KERO Mitaro ya maji Mbezi kwa Zena inatia aibu, tunasubiri magonjwa yatokee ndipo usafi ufanyike?

KERO Mitaro ya maji Mbezi kwa Zena inatia aibu, tunasubiri magonjwa yatokee ndipo usafi ufanyike?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Ni takribani wiki mbili sasa nimekuwa na harakati katika eneo maarufu la Kwa Zena lililopo Mbezi Beach-Dar es salaam. Kuna jambo ambalo siwezi kulikalia kimya, licha ya kwamba mimi si mkazi wa eneo hilo.

Mitaro ya maji katika eneo hilo imejaa taka na maji machafu yanayotoa harufu mbaya. Hali hii inatishia afya za wananchi, hususan wakazi wa eneo hilo.

Siku ya kwanza nilipoona tatizo hili, nilidhani labda wahusika wamejisahau kidogo na watalishughulikia. Hata hivyo, matumaini hayo yamepotea baada ya kushuhudia imepita wiki ya pili bila hatua yoyote kuchukuliwa.
photo_2025-08-26_11-27-57.jpg

photo_2025-08-26_11-28-00.jpg

photo_2025-08-26_11-28-01.jpg
Najiuliza: Je, eneo hilo kweli halina mamlaka za usafi? Au watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni wanaosimamia usafi wanangoja hadi magonjwa ya mlipuko yajitokeze ndipo wachukue hatua?

Natoa wito kwa watendaji wenye jukumu la kusimamia usafi, hususan usafi wa mitaro katika eneo hilo, wawajibike ipasavyo badala ya kujifungia maofisini.
 
Ni takribani wiki mbili sasa nimekuwa na harakati katika eneo maarufu la Kwa Zena lililopo Mbezi Beach-Dar es salaam. Kuna jambo ambalo siwezi kulikalia kimya, licha ya kwamba mimi si mkazi wa eneo hilo.

Mitaro ya maji katika eneo hilo imejaa taka na maji machafu yanayotoa harufu mbaya. Hali hii inatishia afya za wananchi, hususan wakazi wa eneo hilo.

Siku ya kwanza nilipoona tatizo hili, nilidhani labda wahusika wamejisahau kidogo na watalishughulikia. Hata hivyo, matumaini hayo yamepotea baada ya kushuhudia imepita wiki ya pili bila hatua yoyote kuchukuliwa.
Najiuliza: Je, eneo hilo kweli halina mamlaka za usafi? Au watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni wanaosimamia usafi wanangoja hadi magonjwa ya mlipuko yajitokeze ndipo wachukue hatua?

Natoa wito kwa watendaji wenye jukumu la kusimamia usafi, hususan usafi wa mitaro katika eneo hilo, wawajibike ipasavyo badala ya kujifungia maofisini.
Leo wameanza kuisafisha. Ukipita utaona,

Chanzo ni ujenzi wa kufunika mifereii ili kupata parking hapo kweye fremu za barabarani,
 
Back
Top Bottom