Mjomba Mrisho Mpoto alikuwa mbele ya muda

Deleted01

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2018
Posts
3,886
Reaction score
9,014
Wasalaam,
Miaka 11 iliyopita siku kama ya leo, Mjomba Mrisho Mpoto aliachia kibao chake cha Nikipata Nauli ambacho kilitikisa sana mitaa mbali mbali akimshirikisha Banana Zorro. Reflecting this, kuna mistari imenigusa sana kwenye kibao hiki and nikaona kama mjomba alikuwa mbele ya muda. Mjomba kwenye verse ya 2 anasema,

"Eti wanaomba samahani,
watarudisha uhai wa waliopotea kwa uzembe wao?"

Mjomba alikuwa mbele ya muda even though alivyopata nauli akafika mjini, akatusahau mjomba. Kweli Maskini hana kiapo.

Kipande kipi cha mjomba unakikumbuka kwenye kibao cha Nikipata Nauli?
 
Alimuoa mjombangu kakake mama yangu nikampa zawadi.
........Aliwahi kumuoa Binti yangu akamfurahisha nimempa udc.
 
Mtafute sahivi, mkumbushie hiyo verse vp 😄
Kama ataikumbuka

Ova
 
Ipo siku tutamkumbusha kuwa alishasema hili ila hakujua anaongelea ya sasa
 
Mjomba wa kijijini wakikutana na huyu wa mjini lazima wapigane..!! 😹
 
Ukimkumbusha kwasasa atatamani aufute wimbo wote. Maana alipopata nauli akafika kwa mjomba akasahau kabisa kama alitumwa na wananzengo awapelekee changamoto zao alipofika kwa mjomba akatulizwa kwa ukalimu wa kutosha ikabidi alitii tumbo lake na si wale waliomtuma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…