kura. Sikilizeni ongezeni gawio la matawi kutoka asilimia 15 hadi 30 na hisa za walimu ziwekwe wazi kwa wamiliki woteee mhache uchumia tumbo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom