Misikiti 80 kufungwa Tunisia

Status
Not open for further replies.

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
33,569
Reaction score
53,583


Utawala nchini Tunisia unasema kuwa utafunga misikiti 80 katika kipindi cha wiki moja inayokuja kwa madai ya kuhubiri chuki na jihad.


Zaidi ya watalii 2500 kutoka Uingereza wametoroka na kurejea makwao


Hii ni kufuatia shambulizi lililofanyika kwenye hoteli moja hapo jana ambapo takriban watu 39 wengi wao wakiwa raia wa mataifa ya ulaya waliuawa na mwanamme mmoja aliyejifanya kuwa mtalii.



Asili mia kubwa ya wahasiriwa wa mkasa huo ni raia wa Uingereza


Wapiganaji wanaoshirikiana na wanamgambo wa Kundi la kiislamu la Islamic State wamesema kuwa wao ndio waliotekeleza shambulizi hilo.



Miili ya watalii ilikuwa imetapakaa ufukweni


Waziri mkuu nchini Tunisia Hanib Essid anasema kuwa misikiti hiyo ndio iliokuwa ikitumika kueneza propaganda na kuunga mkono ugaidi.




Waziri mkuu ametangaza kuwa misikiti hiyo ndiyo imekuwa ikihubiri Jihad


Hali ya usalama umeimarishwa maradufu katika maeneo mengi mjini Tunis na karibu na majengo yenye watalii wengi.




Mpiganaji mmoja alijifanya kuwa mtalii kabla ya kuwafyatulia risasi watalii ufukweni
Tayari wanajeshi wa akiba wameamrishwa kuripoti mara moja katika kambi za jeshi zilizoko karibu nao.
http://www.bbc.com/swahili/habari/2015/06/150627_tunisia_attack?ocid=socialflow_facebook

 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…