Mitano Tena: kesho kuzinduliwa Kwa SGR Tanzania to Burundi

Mitano Tena: kesho kuzinduliwa Kwa SGR Tanzania to Burundi

Labani og

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2020
Posts
22,854
Reaction score
32,657
Nchi za Burundi na Tanzania kesho zinatarajia kuzindua ujenzi wa Reli ya kisasa maeneo ya Musongati mkoani Burunga nchini Burundi na kuhudhuriwa na Viongozi kutoka Mataifa yote mawili.

Reli ya kisasa (SGR ) itakuwa ni fursa katika kukuza maendeleo kwa Burundi na Tanzania katika Biashara na usafirishaji wa Madini kutoka Musongati kupitia Bandari ya Dar es salaam.

Kutoka Tanzania viongozi ambao watahudhuria uzinduzi huo ni Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa na Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa.

Mbali ya Burundi Reli hiyo itaiunganisha nchi ya DR Congo katika kukuza uchumi wa nchi hiyo na Afrika Mashariki kwa ujumla.
#KitengeUpdates

Japo watu wanapinga lakini bado CCM kwenye maendeleo ni baba lao
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni

Now east Africa it's going to be connected na Tanzania

Haya ni maendeleo ya kimkakati
1755270731259.jpg


Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Mkoloni alipojenja reli ya MGR aliangalia mazao ya ndani mkonge, pamba, tumbaku, chai

Je SGR yetu mazao gani ya ndani yatakayoibeba reli hii ya matrilioni ya shilingi au tunategemea mazao kutoka Burundi, Rwanda na DR Congo yaibebe reli hii yetu kwa asilimia 80 %

Historia inaonesha reli ya TAZARA imeyumba sana kwa kutegemea mazao ya Zambia, nchi hiyo ilivyokengeuka ikaelelea bandari za Mozambique, South Africa na Namibia badala ya Dar es Salaam.

Wakati reli ya mkoloni iliyokuwa ya MGR imebeba visheni ya mazao ya ndani kuibeba pakubwa haikuyumba kiasi hicho ya kwenda Kigoma na Mwanza.

Ila reli ya MGR ya Tanga, Mombo, Moshi, Arusha, pia kipande cha reli MGR toka DSM, Ruvu, Korogwe iliyumba pale mkonge, chai, kahawa mazao na viwanda vyake yalipotelekezwa na wakulima wa Tanzania.

Je reli mpya ya SGR inakwenda na visheni gani ya kuanzisha mashamba makubwa ya alizeti, karanga ktk corridor / mtandao wa reli pia viwanda vikubwa vya bidhaa vipi vitajengwa haraka pembezoni mwa reli kama maeneo ya Buguruni, Pugu, Gerezani jijini Dar es Salaam hadi Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Kigoma, Simiyu, Shinyanga, Mwanza, Musoma hadi Bukoba
 
Ujenzi wa reli haujawahi kuwa moja kati ya mambo yaliyotiliwa shaka na wananchi, japo walitilia shaka uwezo wa serikali kuiendesha kwa faida, watanzania kwa umoja wetu tunaiunga mkono serikali pale inapofanya jambo la maana kama hilo la reli ya kuunganisha nchi yetu na mataifa mengine yanayotegemea bandari yetu, sasa isiishie kujengwa kwa matrilioni ya pesa za walipa kodi halafu yaishie kutafunwa na mafisadi wachache kwa kigezo cha kuichangia ccm hela ya kuzugia, angalau mbgetukata tozo kujenga mradi kama huo tungewaelewa, ila tu mtuhakikishie ufanisi wenye tija kwa taifa, Mungu ibariki TANZANIA
 
