Mitandao ya kijamii na demokrasia; Changamoto, fursa na nini cha kufanya?

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1571725605008.png
Moja ya nguzo muhimu kwenye demokrasia ni pamoja na watu kuwa na uhuru wa kutoa maoni bila kuvunja sheria, kupata taarifa na kushiriki kwenye mijadala kuhusu masuala mbalimbali. Maendeleo ya ‘internet ‘ hususan mitandao ya kijamii yamerahisisha hili.

Hata hivyo, kama ilivyo kwa kila fursa;fursa hii imekuja na changamoto zake. Moja wapo ni baadhi ya watumiaji wake kueneza habari za uongo, uchochezi, taharuki n.k ama kwa bahati mbaya ama kwa makusudi.Hii imekuwa ndio changamoto kubwa ya maendeleo haya.

Changamoto kubwa zaidi inakuja pale unapoanza mjadala juu ya namna ya kuishukulikia changamoto ya hapo juu. Shida inaanza pale tunapodhani tatizo ni mitandao ya kijamii yenyewe na wakati kimsingi, tatizo ni watu “Jamii yenyewe” . Kama jamii tukishakosea kutafsiri tatizo, maana yake pia tutakuja na mapendekezo ya ‘solution’ ambayo si sahihi vile vile.

Mitandao ya kijamii ni kama Ndege, Treni za umeme au basi. Vitu hivyo kwa u-asili wake, ni vitu vizuri lakini pia vinaweza kuleta maafa makubwa kama ikitokea kuna mtumiaji ambaye ana matatizo. Kwa mfano mlevi au kichaa akitumia chombo kimojawapo, anaweza kuua mamia au maelfu ya watu, na tumeshuhudia matukio kama hayo mara nyingi tu.

Hata hivyo, hatuwezi kusema, kwa kuwa kuna watu wenye matatizo wanaotumia vyombo hivyo; basi solution visitumike, au kwa kuwa vinabeba watu wengi na ikitokea madhara watu wengi wanaathirika ndani ya sekunde, basi tutafute viji - chombo ambavyo vitakuwa vinabeba watu wawili wawili ili hata ikitokea tatizo waathirike wachache. Nafikiri hapo kutakuwa na tatizo la kimtizamo.

Kwa hiyo mitandao ya kijamii ni muhimu sana hasa kama tunaamini demokrasia ndio mfumo bora kuliko mingine. Ni muhimu kuelewa kwamba chenye tatizo ni baadhi ya watumiaji na sio mitandao.Pia, Watumiaji tunaowaona ni ‘reflexion’ ya jamii tuliyo nayo; kwa hiyo, tukitaka kupata matokeo bora, tuongeze nguvu kwenye kubadili mitizamo ya kijamii kwani yale wayaandikayo watu mitandaoni, ni mwangwi wa yale wayawazayo vichwani mwao.
 
Jana taarifa ya habari Tbc saa 2 usiku, mwandishi Zacharia, alijaribu kuwabana maswali ya ajabu , mwakilishi TCRA na Police, ... kwamba kufuatia tetesi afya ya Rais, kwanini sheria, taasis hazikuweza kuzuia mtiririko wa taarifa! Walimjibu kwa hekima sana. Atafute kiki nyingine pale u dc bado.
Hayakuwa majibu kwa kifupi walishindwa kujibu swali
 
Kuna kitu kimoja cha muhimu sana umekisema
Hata hivyo, hatuwezi kusema, kwa kuwa kuna watu wenye matatizo wanaotumia vyombo hivyo; basi solution visitumike

Viongozi wote wangekua wanafikiria hivyo labda tungekua tumeendelea, kuna watu wajinga wapo tayari kuzuia kitu ambacho ni kizuri kabisa kwa sababu tu mtu anaweza kukitumia vibaya. Kuzuia hua sio solution, in fact inaleta matatizo zaidi.

Mfano, tanzania kua na youtube channel unaambiwa ulipe leseni 1mil kila mwaka, watanzania wenye uwezo wa kulipa hiyo hela ni wachache mno, nchi za nje mtu anaanza leo kufungua channel bure, ghafla inatokea watu wamependa content yake anajikuta amepata subs kibao anaanza kupiga hela ndefu, wapo watu kutengeneza $1,000 kila siku kitu cha kawaida sana. Ila kwa Tanzania hata hiyo chance ya kuanza tu imeondolewa, kisa tu mtu ana uwezo wa kutengeneza channel kupondea serikali. WTF? hata China na ubabe wao hawajafanya hiki. TCRA inaongoza kwa vilaza.

Zuia zuia, funga funga zimekua nyingi, kila kitu wakiona tu kinaweza tumika vibaya, cha kwanza kabisa unasikia funga, hata kama kitaathiri watu maelfu na kufunga biashara za watu, wao wanaona sawa tu kwa sababu haziwa-affect wao. Hii njia ya kufikiri sijui ilitoka wapi.

In the end, watu wema ni wengi zaidi kuliko wabaya, hua naamini hivyo na hili limekua proved again and again, ndiyo mtu moja anaweza vuruga mtandao mzima ila haimaanishi mazuri yote yatupwe pembeni sababu hiyo tu.
 
Ni kosa kimantiki kudhani watu wa mitandaoni na watu wa mitaani ni tofauti. Ndio hao hao na kwa kasi ya ukuaji wa teknolojia, miaka michache ijayo takribani jamii nzima itakuwa imehamia mtandaoni na itakuwa haina tena ulazima wa kukutana ana kwa ana. Hapo mikutano ya siasa itakuwa inafanyika rasimi mtandaoni, watu wanahudhuria mtandaoni na kila kitu kinaishia huko huko. Huu ni kama upepo, kuuzuia ni ngumu kwa sababu unavuma kutoka pande za mbali. Suala ni kufikiria ni kwa vipi tutaweza ku 'Manage' tusipeperushwe.
 
Ni kosa kimantiki kudhani watu wa mitandaoni na watu wa mitaani ni tofauti. Ndio hao hao na kwa kasi ya ukuaji wa teknolojia, miaka michache ijayo takribani jamii nzima itakuwa imehamia mtandaoni na itakuwa haina tena ulazima wa kukutana ana kwa ana. Hapo mikutano ya siasa itakuwa inafanyika rasimi mtandaoni, watu wanahudhuria mtandaoni na kila kitu kinaishia huko huko. Huu ni kama upepo, kuuzuia ni ngumu kwa sababu unavuma kutoka pande za mbali. Suala ni kufikiria ni kwa vipi tutaweza ku 'Manage' tusipeperushwe.
jiwe na wanaomwabudu ni washamba sana.wanatakiwa wende na wakati bila kuchukia mawazo mbadala yaliyosheheni weledi.kinyume na hapo anaturudisha nyuma miaka 50 au old stone age
 
FACTS AMBAZO NI MUHIMU KUZIJUA KWA HARAKA HARAKA

  • Mitandao ya kijamii kama ilivyo Demokrasia ni kama upepo; kuna siku unaenda kusini mara upo kasikazini. Kuna siku utakusaidia kukupeperusha lakini kuna siku utakupiga usoni.

  • Demokrasia bado inaamika ndio mfumo bora zaidi duniani ukiilinganisha na mifumo mingine ndio maana hata nchi zisizo za kidemokrasia zinadai ni za kidemokrasia.

  • Internet inakuwa kwa kasi, mitandao ya kijamii pia inakuwa kwa kasi, itafika mahali uhusiano wa kijamii utapotea kabisa na watu watakuwa wanakutana kwenye mitandao ya kijamii na kuachana huko huko na hayo ndio yatakuwa mahusiano rasmi ya kijamii.

  • Nchi zinazoendelea sio tu kuwa hazina uwezo wa kudhibiti ‘internet’ na yatokanayo(kwa kuwa sio wao walioasisi vitu hivi) lakini pia hata wangeweza;kufanya hivyo hasara ni kubwa kuliko faida.

  • Nchi zilizoendelea haziwezi kukubali kwa namna yoyote abolition ya internet na mazao yake kwa sababu ya kiuchumi na kisiasa.

  • Kinachokubalika na watu wote ni na kuaminika kuwa kinaweza kuwa na matokeo chanya ni usimamizi wa karibu wa maudhui “Moderation”

  • Ustaarabu, uelewa, na dhamira ya jamii husika inakuwa ‘reflected’ kwenye mitandao.Kwa hiyo mitandao inatusaidia tu kujua jamii inafikiria nini, kivipi na kwa nini lakini hata isingekuwepo, haimaanishi jamii haifikirii inavyofikiria. Cha msingi ni kubadili mitizamo ya jamii husika.

  • Watu walioko kwenye mitandao ya kijamii ndio hao hao walioko mitaani. Kwa hiyo tunayoyaona mtandaoni “Roughly” ndio jamii hiyo ilivyo.Ni kosa kubwa sana kimantiki kuamini kuna watu wa mitandaoni wa watu wa mtaani, kimsingi ndio hao hao.

  • Watu wanaodhani wana mawazo mazuri wayatoe ili ya “Neutralize” yanayofikiriwa kuwa ni mawazo mabaya. Kama watu wanaodhani wana mawazo mazuri hawayatoi, kwanza hakuna atakayejua kama hayo mawazo “Mazuri” yaliwahi kuwepo, na pili mawazo yanayoaminika kuwa mabaya yatakuwa yakitamalaki na hakuna atakayejua kuwa yaliwahi kuwewepo mawazo mbadala.

  • Kuna vitu vinatokea hatuna uwezo wa kuvifanya visitokee kwa kuwa wanaofanya vitokee pia sio sisi. Vitu hivyo ni mfano wa misimu.Mara baridi mara joto. Badala tu ya kulalamika ‘Hili baridi litatuua’ wakati hatuna uwezo wa kuliondoa, ni bora kufikiri tunawezaje kulitumia kwa namna ‘positive’
 
Back
Top Bottom