Mishakaki ya Paka

Khaaa! Hadi nahisi kichefuchefu.
Ashtakiwe aisee kama sheria inaruhusu.
 
Nilisikia hii kitu jamani puuuuh disgusting..mishikaki mie basi.looh!
na anaongea huku akicheka as if anachofanya ni sifa.
Je watu wangapi watakuwa wamedhurika bila kujua sababu ni nini?
Pamoja na kwamba kuna nchi wanakula paka ila wanapitia process mpaka ije kufaa kuliwa sio kama anavyofanya jamaa huyo..
Ila hii yote ni dhiki..kama kungekuwa na ajira za kutosha asingefanya hivi.duh.Mungu atuepushe.
 
hee! haya bwana ingawa anajasiria kupata mali, lakini anshitua kidogo, ila kama wanaokula wanaona ni tamu na haijawadhuru kwa muda wote huo, basi aendelee na biashra cha muhimu awaeleze watu ukweli wa aina ya nyama anyoiuza.
 
Naona kuwa Clouds FM walipaswa kumripoti huyu jamaa kwenye vyombo vya sheria. Haiyumkiniki kumuhoji mvunja sheria na kumuacha aendelee kuvunja sheria tena kwa kumuhifadhi jina lake.

Tuliopita Manzese jana jioni tuliona kuwa watu wamegoma kabisa kula mishikaki wakihofia kula paka. Hii imewaharibia kweli wale wanaofanya biashara halali.
 

Hawa wanyama wana soko sana kule china, kwa hiyo ni msosi wa kawaida tu ni kama sungura
 
Kwani wanaokula umbwa, unyoka, upanya mbona hamsemi , unyau tu ndo maneenoooooooo acheni hizo wananchi
 

Haya ndio yanayonifanya niamini kwamba huyo jamaa anaweza kabisa kuchinja paka na kuuza mishikaki yake, kwa sababu yeye mwenyewe ni kama akili hazimtoshi, nilikuwa nasikiliza kipindi siku hiyo, naamini bonge hakuwa anadanganya, swali la kujiuliza ni labda bonge alipataje habari za huyo mtu mpaka akaenda kumhoji? kama ni taarifa kutoka kwa raia wema ina maana haikuwa siri basi
 
Is this true??????????????????????? Or my lord!!! Ni mburahati ipi maana kuna kipindi nilikuwa naenda kwa mshkaji wangu anakaa mburahati bondeni. Ikawa tunatoka na kwenda kula mishkaki maeneo ya kijiweni.....ni wapi huyu jamaa alikuwa???
Haa haa haaaa!! Mkuu, vipi unataka ujitapishe kabisa au?! Hatari kweli kweli.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…