Hivi CCM imeshindwa kabisa kuilazimisha Serikali yao ipeleke mafao ya wastaafu pspf? Kazi ya chama ni nini?
Hao pspf sashivi wameshindwa kabisa, Ukiwapigia simu wanaweza wasipokee siku nzima, siku wakipokea unapewa majibu ya mkatao tu.
Na ukifanikiwa kuunganishwa na watu wa uhasibu, angalau wao ndio wanakupa majibu ya hali ilivyo kwenye file la mtu wenu. Kwamba hazina haijapeleka makato, ila unaweza kuwasiliana na CUSTOMER CARE MANAGER, yeye atajua namna ya kushughulikia madai yenu kwa haraka.
Tatizo sasa, ni namna ya kumpata huyo Customer Care Manager, mara uambiwe hayupo ofisini, mara uambiwe simu yake inaita tu bila majibu. Jamani tufanyeje sasa sisi watu wa huku mbali, na ndugu yetu ni mahututi? BACK TANZANIA