Kitu ambacho Mjomba Magu alikisahau ilikuwa kuweka reli kwenye daraja la Kigongo Busisi.
Na kama angeonyesha dhamira hiyo Mseveni Kagame wangefanikisha haraka ndoto za kuunganiswa central corridor kwa rail line hadi kwao na labda hata DRC.
Kufanikisha ujenzi wa reli hiyo inahitajika kufua chuma cha pua katika mradi wa Liganga-Mchuchuma ili kupunguza gharama za ujenzi kwa kutumia raslimali zetu.
Lakini yote haya hayaendi kasi kwa kuendekeza kirusi kinachoitwa NDC yaani kwa lugha sahihi ni kimeo hakifai kuwepo ivunjwe inakula pesa tokea kuundwa kwake hadi leo.Kwa miaka zaidi ya 50 wameshindwa kufanikisha uchanjuaji wa chuma lakini Raisi Museveni kwa muda mfupi Uganda ina tengeneza chuma kutoka kwenye udongo wa chuma kama kule Liganga-Mchuchuma.
Na anatumia mkaa wa mawe wetu kutokea maeneo hayo hayo ya kusini mwa Tanzania kuzalisha chuma.
Wamekuja tena hao NDC eti wanahitaji kufanya visibility study upya.
Nadhani Kassim Majaliwa yupo sahihi watu sampuli hiyo to enroll kwenye Vactional training centres wapate ujuzi sahihi.
Mama achana na NDC ni mchwa kwa hazina ya taifa.
 
Mkoloni alipojenja reli ya MGR aliangalia mazao ya ndani mkonge, pamba, tumbaku, chai

Je SGR yetu mazao gani ya ndani yatakayoibeba reli hii ya matrilioni ya shilingi au tunategemea mazao kutoka Burundi, Rwanda na DR Congo yaibebe reli hii yetu kwa asilimia 80 %

Historia inaonesha reli ya TAZARA imeyumba sana kwa kutegemea mazao ya Zambia, nchi hiyo ilivyokengeuka ikaelelea bandari za Mozambique, South Africa na Namibia badala ya Dar es Salaam.

Wakati reli ya mkoloni iliyokuwa ya MGR imebeba visheni ya mazao ya ndani kuibeba pakubwa haikuyumba kiasi hicho ya kwenda Kigoma na Mwanza.

Ila reli ya MGR ya Tanga, Mombo, Moshi, Arusha, pia kipande cha reli MGR toka DSM, Ruvu, Korogwe iliyumba pale mkonge, chai, kahawa mazao na viwanda vyake yalipotelekezwa na wakulima wa Tanzania.

Je reli mpya ya SGR inakwenda na visheni gani ya kuanzisha mashamba makubwa ya alizeti, karanga ktk corridor / mtandao wa reli pia viwanda vikubwa vya bidhaa vipi vitajengwa haraka pembezoni mwa reli kama maeneo ya Buguruni, Pugu, Gerezani jijini Dar es Salaam hadi Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Kigoma, Simiyu, Shinyanga, Mwanza, Musoma hadi Bukoba
Swali zuri .....

SGR itaanzisha direct route Kati ya dare es salaam ( Bandarini)......to Burundi

It means mizigo yote ya Burundi itapitia Bandari ya dar

.....itakuwa utalii

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Ujenzi wa reli haujawahi kuwa moja kati ya mambo yaliyotiliwa shaka na wananchi, japo walitilia shaka uwezo wa serikali kuiendesha kwa faida, watanzania kwa umoja wetu tunaiunga mkono serikali pale inapofanya jambo la maana kama hilo la reli ya kuunganisha nchi yetu na mataifa mengine yanayotegemea bandari yetu, sasa isiishie kujengwa kwa matrilioni ya pesa za walipa kodi halafu yaishie kutafunwa na mafisadi wachache kwa kigezo cha kuichangia ccm hela ya kuzugia, angalau mbgetukata tozo kujenga mradi kama huo tungewaelewa, ila tu mtuhakikishie ufanisi wenye tija kwa taifa, Mungu ibariki TANZANIA
Hapana mkuu.... strategic projects bado ninaendelea kumiminika

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom